Font Size
Mathayo 21:30-32
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mathayo 21:30-32
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
30 Kisha baba akamwendea mwanaye mwingine na kumwambia, ‘Mwanangu, nenda ukafanye kazi kwenye shamba la mizabibu leo.’ Akajibu, ‘Sawa baba, nitakwenda kufanya kazi.’ Lakini hakwenda.
31 Ni yupi kati ya wana hawa wawili alimtii baba yake?”
Viongozi wa Kiyahudi wakajibu, “Ni mwana wa kwanza.”
Yesu akawaambia, “Ukweli ni huu, ninyi ni wabaya kuliko watoza ushuru na makahaba. Ukweli ni kuwa hao wataingia katika ufalme wa Mungu kabla yenu. 32 Yohana alikuja akiwaonesha njia sahihi ya kuishi, na hamkumwamini. Lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini Yohana. Mliona yaliyotokea, lakini hamkubadilika na mlikataa kumwamini.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International