Matendo Ya Mitume 1:1-7:57
Neno: Bibilia Takatifu
1 Mpendwa Teofilo, Katika Kitabu changu cha kwanza nilikuan dikia kuhusu mambo yote aliyotenda Yesu, 2 hadi wakati alipopaa mbinguni. Kabla hajachukuliwa juu, aliwapa mitume wake maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu. 3 Alijionyesha kwao akiwa hai muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kwake. Akawahakikishia kwa njia nyingi ya kuwa ni yeye na akaongea nao kuhusu Ufalme wa Mungu.
4 Wakati mmoja alipokuwa nao, aliwapa amri hii, “Msiondoke Yerusalemu, mpaka mtakapopokea ahadi aliyotoa Baba, ambayo mmeni sikia nikiizungumzia. 5 Kwa maana Yohana aliwabatiza kwa maji lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
Yesu Apaa Mbinguni
6 Mitume walipokutana na Yesu walimwuliza, “Bwana, wakati huu ndipo utawarudishia Waisraeli ufalme ?”
7 Yesu akawaambia, “Si juu yenu kufahamu wakati na majira ambayo yamewekwa na Baba kwa mamlaka yake. 8 Lakini mtapokea nguvu akishawajilia Roho Mtakatifu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu na Yudea yote na Samaria, hadi mwisho wa dunia.”
9 Baada ya kusema haya, wakiwa wanatazama, alichukuliwa juu, na wingu likamficha wasimwone tena. 10 Walikuwa bado wakikaza macho yao mawinguni alipokuwa akienda, ndipo ghafla, wanaume wawili waliovaa mavazi meupe walisimama karibu nao, 11 wakasema, “Ninyi watu wa Galilaya, mbona mnasimama hapa mkitazama mbin guni? Yesu huyu huyu aliyechukuliwa mbinguni atarudi tena kama mlivyomwona akienda mbinguni.”
12 Ndipo mitume waliporudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko umbali wa kama kilometa moja kutoka mjini. 13 Walipoingia mjini Yerusalemu walikwenda katika chumba cha ghorofani walipokuwa wakiishi: Petro, Yohana, Yakobo na Andrea, Filipo, Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo na Simoni aliyeitwa Mzalendo, na Yuda mwana wa Yakobo.
14 Hawa wote waliamua kwa kauli moja kutumia muda wao wote kusali, wakiwa pamoja na wale akina mama, Mariamu mama yake Yesu pamoja na ndugu zake.
15 Ilikuwa ni katika siku hizo ambapo Petro alisimama kati ya waamini wote, watu wapatao mia moja na ishirini, 16 akasema, “Ndugu zangu, ilibidi Maandiko ambayo Roho Mtakatifu alitabiri kupitia kwa Daudi kumhusu Yuda aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu, yatimie. 17 Yuda alikuwa mmoja wetu, kwa maana na yeye alichaguliwa ashiriki katika huduma hii.” 18 Yuda alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na uovu wake na akiwa huko shambani alianguka kifudifudi akapasuka na matumbo yote yakatoka nje. 19 Kila mkazi wa Yerusalemu alisikia habari hizi, kwa hiyo wakapaita mahali hapo kwa lugha yao, Akeldama, yaani ‘shamba la Damu.’ 20 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Zab uri, ‘Mahali pake pasiwe na kitu wala asiwepo mtu atakayekaa hapo,’ na, ‘Nafasi yake ichukuliwe na mwingine.”’
Mathiya Achaguliwa
21 “Kwa hiyo inatubidi tumchague mtu mwingine kati ya wale ambao wamekuwa pamoja nasi 22 tangu wakati Yesu alipobatizwa na Yohana mpaka siku aliyochukuliwa mbinguni. Mmoja wao inabidi aun gane nasi kama shahidi wa ufufuo wa Yesu.”
23 Wakapendekeza majina ya watu wawili. Yusufu, aitwaye Barsaba, pia alijulikana kama Yusto, na Mathiya. 24 Wakaomba, “Bwana ujuaye mioyo ya watu wote, tunakuomba utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua 25 achukue nafasi ya huduma na utume ambayo Yuda aliiacha akaenda panapomstahili.”
