19 Basi malaika huyo akauzungusha mundu wake duniani akakata zabibu za dunia, akazitia ndani ya mtambo mkubwa wa kusindika zabibu wa ghadhabu ya Mungu. 20 Zabibu zikakamuliwa ndani ya mtambo huo wa kusindika zabibu uliokuwa nje ya mji, na damu ika tiririka kama mafuriko kutoka katika mtambo huo na urefu wa mafu riko hayo ulikuwa kama kilometa mia tatu, na kina chake kiasi cha meta moja na nusu.

Read full chapter