Add parallel Print Page Options

Nani ni Mkuu Zaidi?

(Mk 9:33-37; Lk 9:46-48)

18 Wakati huo huo wanafunzi wake wakamjia Yesu na kuuliza, “Nani ni mkuu zaidi katika ufalme wa Mungu?”

Yesu akamwita mtoto mdogo, akamsimamisha mbele yao. Kisha akasema, “Ukweli ni huu, ni lazima mbadilike katika namna mnavyofikiri na muwe kama mtoto mdogo. Msipofanya hivi hamtaingia katika ufalme wa Mungu. Aliye mkuu zaidi katika ufalme wa Mungu ni yule anayejinyenyekeza kama mtoto huyu.

Unapomkubali mtoto mdogo kama huyu kama aliye wangu, unanikubali mimi.

Yesu Aonya Kuhusu Chanzo cha Dhambi

(Mk 9:42-48; Lk 17:1-2)

Ikiwa mmoja wa watoto hawa wadogo ananiamini, na mtu yeyote akasababisha mtoto huyo kutenda dhambi, ole wake mtu huyo. Ingekuwa bora mtu huyo kufungiwa jiwe la kusagia shingoni mwake na kuzamishwa katika kina kirefu baharini. Nawasikitikia watu wa ulimwengu kwa sababu ya mambo yanayofanya watu watende dhambi. Mambo haya lazima yatokee, lakini ole wake mtu yeyote anayeyafanya yatokee.

Mkono au mguu wako ukikufanya utende dhambi, ukate na uutupe. Ni bora ukapoteza kiungo kimoja cha mwili wako na ukaupata uzima wa milele kuliko kuwa na mikono au miguu miwili na ukatupwa katika moto wa milele. Jicho lako likikufanya utende dhambi, ling'oe na ulitupe. Ni bora kwako kuwa na jicho moja tu na ukaupata uzima wa milele kuliko kuwa na macho mawili na ukatupwa katika moto wa Jehanamu.

Yesu Atumia Simulizi ya Kondoo Aliyepotea

(Lk 15:3-7)

10 Iweni waangalifu, msidhani kuwa watoto hawa wadogo si wa muhimu. Ninawaambia kuwa watoto hawa wana malaika mbinguni. Na hao malaika daima wako pamoja na Baba yangu mbinguni. 11 [a]

12 Mtu akiwa na kondoo 100, lakini mmoja wa kondoo akapotea, atafanya nini? Atawaacha kondoo wengine 99 kwenye kilima na kwenda kumtafuta mmoja aliyepotea. Sawa? 13 Na akimpata kondoo aliyepotea, atafurahi kwa sababu ya kondoo huyo mmoja kuliko kondoo wengine 99 ambao hawakupotea. Ninaweza kuwathibitishia, 14 Kwa namna hiyo hiyo, Baba yenu wa mbinguni hapendi mmoja wa watoto hawa wadogo apotee.

Mrekebishe Kila Anayekosea

(Lk 17:3)

15 Ikiwa mmoja wa ndugu au dada yako katika familia ya Mungu akifanya kosa kwako,[b] umwendee na umwambie kile alichokukosea. Ufanye hivi mnapokuwa ninyi wawili tu. Ikiwa mtu huyo atakusikiliza, basi umemsaidia na umfanye kuwa kaka ama dada yako tena. 16 Lakini ikiwa mtu huyo atakataa kukusikiliza, mrudie ukiwa pamoja na ndugu wengine wawili waaminio. Ndipo watakuwepo watu wawili au watatu watakaoweza kueleza kile kilichotokea.[c] 17 Ikiwa mtu aliyetenda dhambi atakataa kuwasikiliza, ndipo uliambie kanisa. Na akikataa kulisikiliza kanisa, mchukulie kama ambavyo ungemchukulia mtu asiyemfahamu Mungu au mtoza ushuru.

18 Ninawahakikishia kuwa mnapotoa hukumu hapa duniani, hukumu hiyo itakuwa hukumu ya Mungu. Na mnapotoa msamaha, nao utakuwa msamaha wa Mungu.[d] 19 Kwa namna nyingine, ikiwa watu wawili waliopo duniani watakubaliana kwa kila wanachokiombea, Baba yangu wa mbinguni atatenda kile wanachokiomba. 20 Ndiyo, ikiwa watu wawili au watatu wanaoniamini watakusanyika pamoja, mimi nitakuwa pamoja nao.”

