Waebrania 1-3
Neno: Bibilia Takatifu
Ukuu Wa Mwana Wa Mungu
1 Hapo zamani Mungu alisema na baba zetu mara nyingi na kwa namna mbali mbali kwa kuwatumia manabii. 2 Lakini katika siku hizi za mwisho, amesema na sisi kwa njia ya Mwanae, ambaye alim chagua kuwa mrithi wa vitu vyote. Na kwa njia ya Mwanae, Mungu aliumba ulimwengu. 3 Yeye Mwana ni mng’ao wa utukufu wa Mungu na chapa halisi ya nafsi yake, naye huudumisha na kuuendeleza ulim wengu kwa neno lake lenye nguvu. Alipokwisha kuwapatia wanadamu utakaso wa dhambi, alikaa upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi aliye juu. 4 Kwa hiyo Mwana alikuwa mkuu zaidi kuliko malaika, kama ambavyo jina alilorithi kwa Mungu ni kuu kuliko jina la malaika ye yote.
5 Kwa maana ni malaika gani ambaye Mungu aliwahi kumwambia: “Wewe ni mwanangu; leo hii nimekuzaa”? Au tena: “Mimi nita kuwa Baba yake na yeye atakuwa Mwanangu”? 6 Na tena Mungu ana pomleta mwanae, mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, anasema: “Malaika wote wa Mungu wamwabudu yeye.” 7 Anapozungumza juu ya malaika anasema: “Anawafanya malaika wake kuwa upepo, watumishi wake kuwa ndimi za moto.” 8 Lakini kuhusu Mwana, anasema: “Kiti chako cha enzi, Wewe Mungu, kitadumu milele na milele, na haki takuwa fimbo ya ufalme wako. 9 Umependa haki na kuchukia uovu. Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuchagua wewe na kukuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.” 10 Pia anasema: “Hapo mwanzo , Wewe Bwana, uliweka misingi ya ulimwengu, na mbingu ni kazi ya mikono yako. 11 Vyote vitaangamia lakini wewe unadumu; vyote vitachakaa kama nguo, nawe 12 utavikunja kama vazi na kuvibadilisha. Bali wewe hubadiliki, na miaka yako haitakwisha kamwe. ” 13 Lakini ni malaika gani amewahi kumwambia, “Keti kulia kwangu mpaka niwafanye adui zako kuwa kiti cha kuwekea miguu yako”? 14 Malaika ni nani basi? Wao ni roho wa utumishi waliotumwa kuwahudumia wale watakaopokea wokovu.
Kuzingatia Mafundisho
2 Kwa hiyo, hatuna budi kuzingatia kwa makini mambo tuliyof undishwa tusije tukatanga-tanga mbali na yale tuliyosikia. 2 Kwa maana kama ujumbe ulioletwa na malaika ulithibitika kuwa kweli, na kila aliyeasi na kutokutii akaadhibiwa ilivyostahili, 3 sisi je? Tutaepukaje kama tusipojali wokovu mkuu namna hii? Wokovu huu kwanza ulitangazwa na Bwana, na ulithibitishwa kwetu na wale wal iomsikia. 4 Mungu pia aliushuhudia kwa ishara na miujiza na maaj abu mbalimbali, pamoja na karama za Roho Mtakatifu alizogawa kufuatana na mapenzi yake.
Wokovu Umeletwa Na Kristo
5 Maana Mungu hakuuweka ulimwengu ujao, tunaouzungumzia, chini ya mamlaka ya malaika. 6 Bali kama inavyothibitishwa katika sehemu fulani ya Maandiko, “Mwanadamu ni kitu gani hata umfi kirie, au mwana wa binadamu ni nani hata umjali? 7 Umemfanya kuwa chini kidogo ya malaika; wewe umemvika taji ya utukufu na heshima, 8 umemfanya kuwa mtawala wa vitu vyote.” Mungu ali poweka vitu vyote chini ya mamlaka ya mwanadamu, hakubakiza cho chote ambacho mwanadamu hakitawali. Lakini kwa wakati huu hatuoni kama kila kitu kiko chini ya mamlaka yake. 9 Lakini tunamwona Yesu, ambaye kwa muda mfupi alifanywa kuwa chini kidogo ya mal aika, sasa akiwa amevikwa taji ya utukufu na heshima kwa sababu aliteseka na kufa, ili kwa neema ya Mungu, aonje mauti kwa ajili ya watu wote.
