Add parallel Print Page Options

Ndipo wazee ishirini na nne na viumbe wenye uhai wanne wakaanguka chini kusujudu wakamwabudu Mungu, akaaye kwenye kiti cha enzi. Wakasema:

“Amina! Haleluya!”

Sauti ikatoka kwenye kiti cha enzi na kusema:

“Msifuni Mungu wetu,
    ninyi nyote mnaomtumikia!
Msifuni Mungu wetu,
    ninyi nyote mlio wadogo na wakubwa mnaomheshimu!”

Kisha nikasikia kitu kilichosikika kama kundi kubwa la watu. Kilikuwa na kelele kama mawimbi ya bahari au radi. Watu walikuwa wakisema:

“Haleluya!
    Bwana Mungu wetu anatawala.
    Ndiye Mwenye Nguvu, Mungu Mwenyezi.

Read full chapter