26 Kisha wakapiga kura na Mathiya akachaguliwa. Basi akain gizwa katika kundi la wale mitume kumi na mmoja.
Kushuka Kwa Roho Mtakatifu
2 Ilipofika siku ya Pentekoste, waamini wote walikuwa wameku tana mahali pamoja. 2 Ghafla, sauti kama mvumo mkubwa wa upepo uliwashukia kutoka mbinguni, ukaijaza nyumba yote walimokuwa wamekaa. 3 Pakatokea kitu kama ndimi za moto ambao uligawanyika ukakaa juu ya kila mmoja wao. 4 Wote walijazwa Roho Mtakatifu wakaamza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kusema.
5 Wakati huo walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka nchi zote za dunia. 6 Waliposikia kelele hizi, walikusany ika kwa wingi. Wote walishangaa kwa sababu waliwasikia waamini wakiongea lugha ya kila mmoja wao.
7 Wakastaajabu sana, wakasema, “Hawa wote wanaozungumza ni Wagalilaya. 8 Imekuwaje basi tunawasikia wakinena lugha ya kila mmoja wetu? 9 Hapa kuna Waparthi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Yudea Kapadokia, Ponto na Asia, 10 Frigia, Pom filia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene; na wageni kutoka Rumi, Wayahudi na watu walioingia dini ya Kiyahudi. 11 Watu wen gine wametoka Krete na Uarabuni. Sisi sote tunasikia watu hawa wakisema katika lugha zetu wenyewe mambo makuu ya ajabu aliyofa nya Mungu.” 12 Wakiwa wameshangaa wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?” 13 Lakini wengine waliwadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai mpya!”
Mahubiri Ya Petro
14 Ndipo Petro akasimama na wale mitume kumi na mmoja, aka hutubia ule umati wa watu kwa sauti kuu akasema, “Wayahudi wen zangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu. Nisikilizeni kwa makini niwaambie jambo hili maana yake ni nini! 15 Hawa watu hawakulewa kama mnavyodhania, kwa maana sasa ni mapema mno, saa tatu asu buhi. 16 La, jambo hili lilitabiriwa na Nabii Yoeli aliposema, 17 ‘Mungu alisema, siku za mwisho nitawamiminia binadamu wote Roho yangu: wavulana wenu na binti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono na wazee wataota ndoto. 18 Ndio, hata watumishi wangu wa kiume na wa kike nitawamiminia Roho yangu, nao watata biri. 19 Nami nitafanya maajabu angani, na duniani nitaonyesha ishara, damu na moto na moshi mnene. 20 Jua litageuka kuwa giza na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya siku ya Bwana kuwa dia, siku ambayo itakuwa ya kutisha. 21 Lakini ye yote ata kayetubu na kukiri jina la Bwana, ataokoka.’
22 “Nawasihi ninyi Waisraeli mnisikilize. Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa njia ya miujiza, maajabu na ishara, kama ninyi wenyewe mjuavyo. 23 Huyu Yesu ali tiwa mikononi mwenu kwa mpango na makusudi ya Mungu aliyoyafahamu tangu awali. Nanyi mlimwua kwa kumtundika na kumpigilia misumari msalabani, mkisaidiwa na watu waovu. 24 Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu hata kifo kisingaliweza kumzuia. 25 Daudi alisema hivi juu yake, ‘Nilimwona Bwana akiwa mbele yangu wakati wote, Bwana yuko upande wangu wa kulia ili nisiogope. 26 Kwa hiyo moyo wangu unafurahi na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao una matumaini ya uzima. 27 Kwa maana wewe Bwana hutaniacha kuzimu; wala hutaacha mtakatifu wako ateseke na kuoza. 28 Wewe umenionyesha njia inifikishayo uzimani. Na uwepo wako ukiwepo nami nitajawa na furaha.’
29 “Ndugu zangu, nataka niwaambie wazi kwamba mfalme Daudi alikufa na kuzikwa, na kaburi lake lipo hata leo. 30 Lakini ali kuwa nabii, na alijua ya kuwa Mungu aliahidi kwa kiapo kwamba angempa mmoja wa uzao wake kiti chake cha ufalme. 31 Kwa hiyo Daudi akaona mambo ambayo yangetokea, akatamka juu ya kufufuka kwa Kristo, kwamba asingeachwa kuzimu, wala mwili wake usingehar ibiwa kwa kuoza. 32 Huyu Yesu, Mungu alimfufua, na sisi ni mash ahidi wa tukio hilo.
