Matendo Ya Mitume 3
Neno: Bibilia Takatifu
Petro Amponya Mlemavu Kwa Jina La Yesu
3 Siku moja Petro na Yohana walikwenda Hekaluni saa tisa kwa sala ya adhuhuri. 2 Karibu na mlango uitwao Mzuri, palikuwa na mtu aliyekuwa amelemaa tangu kuzaliwa. Kila siku huyo mlemavu aliwekwa karibu na lango la Hekalu akawa akiomba fedha kwa watu waliokuwa wakiingia ndani ya Hekalu. 3 Alipowaona Petro na Yohana wakielekea Hekaluni, aliwaomba wampe cho chote. 4 Wakamkazia macho, kisha Petro akamwambia, “Tuangalie!” 5 Akawakodolea macho akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
6 Lakini Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu za kukupa, lakini nitakupa kile nilicho nacho. Kwa jina la Yesu wa Nazareti nakuamuru, tembea!” 7 Petro akamshika yule mtu mkono, akamwinua, akasimama kwa miguu yake mwenyewe. Mara miguu na viungo vyake vikapata nguvu. 8 Akaruka juu, akasimama, akaingia Hekaluni pamoja na Petro na Yohana, huku akirukaruka na kumsifu Mungu. 9 Watu wote walimwona akitembea na kumsifu Mungu 10 wakam tambua kuwa ni yule mlemavu aliyekuwa akiketi nje ya Hekalu penye lango akiomba omba. Wakashangaa mno kuhusu maajabu yaliyomtokea.
Petro Anashuhudia Kuwa Yesu Aponya
11 Yule mtu aliyeponywa alipokuwa bado anawang’ang’ania Petro na Yohana, watu wakawakimbilia mpaka kwenye ukumbi wa Sule mani wakiwa wamejawa na mshangao.
12 Petro alipoona watu wamekusanyika aliwaambia, “Watu wa Israeli, kwa nini mnastaajabu kuhusu jambo hili? Mbona mnatukazia macho kwa mshangao? Mnadhani ni kwa uwezo wetu au utakatifu wetu tumemwezesha mtu huyu kutembea? 13 Sivyo! Mungu wa Ibrahimu na Isaka na Yakobo na wa baba zetu amemtukuza mtumishi wake Yesu kwa muujiza huu. Ninyi mlimtoa ahukumiwe kifo na mkamkana mbele ya Pilato ijapokuwa Pilato alitaka kufuta mashtaka na kumwachilia. 14 Ninyi mlimkataa aliyekuwa Mtakatifu na Mwenye Haki mkaomba mpewe yule muuaji. 15 Hivyo mkamwua aliye chanzo cha Uzima, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu. Sisi ni mashahidi wa mambo haya. 16 Imani katika jina la Yesu imempa nguvu huyu mtu ambaye mnamwona na kumfahamu. Ni kwa jina la Yesu na imani inay opatikana kwake ambayo imemponya huyu mtu kabisa, kama ninyi wenyewe mnavyoona.
17 “Na sasa ndugu zangu, najua ya kuwa mambo mliyomtendea Yesu, ninyi na viongozi wenu, mliyafanya kwa kutokujua. 18 Lakini Mungu alikuwa ametabiri kwa njia ya manabii wake wote kwamba Kristo angeteswa, na hivi ndivyo alivyotimiza utabiri huo. 19 Kwa hiyo tubuni mumgeukie Mungu, ili azifute dhambi zenu, 20 na mpate nguvu za kiroho kutoka kwa Bwana. Naye atampeleka Kristo, yaani Yesu, ambaye alichaguliwa tangu awali kwa ajili yenu. 21 Yeye hana budi kukaa mbinguni mpaka wakati Mungu ataka pofanya kila kitu kuwa kipya tena, kama alivyotamka tangu zamani, kwa kupitia kwa manabii wake watakatifu. 22 Kama Musa alivy osema, ‘Bwana Mungu atawateulia nabii kati ya ndugu zenu kama alivyoniteua mimi. Mtamtii huyo kwa kila jambo atakalowaambia. 23 Mtu ye yote ambaye hatamsikiliza huyo nabii, atatengwa daima na watu wake na kuangamizwa.’
