Font Size
Tito 1:4-6
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Tito 1:4-6
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
4 Nakuandikia wewe Tito, mwanangu halisi katika imani tunayoshiriki:
Neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu[a] Mwokozi wetu iwe nanyi.
Kazi ya Tito Krete
5 Nilikuacha kule Krete ili uweze kuyakamilisha yale yaliyokuwa yamebaki kufanyiwa kazi. Kisha nakuagiza uteue wazee na kuwaweka kuwa viongozi katika kila mji. 6 Anayeweza kuteuliwa ni yule ambaye halaumiwi kwa matendo yoyote mabaya, na aliye mwaminifu kwa mkewe,[b] na anao watoto wanaoamini Mungu[c] na ambao sio wakaidi.
Read full chapterFootnotes
- 1:4 Kristo Yesu Au “Mfalme Yesu”. Neno “Kristo” ni tafsiri ya Kiyunani ya neno la Kiebrania “Masihi”, ambao ni wadhifa wa kifalme. Tazama Mk 15:32: Lk 23:2. Tazama pia Kristo na Masihi katika Orodha ya Maneno.
- 1:6 mwaminifu kwa mkewe Kwa maana ya kawaida, “mtu mwenye mke mmoja”, yenye maana pia ameoa mara mmoja tu.
- 1:6 wanaoamini Mungu Neno hli laweza kuwa na maana ya “waaminifu” au “waaminio”. Hapa, maana zote zaweza kujumuishwa. Linganisha kifungu hiki na 1 Tim 3:4.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Copyright © 2017 by Bible League International