Add parallel Print Page Options

Yohana Atuma Watu Kumwuliza Yesu Swali

(Lk 7:18-35)

11 Yesu alipomaliza maelekezo haya kwa wafuasi wake kumi na wawili wa karibu, aliondoka mahali pale. Akaenda katika miji ya Galilaya kuwafundisha watu na kuwaeleza ujumbe wa Mungu.

Yohana alipokuwa gerezani, alisikia kuhusu mambo yaliyokuwa yanatokea; mambo ambayo Masihi angefanya. Hivyo akawatuma baadhi ya wafuasi wake kwa Yesu. Wakamuuliza, “Wewe ni yule tuliyekuwa tunamngojea, au tumsubiri mwingine?”

Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mliyosikia na kuona: Vipofu wanaona. Viwete wanatembea. Watu wenye magonjwa ya ngozi wanaponywa. Wasiyesikia wanasikia. Wafu wanafufuliwa. Na habari njema inahubiriwa kwa maskini. Heri ni kwa wale wasio na shida kunikubali.”

Wafuasi wa Yohana walipoondoka, Yesu alianza kuongea na watu kuhusu Yohana. Alisema, “Ninyi watu mlikwenda jangwani kuona nini? Mtu aliye dhaifu, kama unyasi unaoyumbishwa na upepo? Hakika, ni nini mlichotarajia kuona? Aliyevaa mavazi mazuri? Hakika si hivyo. Watu wote wanaovaa mavazi mazuri wanapatikana katika ikulu za wafalme. Hivyo mlitoka kuona nini? Nabii? Ndiyo, Yohana ni nabii. Lakini ninawaambia, Yeye ni zaidi ya hilo. 10 Andiko hili liliandikwa kuhusu Yohana:

‘Sikiliza! Nitamtuma mjumbe mbele yako.
    Yeye ataandaa njia kwa ajili yako.’(A)

11 Ukweli ni kuwa Yohana Mbatizaji ni mkuu kuliko yeyote aliyewahi kuja katika ulimwengu huu. Lakini hata mtu asiye wa muhimu katika ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko Yohana. 12 Tangu wakati wa Yohana Mbatizaji ulipokuja mpaka sasa, Ufalme wa Mungu umekabiliwa na mashambulizi. Watu wenye nguvu wamejaribu kuudhibiti ufalme huu.[a] 13 Kabla ya Yohana kuja, Sheria ya Musa na manabii wote wamesema kuhusu mambo ambayo yangetokea. 14 Na ikiwa mnaamini waliyosema, basi Yohana ni Eliya. Ndiye waliyesema angekuja. 15 Ninyi watu mnaonisikia, sikilizeni!

16 Ninaweza kusema nini kuhusu watu wanaoishi leo? Watu siku ya leo ni kama watoto wanaokaa katika masoko. Kundi moja la watoto linaliambia kundi lingine,

17 ‘Tuliwapigia filimbi,
    lakini hamkucheza;
tuliimba wimbo wa maziko,
    lakini hamkuhuzunika.’

18 Kwa nini ninasema watu wako hivyo? Kwa sababu Yohana alikuja na hakula vyakula vya kawaida na kunywa divai, na watu walisema, ‘Ana pepo ndani yake.’ 19 Mwana wa Adamu amekuja akila na kunywa, na watu husema, ‘Mwangalie! Hula sana na kunywa divai nyingi. Ni rafiki wa wakusanya kodi na wenye dhambi wengine.’ Lakini hekima inaonesha kuwa sahihi kutokana na yale inayotenda.”