24 “Manabii wote tangu wakati wa Samweli na kuendelea pia walitabiri kuhusu siku hizi. 25 Ninyi ni wana wa manabii na wa ile ahadi ambayo Mungu aliwapa baba zenu, alipomwambia Abrahamu, ‘Kutokana na uzao wako familia zote ulimwenguni zitabarikiwa.’ 26 Mungu alipomfufua mtumishi wake alimtuma kwenu kwanza ili awaletee baraka kwa kuwawezesha kuacha uovu wenu.”
Acts 3
English Standard Version
The Lame Beggar Healed
3 Now Peter and John were (A)going up to the temple at (B)the hour of prayer, (C)the ninth hour.[a] 2 And a man (D)lame from birth was being carried, (E)whom they laid daily at the gate of the temple that is called the Beautiful Gate (F)to ask alms of those entering the temple. 3 Seeing Peter and John about to go into the temple, he asked to receive alms. 4 And Peter directed his gaze at him, as did John, and said, “Look at us.” 5 And he fixed his attention on them, expecting to receive something from them. 6 But Peter said, (G)“I have no silver and gold, but what I do have I give to you. (H)In the name of Jesus Christ of Nazareth, rise up and walk!” 7 And he took him by the right hand and raised him up, and immediately his feet and ankles were made strong. 8 And (I)leaping up, he stood and began to walk, and entered the temple with them, walking and leaping and praising God. 9 And (J)all the people saw him walking and praising God, 10 and recognized him as the one who sat at the Beautiful Gate of the temple, asking for alms. And they were filled with wonder and amazement at what had happened to him.
Peter Speaks in Solomon's Portico
11 (K)While he clung to Peter and John, all the people, utterly astounded, ran together to them in (L)the portico called Solomon's. 12 And when Peter saw it he addressed the people: “Men of Israel, why do you wonder at this, or why do you stare at us, as though by our own power or piety we have made him walk? 13 (M)The God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob, (N)the God of our fathers, (O)glorified his servant[b] Jesus, whom (P)you delivered over and (Q)denied in the presence of Pilate, (R)when he had decided to release him. 14 But you denied (S)the Holy and (T)Righteous One, and (U)asked for a murderer to be granted to you, 15 and you killed (V)the Author of life, (W)whom God raised from the dead. To this we are witnesses. 16 And (X)his name—by (Y)faith in his name—has made this man strong whom you see and know, and the faith that is (Z)through Jesus[c] has given the man this perfect health in the presence of you all.
17 “And now, brothers, I know that (AA)you acted in ignorance, as did also your rulers. 18 But what God (AB)foretold (AC)by the mouth of all the prophets, that (AD)his Christ would (AE)suffer, he thus fulfilled. 19 (AF)Repent therefore, and (AG)turn back, that (AH)your sins may be blotted out, 20 that times of refreshing may come from the presence of the Lord, and that he may send the Christ (AI)appointed for you, Jesus, 21 (AJ)whom heaven must receive until the time for (AK)restoring all the things about which (AL)God spoke by the mouth of his holy prophets long ago. 22 Moses said, ‘The Lord God will raise up for you (AM)a prophet like me from your brothers. You shall listen (AN)to him in whatever he tells you. 23 And it shall be that every soul who does not listen to that prophet (AO)shall be destroyed from the people.’ 24 And (AP)all the prophets who have spoken, from Samuel and those who came after him, also proclaimed these days. 25 (AQ)You are the sons of the prophets and of (AR)the covenant that God made with your fathers, saying to Abraham, (AS)‘And in your offspring shall all the families of the earth be blessed.’ 26 (AT)God, (AU)having raised up his servant, sent him to you first, (AV)to bless you (AW)by turning every one of you from your wickedness.”
Copyright © 1989 by Biblica
The ESV® Bible (The Holy Bible, English Standard Version®), © 2001 by Crossway, a publishing ministry of Good News Publishers. ESV Text Edition: 2025.