Simulizi Kuhusu Msamaha

21 Kisha Petro akamwendea Yesu na kumwuliza, “Bwana, ndugu yangu akiendelea kunikosea, ninapaswa kumsamehe anaponikosea mara ngapi? Mara saba?”

22 Yesu akamjibu, “Ninakwambia, ni lazima umsamehe zaidi ya mara saba. Ni lazima uendelee kumsamehe hata kama atakukosea saba mara sabini.[e]

23 Ninawaambia kwa sababu ufalme wa Mungu unafanana na mfalme aliyetaka kupata taarifa kutoka kwa watumishi wake. 24 Mtumishi aliyekuwa anadaiwa na mfalme tani 300[f] za fedha aliletwa kwake. 25 Hakuwa na fedha za kutosha kulipa deni lake. Hivyo mfalme aliamuru kila kitu anachomiliki mtumishi yule kiuzwe ikiwa ni pamoja na mke na watoto wake.

26 Lakini mtumishi alipiga magoti na kumsihi mfalme akisema, ‘Nivumilie. Nitakulipa kila kitu unachonidai.’ 27 Mfalme alimhurumia. Hivyo akamsamehe yule mtumishi deni lote na akamwacha aende akiwa huru.

28 Lakini mtumishi huyo alipoondoka, alimwona mtumishi mwingine aliyekuwa anamdai sarafu mia za fedha. Akamkaba shingo yake na akasema, ‘Nilipe pesa ninayokudai!’

29 Mtumishi anayedaiwa akapiga magoti na kumsihi akisema, ‘Nivumilie. Nitakulipa kila kitu unachonidai.’

30 Lakini mtumishi wa kwanza alikataa kumvumilia. Alimwambia hakimu kuwa alikuwa anamdai pesa, na mtumishi yule alitupwa gerezani mpaka atakapoweza kulipa deni lake. 31 Watumishi wengine walipoona hili, walimhurumia mtumishi aliyefungwa gerezani. Hivyo walienda na kumwambia mfalme kila kitu kilichotokea.

32 Ndipo mfalme alimwita msimamizi wa kwanza na kumwambia, ‘Wewe ni mbaya sana! Ulinisihi nikusamehe deni lako, na nilikuacha ukaondoka bila kulipa kitu chochote! 33 Hivyo ulipaswa kumpa mtu yule mwingine anayetumika pamoja nawe rehema ile ile niliyokupa mimi.’ 34 Mfalme alikasirika sana. Hivyo alifungwa gerezani mpaka atakapoweza kulipa kila kitu anachodaiwa.

35 Mfalme huyu alifanya kama ambavyo Baba yangu wa mbinguni atawafanyia ninyi. Ni lazima umsamehe ndugu au dada yako kwa moyo wako wote, usipofanya hivyo, Baba yangu wa mbinguni hatakusamehe wewe.”

Footnotes

  1. 18:11 Nakala zingine za Kiyunani zimeongeza mstari wa 11: “Mwana wa Adamu amekuja kuokoa waliopotea.” Tazama Lk 19:10.
  2. 18:15 kwako Nakala bora za kale za Kiyunani hazina neno “kwako”.
  3. 18:16 Ndipo watakuwepo … kile kilichotokea Tazama Kum 19:15.
  4. 18:18 mnapotoa msamaha … wa Mungu Kwa maana ya kawaida, “chochote mtakachokifunga hapa duniani kitakuwa kimefungwa mbinguni, na chochote mtakachokifungua kitakuwa kimefunguliwa mbinguni”.
  5. 18:22 saba mara sabini Ni idadi kubwa sana ya makosa, ikiwa na maana kuwa msamaha haupaswi kuwekewa kiwango.
  6. 18:24 tani 300 Kwa maana ya kawaida, “talanta 10,000”. Talanta 1 ilikuwa kama kilo 27 hadi 36 za sarafu za dhahabu, fedha, ama za shaba.