Maonyo Kwa Wanaomkataa Yesu

(Lk 10:13-15)

20 Kisha Yesu akaanza kuikosoa miji ambako alifanya miujiza yake mingi. Aliikosoa miji hii kwa sababu watu katika miji hii hawakubadili maisha yao na kuacha kutenda dhambi. 21 Yesu alisema, “Itakuwa vibaya kwako Korazini! Itakuwa vibaya kwako Bethsaida![b] Ikiwa miujiza hii hii ingetokea Tiro na Sidoni,[c] watu huko wangeshabadili maisha yao kitambo. Wangekwishavaa magunia na kujimwagia majivu kuonesha kuwa wanasikitikia dhambi zao. 22 Lakini ninawaambia, siku ya hukumu itakuwa vibaya zaidi kwako kuliko Tiro na Sidoni.

23 Nawe Kapernaumu, utakwezwa mpaka mbinguni? Hapana! Utatupwa chini mpaka Kuzimu. Nimetenda miujiza mingi ndani yako. Iwapo miujiza hii ingetokea Sodoma,[d] watu huko wangeacha kutenda dhambi na ungekuwa bado ni mji hata leo. 24 Lakini ninakuambia, itakuwa vibaya kwako siku ya hukumu kuliko Sodoma.”

Yesu Awapa Pumziko Watu Wake

(Lk 10:21-22)

25 Kisha Yesu akasema, “Ninakusifu wewe, Baba, Bwana wa mbinguni na duniani. Ninashukuru kwa sababu umeyaficha mambo haya kwa wale wanaofikiri kuwa ni wenye hekima na werevu sana. Lakini umeyaonesha haya kwa watu walio kama watoto wadogo.[e] 26 Ndiyo, Baba, ulifanya hivi kwa sababu hakika ndivyo ulivyotaka kufanya.

27 Baba yangu amenipa kila kitu. Hakuna amjuaye Mwana isipokuwa Baba peke yake. Na hakuna amjuaye Baba isipokuwa Mwana ndiye anayemjua Baba. Na watu pekee watakaomjua Baba ni wale ambao Mwana atachagua kuwaonesha.

28 Njooni kwangu ninyi nyote mliochoka kutokana na mizigo mizito mnayolazimishwa kubeba. Nitawapa pumziko. 29 Chukueni nira yangu,[f] jifunzeni kutoka kwangu. Mimi ni mwema na mnyenyekevu katika roho. Nanyi mtaweza kupumzika. 30 Ndiyo, nira yangu ni rahisi. Mzigo ninaowapa muubebe ni mwepesi.”

Footnotes

  1. 11:12 Herode Antipa alimkamata na kisha kumwua Yohana Mbatizaji na pia alijaribu kumzuia Yesu na wanafunzi wake kwa nguvu. Tazama Herode katika Orodha ya Maneno.
  2. 11:21 Korazini, Bethsaida Miji ya Kiyahudi iliyokuwa kando kando mwa Ziwa Galilaya ambapo Yesu alifanya miujiza mingi kudhihirisha mamlaka yake yanayotoka kwa Mungu. Pamoja na hili, watu walikataa kubadili maisha waliyoishi yasiyokuwa na Mungu.
  3. 11:21 Tiro na Sidoni Miji iliyojaa ibada ya sanamu ambayo ilijulikana sana kwa uovu uliokuwemo humo.
  4. 11:23 Sodoma Mji ambao Mungu aliuangamiza, pamoja na Jiji la Gomora, kwa sababu watu walioishi walikuwa waovu sana. Tazama Mwa 19.
  5. 11:25 kama watoto wadogo Maana wale ambao hawajaenda shule bado.
  6. 11:29 nira yangu Nira iliwekwa shingoni mwa mnyama anayefanya kazi ili kuvuta mzigo. Ilikuwa pia ni alama ya Kiyahudi kwa sheria. Tazama Mdo 15:10; Gal 5:1. Ilikuwa pia alama ya kutawaliwa na taifa katili la kigeni, kama vile Ufalme wa Rumi.

