Wafilipi 2
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Iweni katika Umoja na Msaidiane
2 Fikirini kuhusu kile ambacho tulichonacho kwa sababu tunamilikiwa na Kristo: hamasa aliyotuletea, faraja ya upendo wake, ushirika katika Roho wake, huruma na wema aliotuonyesha. Ikiwa mnazifurahia baraka hizi, 2 basi fanyeni yale yatakayoikamilisha furaha yangu: iweni na nia moja na mpendane ninyi kwa ninyi. Iweni na umoja katika malengo yenu na katika kufikiri kwenu. 3 Msiruhusu ubinafsi au kiburi viwe dira yenu. Badala yake muwe wanyenyekevu mkiwathamini wengine kuliko ninyi wenyewe. 4 Kila mmoja wenu asijishugulishe kwa mema yake yeye mwenyewe bali kwa mema ya wengine.
5 Hivi ndivyo mnapaswa kufikiri, kuhisi na kutenda katika maisha yenu kwa pamoja, kama vile Kristo Yesu alivyofikiri:
6 Alikuwa sawa na Mungu katika namna zote,
lakini hakufikiri kwamba kuwa sawa na Mungu
kilikuwa kitu cha manufaa kwake.
7 Badala yake, aliacha kila kitu,
hata sehemu yake pamoja na Mungu.
Akakubali kuwa kama mtumwa,
akiwa katika umbo la binadamu.
Wakati wa maisha yake kama mtu,
8 Alijinyenyekeza na akawa mtiifu kabisa kwa Mungu,
hata jambo hilo liliposababisha kifo chake msalabani.
9 Hivyo ndiyo sababu Mungu alimpa mahali pa heshima sana,
na akampa jina lililo kuu kuliko majina yote.
10 Hivyo kila mtu atasujudu kumheshimu Yesu.
Kila mmoja aliye mbinguni, duniani na wale walio chini ya dunia.
11 Wote watakiri kwamba, “Yesu Kristo ni Bwana,”
na hili litamtukuza Mungu Baba.
Iweni Kama Mungu Anavyotaka
12 Rafiki zangu wapendwa, daima mnatii yale mliyofundishwa. Kama mlivyotii nilipokuwa pamoja nanyi, ni muhimu zaidi na zaidi kwamba mtii wakati huu ambapo sipo pamoja nanyi. Hivyo ni lazima mwendelee kuishi katika namna inayoleta maana kwa wokovu wenu. Fanyeni hivi kwa wingi wa heshima na utii kwa Mungu. 13 Ndiyo, Mungu ndiye anayetenda kazi ndani na miongoni mwenu. Anawasaidia ninyi kutaka kutenda yanayomfurahisha, naye anawapa nguvu ya kuyatenda.
14 Fanyeni mambo yote pasipo kulalamika wala kubishana. 15 Nanyi mtakuwa watoto wa Mungu wasiolaumiwa na wasio na hatia. Ijapokuwa mnaishi mkiwa mmezungukwa na watu wasio waaminifu wasiojali thamani haki. Katikati ya watu hao mnang'ara kama mianga katika ulimwengu wenye giza, 16 nanyi mnawapa mafundisho yanayotoa uhai. Hivyo nitaona fahari juu yenu wakati Kristo atakapokuja tena. Ninyi ndiyo mtakaothibitisha kuwa kazi niliyoifanya haikukosa matokeo, ya kwamba nilishindana mbio na nikashinda.
17 Imani yenu inayatoa maisha yenu kama sadaka katika kumtumikia Mungu. Hata kama ni kweli kwamba sasa ninajimimina mimi mwenyewe kama sadaka ya kinywaji pamoja na sadaka yenu, ninayo furaha, na nitawashirikisha ninyi nyote furaha yangu. 18 Ninyi pia mnapaswa kufurahi na kunishirikisha furaha yenu.
