Add parallel Print Page Options

Yesu Afundisha Kuhusu Talaka

(Mk 10:1-12)

19 Yesu alipomaliza kuzungumza haya yote, aliondoka Galilaya. Alikwenda maeneo ya Yuda ng'ambo ya Mto Yordani. Watu wengi walimfuata na akaponya wagonjwa wengi huko.

Baadhi ya Mafarisayo wakamjia Yesu. Walitaka aseme jambo fulani lisilo sahihi. Wakamwuliza, “Je, ni sahihi kwa mume kumtaliki mke wake kutokana na sababu yoyote ile kama anavyotaka?”

Yesu akajibu, “Hakika mmesoma hili katika Maandiko: Mungu alipoumba ulimwengu, ‘aliumba watu wa jinsi ya kiume na wa jinsi ya kike.’(A) Na Mungu alisema, ‘Hii ndiyo sababu mwanaume atawaacha baba na mama yake na kuungana na mke wake. Na hao watu wawili watakuwa mmoja.’(B) Hivyo wao si wawili tena, bali mmoja. Ni Mungu aliowaunganisha pamoja, hivyo mtu yeyote asiwatenganishe.”

Mafarisayo wakauliza, “Sasa kwa nini Musa alitoa amri ya kumruhusu mwanaume kumtaliki mke wake kwa kuandika hati ya talaka?”[a]

Yesu akajibu, “Musa aliwaruhusu kuwataliki wake zenu kwa sababu mlikataa kupokea mafundisho ya Mungu. Lakini talaka haikuruhusiwa hapo mwanzo. Ninawaambia kuwa, kila anayemtaliki mke wake, isipokuwa kutokana na uzinzi, na akamwoa mwanamke mwingine, anazini.”

10 Wafuasi wakamwambia Yesu, “Ikiwa hiyo ndiyo sababu pekee ambayo mtu anaruhusiwa kumtaliki mke wake, ni bora kutooa.”

11 Akajibu, “Tamko hili ni la kweli kwa baadhi ya watu, lakini si kwa kila mtu. Bali ni kwa wale tu waliopewa karama hii. 12 Kuna sababu tofauti kwa nini baadhi ya wanaume hawaoi.[b] Wengine wamezaliwa wakiwa hawana uwezo wa kuzaa watoto, wengine walifanywa hivyo katika maisha yao ya baadaye. Na wengine walichagua kutokuoa kwa ajili ya ufalme wa Mungu. Hili liko hivyo kwa kila anayeweza kulikubali.”

Yesu Awakaribisha Watoto

(Mk 10:13-16; Lk 18:15-17)

13 Ndipo watu wakawaleta watoto wao wadogo kwa Yesu ili awabariki na kuwaombea. Wafuasi wake walipoliona hili, waliwakataza watu wasiwalete watoto kwa Yesu. 14 Lakini Yesu akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie, kwa sababu ufalme wa Mungu ni wa watu walio kama watoto hawa wadogo.” 15 Baada ya Yesu kuwabariki watoto, aliondoka huko.

Mtu Tajiri Akataa Kumfuata Yesu

(Mk 10:17-31; Lk 18:18-30)

16 Mtu mmoja alimwendea Yesu na kumwuliza, “Mwalimu, nifanye jambo gani lililo jema ili niweze kuupata uzima wa milele?”

17 Yesu akajibu, “Kwa nini unaniuliza kuhusu jambo gani lililo jema? Mungu pekee yake ndiye mwema. Lakini ikiwa unataka kuupata uzima wa milele, zitii amri.”

18 Yule mtu akauliza, “Amri zipi?”

Yesu akajibu, “‘Usiue, usizini, usiibe, usiseme uongo, 19 mheshimu baba na mama yako,’(C) na ‘mpende jirani yako[c] kama unavyojipenda wewe mwenyewe.’”(D)

20 Yule kijana akasema, “Ninazitii amri hizi zote. Nifanye nini zaidi?”

21 Yesu akajibu, “Ikiwa unataka kuwa mkamilifu, nenda ukauze kila kitu unachomiliki. Uwape pesa maskini na utakuwa na utajiri mbinguni. Kisha njoo unifuate!”

22 Lakini kijana aliposikia Yesu anamwambia kuhusu kugawa pesa yake, alihuzunika. Hakutaka kufanya hivi kwa kuwa alikuwa tajiri sana. Hivyo aliondoka.

23 Ndipo Yesu aliwaambia wafuasi wake, “Ukweli ni huu, itakuwa vigumu sana kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu. 24 Ndiyo, ninawaambia, ni rahisi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”

25 Wafuasi waliposikia hili walishangaa. Wakauliza, “Sasa ni nani ataweza kuokolewa?”

26 Yesu akawatazama na kuwaambia, “Hili haliwezekani kwa wanadamu, Lakini yote yanawezekana kwa Mungu.”

27 Petro akamwambia, “Tuliacha kila kitu tulichonacho na kukufuata wewe. Tutapata nini?”

28 Yesu akawaambia, “Wakati wa ulimwengu mpya utakapofika, Mwana wa Adamu ataketi kwenye kiti chake cha enzi, kikuu na chenye utukufu mwingi. Na ninaweza kuwaahidi kuwa ninyi mnaonifuata mtaketi kwenye viti kumi na viwili vya enzi, na mtayahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli. 29 Kila aliyeacha nyumba, ndugu, dada, baba, mama, watoto au shamba na akanifuata atapata zaidi ya yale aliyoacha. Na atapata uzima wa milele. 30 Watu wengi walio wa kwanza sasa watakuwa wa mwisho siku zijazo. Na walio wa mwisho sasa watakuwa wa kwanza siku zijazo.