Messengers from John the Baptist

11 When Jesus had finished instructing his twelve disciples, he went on from there to teach and preach in their cities.

(A)Now when John heard (B)in prison about the deeds of (C)the Christ, he sent word by (D)his disciples and said to him, “Are you (E)the one who is to come, or shall we (F)look for another?” And Jesus answered them, “Go and tell John what you hear and see: (G)the blind receive their sight and the lame walk, lepers[a] are cleansed and the deaf hear, and the dead are raised up, and (H)the poor have good news preached to them. And blessed is the one who (I)is not offended by me.”

As they went away, Jesus began to speak to the crowds concerning John: “What did you go out (J)into the wilderness to see? (K)A reed shaken by the wind? What then did you go out to see? A man[b] dressed in soft clothing? Behold, those who wear soft clothing are in kings' houses. What then did you go out to see? (L)A prophet?[c] Yes, I tell you, and more than a prophet. 10 This is he of whom it is written,

(M)“‘Behold, I send my messenger before your face,
    who will prepare your way before you.’

11 Truly, I say to you, among those born of women there has arisen no one greater than John the Baptist. Yet the one who is least in the kingdom of heaven is greater than he. 12 (N)From the days of John the Baptist until now the kingdom of heaven has suffered violence,[d] and the violent take it by force. 13 (O)For all the Prophets and the Law prophesied until John, 14 and if you are willing to accept it, he is (P)Elijah who is to come. 15 (Q)He who has ears to hear,[e] let him hear.

16 “But to what shall I compare this generation? It is like children sitting in the marketplaces and calling to their playmates,

17 “‘We played the flute for you, and you did not dance;
    we sang a dirge, and you did not mourn.’

18 For John came (R)neither eating (S)nor drinking, and they say, ‘He has a demon.’ 19 The Son of Man came (T)eating and drinking, and they say, ‘Look at him! A glutton and a drunkard, (U)a friend of (V)tax collectors and sinners!’ Yet wisdom is justified by her deeds.”[f]

Woe to Unrepentant Cities

20 (W)Then he began to denounce the cities where most of his mighty works had been done, because they did not repent. 21 (X)“Woe to you, Chorazin! Woe to you, Bethsaida! For if the mighty works done in you had been done in (Y)Tyre and Sidon, they would have repented long ago in sackcloth and ashes. 22 (Z)But I tell you, it will be more bearable on (AA)the day of judgment for (AB)Tyre and Sidon than for you. 23 And you, (AC)Capernaum, will you be exalted to heaven? You will be brought down to (AD)Hades. For if the mighty works done in you had been done in Sodom, it would have remained until this day. 24 (AE)But I tell you that (AF)it will be more tolerable on (AG)the day of judgment for the land of Sodom than for you.”

Come to Me, and I Will Give You Rest

25 (AH)At that time Jesus declared, “I thank you, Father, (AI)Lord of heaven and earth, that (AJ)you have hidden these things from the wise and understanding and (AK)revealed them to little children; 26 yes, Father, for such was your (AL)gracious will.[g] 27 (AM)All things have been handed over to me by my Father, and no one knows the Son (AN)except the Father, and no one knows the Father except the Son and anyone (AO)to whom the Son chooses to reveal him. 28 (AP)Come to (AQ)me, all who labor and are (AR)heavy laden, and I will give you rest. 29 Take my yoke upon you, and (AS)learn from me, for I am (AT)gentle and lowly in heart, and (AU)you will find rest for your souls. 30 For (AV)my yoke is easy, and my burden is light.”

Footnotes

  1. Matthew 11:5 Leprosy was a term for several skin diseases; see Leviticus 13
  2. Matthew 11:8 Or Why then did you go out? To see a man
  3. Matthew 11:9 Some manuscripts Why then did you go out? To see a prophet?
  4. Matthew 11:12 Or has been coming violently
  5. Matthew 11:15 Some manuscripts omit to hear
  6. Matthew 11:19 Some manuscripts children (compare Luke 7:35)
  7. Matthew 11:26 Or for so it pleased you well