Font Size
                  
                
              
            
Mathayo 10:39-41
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Mathayo 10:39-41
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
39 Wale wanaojaribu kuyatunza maisha waliyonayo, watayapoteza. Lakini wale wanaoyaacha maisha yao kwa ajili yangu watapata uzima halisi.
Mungu Atawabariki Wanaowakaribisha Ninyi
(Mk 9:41)
40 Yeyote anayewakubali ninyi ananikubali mimi. Na yeyote anayenikubali anamkubali yule aliyenituma. 41 Yeyote anayemkubali nabii kwa sababu ni nabii atapata ujira wa nabii. Na yeyote anayemkubali mwenye haki kwa sababu ni mwenye haki atapata ujira anaoupata mwenye haki.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU) 
    © 2017 Bible League International