Habari Kuhusu Timotheo na Epafrodito
19 Kwa baraka za Bwana Yesu, ninategemea kuwa nitamtuma Timotheo kwenu hivi karibuni. Naye atarejesha kwangu taarifa kuhusu ninyi ili nifurahi. 20 Sina mtu mwingine yeyote kama Timotheo, ambaye kwa dhati kabisa anayajali mambo yanayowahusu. 21 Wengine wote wanajishughulisha na maisha yao wenyewe. Hawajali kazi ya Yesu Kristo. 22 Mnafahamu Timotheo amejithibitisha kuwa ni mtu wa aina gani. Ametumika pamoja nami katika kuhubiri Habari Njema kwa njia ambavyo mwana angemtumikia baba yake. 23 Ninategemea kumtuma aje kwenu haraka baada ya kujua yatakayonipata. 24 Bwana hunifanya niwe jasiri ili niweze pia kuja kwenu haraka.
25 Kwa sasa, nadhani ni lazima nimrudishe Epafrodito kwenu. Ni mtumishi na mtenda kazi pamoja nami na askari mwenzangu katika jeshi la Bwana. Nilipotaka msaada, mlimtuma kwangu. Kama mjumbe wenu, alinihudumia mahitaji yangu. 26 Lakini sasa anataka kuwaona ninyi nyote tena. Ana wasiwasi sana kwa sababu mlisikia kuwa alikuwa mgonjwa. 27 Alikuwa mgonjwa karibu ya kufa. Lakini Mungu alimsaidia yeye na mimi ili nisiwe na huzuni zaidi. 28 Hivyo ninataka sana kumtuma kwenu. Ili mtakapomwona, mfurahi. Nami nitaacha kuwa na wasiwasi juu yenu. 29 Mkaribisheni kwa furaha nyingi katika Bwana. Waheshimuni watu kama Epafrodito. 30 Anapaswa kuheshimiwa kwa sababu alikaribia kufa akifanya kazi kwa ajili ya Kristo. Aliyaweka maisha yake katika hatari ili aweze kunisaidia. Ni msaada ambao msingeweza kunisaidia.
Wafilipi 2
Neno: Bibilia Takatifu
Unyenyekevu Na Ukuu Wa Kristo
2 Ikiwa mmepata faraja kwa kuwa mmeunganishwa na Kristo, kama mmevutwa na upendo wake na kushiriki Roho wake, kama mnaoneana huruma na kusaidiana; 2 basi kamilisheni furaha yangu kwa kuwa na nia moja, upendo mmoja na kuwa wamoja katika roho na shabaha. 3 Msifanye jambo lo lote kwa ajili ya ubinafsi au kwa kujiona, bali kuweni wanyenyekevu, mkiwahesabu wengine kuwa bora kuliko ninyi. 4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu ajishughulishe pia kwa faida ya wengine. 5 Muwe na nia kama ile aliyokuwa nayo Kristo Yesu; 6 yeye kwa asili alikuwa sawa na Mungu, lakini hakuona kwamba kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kush ikilia sana. 7 Bali alikubali kuacha vyote, akachukua hali ya mtumishi, akazaliwa na umbo la wanadamu. 8 Alipochukua umbo la mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii mpaka kufa, tena kifo cha msalaba. 9 Kwa sababu hiyo, Mungu alimwinua juu kabisa, akampa jina ambalo ni kuu kuliko majina yote; 10 ili kwa jina la Yesu, kila goti lipigwe, mbinguni na duniani na kuzimu; 11 na kila ulimi ukiri kwamba Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu
Ng’aeni Kama Nyota
12 Basi rafiki zangu wapendwa, kama ambavyo mmekuwa mkitii nilipokuwa nanyi, nawasihi mwendelee kunitii vivyo hivyo, na hata zaidi sasa kwa kuwa sipo pamoja nanyi. Endeleeni kufanya bidii kwa ajili ya wokovu wenu huku mkitetemeka na kuogopa. 13 Kwa maana ni Mungu ambaye anatenda kazi ndani yenu, akiwapa nia ya kutimiza mapenzi yake na kuwawezesha kutenda yale yanayompendeza 14 Fanyeni mambo yote bila manung’uniko au mabishano 15 ili msiwe na lawama au kosa bali muwe wana wa Mungu wasio na kasoro katika ulimwengu uliopotoka, mking’aa kama nyota angani, 16 na kusisitiza neno la uzima. Mkifanya hivyo siku ya Kristo nitajisi fia kwamba sikupiga mbio au kufanya kazi bure. 17 Hata kama damu yangu itamwagwa kama sadaka juu ya dhabihu na huduma inayotokana na imani yenu, mimi ninafurahi na kushangilia pamoja nanyi nyote. 18 Vivyo hivyo, nanyi pia mnapaswa kufurahi na kushangilia pamoja nami.