10 Kwa maana ilikuwa ni sawa kabisa kwamba Mungu, ambaye kwa ajili yake na kwa uweza wake vitu vyote vimekuwepo, amfanye Mwan zilishi wa wokovu wao kuwa mkamilifu kwa njia ya mateso, ili awalete wana wengi washiriki utukufu wake. 11 Maana yule anayetakasa na wale wanaotakaswa, wote wanatoka katika uzao mmoja. 12 Ndio maana Yesu haoni aibu kuwaita wao ndugu zake, akisema: “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katikati yao nitakusifu.” 13 Na tena anasema, “Nitamwekea Mungu tumaini langu.” Na tena, “Niko hapa, mimi pamoja na watoto niliopewa na Mungu.”
Mungu.”
14 Basi, kwa kuwa watoto hao wana mwili na damu, yeye pia alishiriki katika ubinadamu wao, ili kwa kufa kwake apate kumwan gamiza yule mwenye mamlaka juu ya kifo, yaani shetani; 15 na hivyo awaweke huru wale ambao walikuwa utumwani maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa kifo. 16 Maana ni wazi kwamba hakuja kuwa saidia malaika bali kuwasaidia uzao wa Ibrahimu. 17 Kwa sababu hii ilibidi awe kama ndugu zake kwa kila hali, apate kuwa kuhani mkuu mwenye huruma na mwaminifu katika huduma ya Mungu, ili aweze kujitoa kama sadaka kwa ajili ya dhambi za watu. 18 Na kwa kuwa yeye mwenyewe ameteswa na kujaribiwa, anaweza kuwasaidia wanaoj aribiwa.
Yesu Ni Mkuu Kuliko Musa
3 Kwa hiyo, ndugu zangu watakatifu, ambao mmeshiriki wito wa mbinguni, mtafakarini Yesu, mtume na kuhani mkuu wa imani tunay oikiri.
2 Kwa maana Yesu alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemchagua, kama vile Musa alivyokuwa mwaminifu katika nyumba ya Mungu. 3 Lakini Yesu amehesabiwa kuwa anastahili utukufu zaidi kuliko Musa, kama vile mjenzi wa nyumba anavyopewa heshima zaidi kuliko nyumba aliyoijenga. 4 Maana kila nyumba hujengwa na mtu fulani bali aliyejenga vitu vyote ni Mungu. 5 Ni kweli kwamba Musa ali kuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, akishu hudia juu ya yale mambo ambayo Mungu angeyatamka baadaye, 6 lakini Kristo alikuwa mwaminifu katika nyumba ya Mungu kama mwana. Na sisi ni nyumba yake, ikiwa tutashikilia ujasiri wetu na lile tumaini tunalojivunia.
Jihadharini Na Kutokuamini
7 Kwa hiyo, kama Roho Mtakatifu asemavyo, “Leo, mkiisikia sauti yake, 8 msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama mlivyofanya wakati wa uasi , siku ile ya majaribio jangwani, 9 ambapo baba zenu walinijaribu wakaona kazi zangu kwa miaka arobaini. 10 Kwa hiyo kizazi kile kilinikasirisha, nikasema, ‘Mioyo ya watu hao imepotoka; hawajapata kujua njia zangu.’ 11 Katika hasira yangu nikaapa, ‘Hawataingia kwenye pumziko langu kamwe.’
12 Angalieni, ndugu zangu, asiwepo miongoni mwenu mtu ye yote mwenye moyo wa dhambi, usioamini, unaomfanya ajitenge na Mungu wa uzima. 13 Bali muonyane kila siku maadamu bado ni ‘ ‘leo” ili asiwepo mtu kati yenu anayefanywa mkaidi na udangany ifu wa dhambi. 14 Kwa maana sisi ni washiriki pamoja na Kristo iwapo tutashikilia tumaini letu la kwanza kwa uaminifu mpaka mwisho. 15 Kama Maandiko yalivyosema: “Leo mkiisikia sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu. Kama mlivyofanya wakati wa uasi.” 16 Ni nani hao waliosikia lakini wakaasi? Si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Musa? 17 Na ni nani waliom kasirisha Mungu kwa miaka arobaini? Si wale waliofanya dhambi wakafa jangwani? 18 Na ni nani ambao Mungu aliapa kuwa hawatain gia kwenye pumziko lake, isipokuwa wale waliokataa kutii? 19 Kwa hiyo tunaona kwamba walishindwa kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao. Pumziko La Sabato
Copyright © 1989 by Biblica