Footnotes

  1. 19:7 amri ya … ya talaka Tazama Kum 24:1.
  2. 19:12 wanaume hawaoi Kwa maana ya kawaida, “Maana wapo walio matowashi”.
  3. 19:19 jirani yako Mafundisho ya Yesu katika Lk 10:25-37 yanaonesha kwa uwazi kuwa hii ni pamoja na yeyote mwenye uhitaji.

Marriage and Divorce(A)

19 Now it came to pass, (B)when Jesus had finished these sayings, that He departed from Galilee and came to the region of Judea beyond the Jordan. (C)And great multitudes followed Him, and He healed them there.

The Pharisees also came to Him, testing Him, and saying to Him, “Is it lawful for a man to divorce his wife for just any reason?”

And He answered and said to them, “Have you not read that He who [a]made them at the beginning (D)‘made them male and female,’ and said, (E)‘For this reason a man shall leave his father and mother and be joined to his wife, and (F)the two shall become one flesh’? So then, they are no longer two but one flesh. Therefore what God has joined together, let not man separate.”

They said to Him, (G)“Why then did Moses command to give a certificate of divorce, and to put her away?”

He said to them, “Moses, because of the (H)hardness of your hearts, permitted you to divorce your (I)wives, but from the beginning it was not so. (J)And I say to you, whoever divorces his wife, except for [b]sexual immorality, and marries another, commits adultery; and whoever marries her who is divorced commits adultery.”

10 His disciples said to Him, (K)“If such is the case of the man with his wife, it is better not to marry.”

Jesus Teaches on Celibacy

11 But He said to them, (L)“All cannot accept this saying, but only those to whom it has been given: 12 For there are [c]eunuchs who were born thus from their mother’s womb, and (M)there are eunuchs who were made eunuchs by men, and there are eunuchs who have made themselves eunuchs for the kingdom of heaven’s sake. He who is able to accept it, let him accept it.”

Jesus Blesses Little Children(N)

13 (O)Then little children were brought to Him that He might put His hands on them and pray, but the disciples rebuked them. 14 But Jesus said, “Let the little children come to Me, and do not forbid them; for (P)of such is the kingdom of heaven.” 15 And He laid His hands on them and departed from there.

Jesus Counsels the Rich Young Ruler(Q)

16 (R)Now behold, one came and said to Him, (S)“Good[d] Teacher, what good thing shall I do that I may have eternal life?”

17 So He said to him, [e]“Why do you call Me good? [f]No one is (T)good but One, that is, God. But if you want to enter into life, (U)keep the commandments.”

18 He said to Him, “Which ones?”

Jesus said, (V)“‘You shall not murder,’ ‘You shall not commit adultery,’ ‘You shall not steal,’ ‘You shall not bear false witness,’ 19 (W)‘Honor your father and your mother,’ and, (X)‘You shall love your neighbor as yourself.’

20 The young man said to Him, “All these things I have (Y)kept [g]from my youth. What do I still lack?”

21 Jesus said to him, “If you want to be perfect, (Z)go, sell what you have and give to the poor, and you will have treasure in heaven; and come, follow Me.”

22 But when the young man heard that saying, he went away sorrowful, for he had great possessions.

With God All Things Are Possible(AA)

23 Then Jesus said to His disciples, “Assuredly, I say to you that (AB)it is hard for a rich man to enter the kingdom of heaven. 24 And again I say to you, it is easier for a camel to go through the eye of a needle than for a rich man to enter the kingdom of God.”

25 When His disciples heard it, they were greatly astonished, saying, “Who then can be saved?”

26 But Jesus looked at them and said to them, “With men this is impossible, but (AC)with God all things are possible.”

27 Then Peter answered and said to Him, “See, (AD)we have left all and followed You. Therefore what shall we have?”

28 So Jesus said to them, “Assuredly I say to you, that in the regeneration, when the Son of Man sits on the throne of His glory, (AE)you who have followed Me will also sit on twelve thrones, judging the twelve tribes of Israel. 29 (AF)And everyone who has left houses or brothers or sisters or father or mother [h]or wife or children or [i]lands, for My name’s sake, shall receive a hundredfold, and inherit eternal life. 30 (AG)But many who are first will be last, and the last first.

Footnotes

  1. Matthew 19:4 NU created
  2. Matthew 19:9 Or fornication
  3. Matthew 19:12 Emasculated men
  4. Matthew 19:16 NU omits Good
  5. Matthew 19:17 NU Why do you ask Me about what is good?
  6. Matthew 19:17 NU There is One who is good. But
  7. Matthew 19:20 NU omits from my youth
  8. Matthew 19:29 NU omits or wife
  9. Matthew 19:29 Lit. fields