Safari Ya Timotheo Na Epafrodita
19 Nina matumaini katika Bwana Yesu ya kumtuma Timotheo hivi karibuni aje kwenu, ili nipate habari za kunitia moyo kutoka kwenu. 20 Sina mtu mwingine hapa kama yeye, anayewatakieni mema kwa moyo wote. 21 Wengine wanajishughulisha zaidi na mambo yao wenyewe na hawajali lo lote kuhusu kazi ya Yesu Kristo. 22 Lakini ninyi wenyewe mnajua jinsi Timotheo alivyojithibit isha, kwa maana amefanya kazi ya Injili pamoja nami kama vile mtoto na baba yake. 23 Kwa hiyo, natumaini kumtuma Timotheo kwenu mara tu nipatapo habari kuhusu mambo yangu yatakavyokuwa. 24 Nami naamini katika Bwana kwamba mimi mwenyewe nitakuja kwenu hivi karibuni.
25 Nimeona vema kumrudisha ndugu yangu Epafrodita kwenu. Yeye ni mtumishi na askari mwenzangu, ambaye pia ni mjumbe wenu mliyemtuma anihudumie katika mahitaji yangu. 26 Yeye ana hamu kuwaoneni ninyi nyote, na amesikitishwa kwa sababu mlipata habari kwamba alikuwa mgonjwa. 27 Hakika alikuwa mgonjwa, tena karibu ya kufa. Lakini Mungu alimhurumia, na si yeye tu, bali hata na mimi alinihurumia, nisipatwe na huzuni juu ya huzuni . 28 Kwa hiyo napenda kumtuma kwenu ili mtakapomwona kwa mara nyingine, mpate kufurahi, na mimi nipunguziwe wasiwasi wangu. 29 Kwa hiyo mpokeeni katika Bwana kwa furaha kubwa; na wapeni heshima watu kama hawa. 30 Kwa maana alikaribia kufa kwa ajili ya kazi ya Kristo; alihatarisha maisha yake ili aweze kunipa msaada ambao ninyi msingeweza kunipa.
Филипяни 2
Библия, нов превод от оригиналните езици (с неканоничните книги)
Иисус Христос – образец за живот
2 И тъй, ако имате насърчение чрез Христос, утеха от любовта, общение с Духа, ако имате милосърдие и състрадание – 2 (A)направете радостта ми пълна: имайте едни мисли, една и съща любов, бъдете единодушни и единомислени. 3 (B)Не правете нищо от съперничество или от тщеславие, но нека всеки смирено да смята другия за по-горен от себе си. 4 Не се грижете всеки само за себе си, но и за другите.
5 Вие трябва да имате същите мисли, каквито е имал Иисус Христос.
6 (C)Той, Който беше Бог по природа[a], не се възползва от равенството си с Бога, 7 (D)но унизи Себе Си, като стана служител и се уподоби на човек. А когато се яви като човек, 8 Той смири Себе Си и стана послушен дори до смърт – до смъртта на кръста. 9 (E)Затова Бог Го извиси и Му даде име, което е над всяко име, 10 (F)тъй че в името на Иисус да преклони колене всичко, което е на небето, на земята и под земята, 11 и всяка уста да изповяда за слава на Бог Отец: „Иисус Христос е Господ.“
Усърдие в доброто
12 Затова, възлюбени мои, както винаги сте послушни – не само в мое присъствие, но много повече сега, когато отсъствам, – постигайте спасението си със страх и трепет, 13 защото Бог е, Който подтиква и да искате, и да действате според благата Му воля. 14 Всичко вършете без ропот и съмнение, 15 (G)за да бъдете безукорни и чисти, непорочни Божии деца посред опак и развратен род, посред който сияете като светила във вселената, 16 (H)отстоявайки словото на живота за моя похвала в Христовия ден, че не съм тичал напразно и не съм се трудил напразно, 17 (I)но макар да се принасям като жертвено възлияние в служба на вярата ви, аз се радвам и споделям радостта на всички вас. 18 Така също и вие се радвайте и споделяйте моята радост.
