Font Size
Mathayo 7:1-5
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mathayo 7:1-5
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Iweni Waangalifu Mnapokosoa Wengine
(Lk 6:37-38,41-42)
7 Msiwahukumu wengine, ili Mungu asiwahukumu ninyi pia. 2 Mtahukumiwa jinsi ile ile mnavyowahukumu wengine. Mungu atawatendea kama mnavyowatendea wengine.
3 Kwa nini unaona vumbi iliyo katika jicho la rafiki yako, na hujali kipande cha mti kilicho katika jicho lako? 4 Kwa nini unamwambia rafiki yako, ‘Ngoja nitoe vumbi lililo katika jicho lako wakati wewe mwenyewe bado una kipande cha mti katika jicho lako?’ 5 Ewe mnafiki! Ondoa kwanza kipande cha mti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utaweza kuona vizuri na kutoa vumbi katika jicho la rafiki yako.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International