Who Is the Greatest?(A)

18 At (B)that time the disciples came to Jesus, saying, “Who then is greatest in the kingdom of heaven?”

Then Jesus called a little (C)child to Him, set him in the midst of them, and said, “Assuredly, I say to you, (D)unless you are converted and become as little children, you will by no means enter the kingdom of heaven. (E)Therefore whoever humbles himself as this little child is the greatest in the kingdom of heaven. (F)Whoever receives one little child like this in My name receives Me.

Jesus Warns of Offenses(G)

(H)“But whoever causes one of these little ones who believe in Me to sin, it would be better for him if a millstone were hung around his neck, and he were drowned in the depth of the sea. Woe to the world because of [a]offenses! For (I)offenses must come, but (J)woe to that man by whom the offense comes!

(K)“If your hand or foot causes you to sin, cut it off and cast it from you. It is better for you to enter into life lame or maimed, rather than having two hands or two feet, to be cast into the everlasting fire. And if your eye causes you to sin, pluck it out and cast it from you. It is better for you to enter into life with one eye, rather than having two eyes, to be cast into [b]hell fire.

The Parable of the Lost Sheep(L)

10 “Take heed that you do not despise one of these little ones, for I say to you that in heaven (M)their angels always (N)see the face of My Father who is in heaven. 11 (O)For[c] the Son of Man has come to save that which was lost.

12 (P)“What do you think? If a man has a hundred sheep, and one of them goes astray, does he not leave the ninety-nine and go to the mountains to seek the one that is straying? 13 And if he should find it, assuredly, I say to you, he rejoices more over that sheep than over the ninety-nine that did not go astray. 14 Even so it is not the (Q)will of your Father who is in heaven that one of these little ones should perish.

Dealing with a Sinning Brother

15 “Moreover (R)if your brother sins against you, go and tell him his fault between you and him alone. If he hears you, (S)you have gained your brother. 16 But if he will not hear, take with you one or two more, that (T)‘by the mouth of two or three witnesses every word may be established.’ 17 And if he refuses to hear them, tell it to the church. But if he refuses even to hear the church, let him be to you like a (U)heathen and a tax collector.

18 “Assuredly, I say to you, (V)whatever you bind on earth will be bound in heaven, and whatever you loose on earth will be loosed in heaven.

19 (W)“Again[d] I say to you that if two of you agree on earth concerning anything that they ask, (X)it will be done for them by My Father in heaven. 20 For where two or three are gathered (Y)together in My name, I am there in the midst of them.”

The Parable of the Unforgiving Servant

21 Then Peter came to Him and said, “Lord, how often shall my brother sin against me, and I forgive him? (Z)Up to seven times?”

22 Jesus said to him, “I do not say to you, (AA)up to seven times, but up to seventy times seven. 23 Therefore the kingdom of heaven is like a certain king who wanted to settle accounts with his servants. 24 And when he had begun to settle accounts, one was brought to him who owed him ten thousand talents. 25 But as he was not able to pay, his master commanded (AB)that he be sold, with his wife and children and all that he had, and that payment be made. 26 The servant therefore fell down before him, saying, ‘Master, have patience with me, and I will pay you all.’ 27 Then the master of that servant was moved with compassion, released him, and forgave him the debt.

28 “But that servant went out and found one of his fellow servants who owed him a hundred denarii; and he laid hands on him and took him by the throat, saying, ‘Pay me what you owe!’ 29 So his fellow servant fell down [e]at his feet and begged him, saying, ‘Have patience with me, and I will pay you [f]all.’ 30 And he would not, but went and threw him into prison till he should pay the debt. 31 So when his fellow servants saw what had been done, they were very grieved, and came and told their master all that had been done. 32 Then his master, after he had called him, said to him, ‘You wicked servant! I forgave you (AC)all that debt because you begged me. 33 Should you not also have had compassion on your fellow servant, just as I had pity on you?’ 34 And his master was angry, and delivered him to the torturers until he should pay all that was due to him.

35 (AD)“So My heavenly Father also will do to you if each of you, from his heart, does not forgive his brother [g]his trespasses.”

Footnotes

  1. Matthew 18:7 enticements to sin
  2. Matthew 18:9 Gr. Gehenna
  3. Matthew 18:11 NU omits v. 11.
  4. Matthew 18:19 NU, M Again, assuredly, I say
  5. Matthew 18:29 NU omits at his feet
  6. Matthew 18:29 NU, M omit all
  7. Matthew 18:35 NU omits his trespasses