Font Size
Mathayo 3:13-17
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mathayo 3:13-17
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana Ambatiza Yesu
(Mk 1:9-11; Lk 3:21-22)
13 Ndipo Yesu alitoka Galilaya na kwenda Mto Yordani. Alikwenda kwa Yohana, akitaka kubatizwa. 14 Lakini Yohana alijaribu kumzuia. Yohana akamwambia Yesu, “Kwa nini unakuja kwangu ili nikubatize? Mimi ndiye ninayepaswa kubatizwa na wewe!”
15 Yesu akajibu, “Acha iwe hivyo kwa sasa. Tunapaswa kuyatimiza mapenzi ya Mungu.” Ndipo Yohana akakubali.
16 Hivyo Yesu akabatizwa. Mara tu aliposimama kutoka ndani ya maji, mbingu zilifunguka na akamwona Roho Mtakatifu akishuka kutoka mbinguni kama hua[a] na kutua juu yake. 17 Sauti kutoka mbinguni ikasema, “Huyu ni Mwanangu, nimpendaye. Ninapendezwa naye.”
Read full chapterFootnotes
- 3:16 hua Ndege mfano wa njiwa, aendaye kwa kasi au “njiwa pori”, “tetere”.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International