Font Size
Waefeso 4:10-12
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Waefeso 4:10-12
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
10 Hivyo Kristo alishuka chini, na ndiye aliyekwenda juu. Alikwenda juu ya mbingu za juu zaidi ili avijaze vitu vyote pamoja naye. 11 Na Kristo huyo huyo aliwapa watu hawa vipawa: aliwafanya wengine kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kwenda na kuhubiri Habari Njema, na wengine kuwa wachungaji[a] ili wawafundishe watu wa Mungu. 12 Mungu aliwapa hao ili kuwaandaa watakatifu wa Mungu kwa ajili ya kazi ya huduma, kuufanya imara mwili wa Kristo.
Read full chapterFootnotes
- 4:11 wachungaji Kwa maana ya kawaida “kuwahudumia na kuwafundisha watu”.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Copyright © 2017 by Bible League International