Тимотей и Епафродит – апостолски сътрудници
19 Изразявам надежда чрез Господ Иисус скоро да изпратя при вас Тимотей, тъй че, като узная как сте, да се утеша духом. 20 Защото нямам никой друг, който като мене[b] така искрено да се грижи за вас, 21 (J)докато всички търсят своето, а не онова, което е на Иисус Христос. 22 А неговата изпитана вярност вие знаете – както син с баща си, така и той заедно с мене служи на благовестието. 23 И тъй, надявам се да го изпратя веднага, щом узная какво ще стане с мене, 24 (K)а съм убеден чрез Господ, че и сам скоро ще дойда при вас.
25 Намерих обаче за нужно да изпратя при вас брат Епафродит, мой сътрудник и съратник, изпратен от вас, за да ми помага в моите нужди. 26 Той копнееше за всички ви и дълбоко скърбеше, че бяхте чули за неговото заболяване. 27 Да, той беше смъртно болен, но Бог му оказа милост, и то не само на него, но и на мене, за да не ми се трупа скръб върху скръб. 28 Затова го изпратих по-скоро, та като го видите пак, да се зарадвате и аз да бъда по-малко наскърбен. 29 И така, приемете го в името на Господа с пълна радост и към такива братя се отнасяйте с почит, 30 понеже за Христовото дело той изложи на опасност живота си дори до смърт, за да ви замести в служението поради вашето отсъствие.
Philippians 2
King James Version
2 If there be therefore any consolation in Christ, if any comfort of love, if any fellowship of the Spirit, if any bowels and mercies,
2 Fulfil ye my joy, that ye be likeminded, having the same love, being of one accord, of one mind.
3 Let nothing be done through strife or vainglory; but in lowliness of mind let each esteem other better than themselves.
4 Look not every man on his own things, but every man also on the things of others.
5 Let this mind be in you, which was also in Christ Jesus:
6 Who, being in the form of God, thought it not robbery to be equal with God:
7 But made himself of no reputation, and took upon him the form of a servant, and was made in the likeness of men:
8 And being found in fashion as a man, he humbled himself, and became obedient unto death, even the death of the cross.
9 Wherefore God also hath highly exalted him, and given him a name which is above every name:
10 That at the name of Jesus every knee should bow, of things in heaven, and things in earth, and things under the earth;
11 And that every tongue should confess that Jesus Christ is Lord, to the glory of God the Father.
12 Wherefore, my beloved, as ye have always obeyed, not as in my presence only, but now much more in my absence, work out your own salvation with fear and trembling.
13 For it is God which worketh in you both to will and to do of his good pleasure.
14 Do all things without murmurings and disputings:
15 That ye may be blameless and harmless, the sons of God, without rebuke, in the midst of a crooked and perverse nation, among whom ye shine as lights in the world;
16 Holding forth the word of life; that I may rejoice in the day of Christ, that I have not run in vain, neither laboured in vain.
17 Yea, and if I be offered upon the sacrifice and service of your faith, I joy, and rejoice with you all.
18 For the same cause also do ye joy, and rejoice with me.
19 But I trust in the Lord Jesus to send Timotheus shortly unto you, that I also may be of good comfort, when I know your state.
20 For I have no man likeminded, who will naturally care for your state.
21 For all seek their own, not the things which are Jesus Christ's.
22 But ye know the proof of him, that, as a son with the father, he hath served with me in the gospel.
23 Him therefore I hope to send presently, so soon as I shall see how it will go with me.
24 But I trust in the Lord that I also myself shall come shortly.
25 Yet I supposed it necessary to send to you Epaphroditus, my brother, and companion in labour, and fellowsoldier, but your messenger, and he that ministered to my wants.
26 For he longed after you all, and was full of heaviness, because that ye had heard that he had been sick.
27 For indeed he was sick nigh unto death: but God had mercy on him; and not on him only, but on me also, lest I should have sorrow upon sorrow.
28 I sent him therefore the more carefully, that, when ye see him again, ye may rejoice, and that I may be the less sorrowful.
29 Receive him therefore in the Lord with all gladness; and hold such in reputation:
30 Because for the work of Christ he was nigh unto death, not regarding his life, to supply your lack of service toward me.
© 2017 Bible League International
Copyright © 1989 by Biblica
Copyright by © Българско библейско дружество 2013. Използвани с разрешение.