Kutenda Mema

Wakumbushe watu kujinyenyekeza kwa watawala na watu wenye mamlaka; wawe watii na wepesi kufanya kazi yo yote halali. Wakumbushe wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wapole na waonyeshe unyenyekevu kwa kila mtu.

Maana kuna wakati ambapo sisi wenyewe tulikuwa wajinga, wakaidi; tukidanganywa na daima kutawaliwa na tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tulikuwa tukiishi maisha ya uovu na wivu, tukichukiwa na watu na kuchukiana sisi kwa sisi. Lakini wakati wema na upendo wa Mungu Mkombozi wetu ulipodhihirishwa, ali tuokoa, si kwa sababu ya matendo mema ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya huruma yake. Alituokoa kwa kuoshwa na kuzaliwa mara ya pili na kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu, ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu. Na tukishahesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele tunaoutumainia . Neno hili ni kweli kabisa. Ninataka uyatilie mkazo mambo haya ili wale waliomwamini Mungu waone umuhimu wa kutenda mema wakati wote, maana mambo haya ni mazuri na tena ni ya manufaa kwa watu.

Lakini jiepushe na ubishi wa kipuuzi: mambo kama orodha ndefu za vizazi na ubishi na ugomvi juu ya sheria; haya hayana maana wala hayamsaidii mtu ye yote. 10 Mtu anayesababisha mafarakano, muonye mara ya kwanza na mara ya pili. Baada ya hapo, usijishughulishe naye tena. 11 Una jua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi ambaye amejihukumu mwenyewe.

Maagizo Ya Mwisho

12 Nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja Nika poli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya bar idi. 13 Wahimize Zena, yule mwanasheria, na Apolo waje upesi na uhakikishe kwamba hawapungukiwi na kitu cho chote. 14 Watu wetu hawana budi kujifunza kuona umuhimu wa kutenda mema, ili waweze kusaidia watu wenye mahitaji ya lazima na maisha yao yasikose kuwa na matunda.

Put them in mind to be subject to principalities and powers, to obey magistrates, to be ready to every good work,

To speak evil of no man, to be no brawlers, but gentle, shewing all meekness unto all men.

For we ourselves also were sometimes foolish, disobedient, deceived, serving divers lusts and pleasures, living in malice and envy, hateful, and hating one another.

But after that the kindness and love of God our Saviour toward man appeared,

Not by works of righteousness which we have done, but according to his mercy he saved us, by the washing of regeneration, and renewing of the Holy Ghost;

Which he shed on us abundantly through Jesus Christ our Saviour;

That being justified by his grace, we should be made heirs according to the hope of eternal life.

This is a faithful saying, and these things I will that thou affirm constantly, that they which have believed in God might be careful to maintain good works. These things are good and profitable unto men.

But avoid foolish questions, and genealogies, and contentions, and strivings about the law; for they are unprofitable and vain.

10 A man that is an heretick after the first and second admonition reject;

11 Knowing that he that is such is subverted, and sinneth, being condemned of himself.

12 When I shall send Artemas unto thee, or Tychicus, be diligent to come unto me to Nicopolis: for I have determined there to winter.

13 Bring Zenas the lawyer and Apollos on their journey diligently, that nothing be wanting unto them.

14 And let our's also learn to maintain good works for necessary uses, that they be not unfruitful.

15 All that are with me salute thee. Greet them that love us in the faith. Grace be with you all. Amen.