Mathayo 21:33-46
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Atoa Simulizi Kuhusu Shamba la Mzabibu
(Mk 12:1-12; Lk 20:9-19)
33 Sikilizeni simulizi hii: Alikuwepo mtu aliyemiliki shamba la mizabibu. Alijenga uzio kuzunguka shamba lile la mizabibu na akachimba shimo kwa ajili ya kukamulia zabibu.[a] Kisha akajenga mnara wa lindo. Akalikodisha shamba kwa wakulima kisha akasafiri. 34 Wakati wa kuvuna zabibu ulipofika, akawatuma watumishi wake waende kwa wakulima ili apate gawio lake la zabibu.
35 Lakini wakulima waliwakamata wale watumishi na kumpiga mmoja wao. Wakamwua mwingine na wa tatu wakampiga kwa mawe mpaka akafa. 36 Hivyo mwenye shamba akawatuma baadhi ya watumishi wengine wengi zaidi ya aliowatuma hapo kwanza. Lakini wakulima wakawatendea kama walivyowatendea watumishi wa kwanza. 37 Hivyo mwenye shamba akaamua kumtuma mwanaye kwa wakulima. Alisema, ‘Wakulima watamheshimu mwanangu.’
38 Lakini wakulima walipomwona mwanaye, wakaambizana, ‘Huyu ni mwana wa mwenye shamba. Shamba hili litakuwa lake. Tukimwua, shamba la mizabibu litakuwa letu.’ 39 Hivyo wakulima wakamchukua mwana wa mwenye shamba, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu na kumwua.
40 Hivyo mmiliki wa shamba la mizabibu atawafanya nini wakulima hawa atakaporudi?”
41 Makuhani wa Kiyahudi na viongozi wakasema, “Kwa hakika atawaua watu hao waovu. Kisha atawakodishia wakulima wengine shamba hilo, watakaompa gawio la mazao yake wakati wa mavuno.”
42 Yesu akawaambia, “Hakika mmesoma hili katika Maandiko:
‘Jiwe walilolikataa waashi
limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Bwana amefanya hivi,
na ni ajabu kubwa kwetu kuliona.’(A)
43 Hivyo ninawaambia kuwa, ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na watapewa watu wanaofanya mambo anayoyataka Mungu katika ufalme wake. 44 Kila aangukaye kwenye jiwe hili atavunjika na litamsaga kila linayemwangukia.”[b]
45 Viongozi wa makuhani na Mafarisayo waliposikia simulizi hizi, wakajua kuwa Yesu alikuwa anawasema wao. 46 Walitaka kumkamata Yesu. Lakini waliogopa kwani watu waliamini kuwa Yesu ni nabii.
Read full chapter
Matthew 21:33-46
New International Version
The Parable of the Tenants(A)
33 “Listen to another parable: There was a landowner who planted(B) a vineyard. He put a wall around it, dug a winepress in it and built a watchtower.(C) Then he rented the vineyard to some farmers and moved to another place.(D) 34 When the harvest time approached, he sent his servants(E) to the tenants to collect his fruit.
35 “The tenants seized his servants; they beat one, killed another, and stoned a third.(F) 36 Then he sent other servants(G) to them, more than the first time, and the tenants treated them the same way. 37 Last of all, he sent his son to them. ‘They will respect my son,’ he said.
38 “But when the tenants saw the son, they said to each other, ‘This is the heir.(H) Come, let’s kill him(I) and take his inheritance.’(J) 39 So they took him and threw him out of the vineyard and killed him.
40 “Therefore, when the owner of the vineyard comes, what will he do to those tenants?”
41 “He will bring those wretches to a wretched end,”(K) they replied, “and he will rent the vineyard to other tenants,(L) who will give him his share of the crop at harvest time.”
42 Jesus said to them, “Have you never read in the Scriptures:
“‘The stone the builders rejected
has become the cornerstone;
the Lord has done this,
and it is marvelous in our eyes’[a]?(M)
43 “Therefore I tell you that the kingdom of God will be taken away from you(N) and given to a people who will produce its fruit. 44 Anyone who falls on this stone will be broken to pieces; anyone on whom it falls will be crushed.”[b](O)
45 When the chief priests and the Pharisees heard Jesus’ parables, they knew he was talking about them. 46 They looked for a way to arrest him, but they were afraid of the crowd because the people held that he was a prophet.(P)
Footnotes
- Matthew 21:42 Psalm 118:22,23
- Matthew 21:44 Some manuscripts do not have verse 44.
© 2017 Bible League International
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.