33 “Basi akiwa ametukuzwa na kukaa upande wa kulia wa Mungu, alipokea Roho Mtakatifu aliyeahidiwa na Baba yake. Huyo Roho Mtakatifu ndiye aliyetumiminia haya mnayoyaona na kuyasikia. 34 Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini alisema, ‘Bwana alim wambia Bwana wangu: kaa upande wangu wa kulia, 35 mpaka nitaka powafanya maadui zako kiegemezo cha miguu yako.’
36 “Basi nataka niwahakikishie Waisraeli wote ya kuwa, Mungu amemfanya huyu Yesu ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa ndiye
Ongezeko La Waamini
37 Watu waliposikia maneno haya yaliwachoma moyoni, wakawau liza Petro na wale mitume wengine, “Tufanye nini ndugu zetu?” 38 Petro aliwajibu, “Tubuni, muache dhambi na kila mmoja wenu abatizwe katika jina la Yesu Kristo, ili msamehewe dhambi zenu; nanyi mtapokea zawadi ya Roho Mtakatifu. 39 Kwa maana ahadi hii ilitolewa na Mungu kwa ajili yenu na watoto wenu, na wale wote walio nchi za mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu anamwita kwake.”
40 Petro aliwasihi kwa maneno mengine mengi na kuwaonya akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kiovu.” 41 Wote waliopokea ujumbe wa Petro walibatizwa na zaidi ya watu elfu tatu wal iongezeka katika kundi la waamini siku hiyo.
Ushirika Wa Waamini
42 Waamini hawa walitumia muda wao wakifundishwa na mitume, wakiishi pamoja katika ushirika, wakila pamoja na kusali. 43 Watu wote wakajawa na hofu kwa maana miujiza mingi na maajabu yalifanywa na mitume.
44 Waamini wote waliishi pamoja na kushirikiana kila kitu walichokuwa nacho kwa pamoja. 45 Waliuza mali zao na vitu waliv yokuwa navyo wakagawiana fedha walizopata, kila mtu akapata kadiri ya mahitaji yake. 46 Siku zote waliendelea kuabudu katika Hekalu na kushiriki chakula cha Bwana nyumbani mwao na kula pamoja kwa furaha na shukrani, 47 huku wakimsifu Mungu na kupendwa na watu wote. Na kila siku Bwana alikuwa akiongeza katika kundi lao watu aliokuwa akiwaokoa.
Petro Amponya Mlemavu Kwa Jina La Yesu
3 Siku moja Petro na Yohana walikwenda Hekaluni saa tisa kwa sala ya adhuhuri. 2 Karibu na mlango uitwao Mzuri, palikuwa na mtu aliyekuwa amelemaa tangu kuzaliwa. Kila siku huyo mlemavu aliwekwa karibu na lango la Hekalu akawa akiomba fedha kwa watu waliokuwa wakiingia ndani ya Hekalu. 3 Alipowaona Petro na Yohana wakielekea Hekaluni, aliwaomba wampe cho chote. 4 Wakamkazia macho, kisha Petro akamwambia, “Tuangalie!” 5 Akawakodolea macho akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
6 Lakini Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu za kukupa, lakini nitakupa kile nilicho nacho. Kwa jina la Yesu wa Nazareti nakuamuru, tembea!” 7 Petro akamshika yule mtu mkono, akamwinua, akasimama kwa miguu yake mwenyewe. Mara miguu na viungo vyake vikapata nguvu. 8 Akaruka juu, akasimama, akaingia Hekaluni pamoja na Petro na Yohana, huku akirukaruka na kumsifu Mungu. 9 Watu wote walimwona akitembea na kumsifu Mungu 10 wakam tambua kuwa ni yule mlemavu aliyekuwa akiketi nje ya Hekalu penye lango akiomba omba. Wakashangaa mno kuhusu maajabu yaliyomtokea.
Petro Anashuhudia Kuwa Yesu Aponya
11 Yule mtu aliyeponywa alipokuwa bado anawang’ang’ania Petro na Yohana, watu wakawakimbilia mpaka kwenye ukumbi wa Sule mani wakiwa wamejawa na mshangao.
12 Petro alipoona watu wamekusanyika aliwaambia, “Watu wa Israeli, kwa nini mnastaajabu kuhusu jambo hili? Mbona mnatukazia macho kwa mshangao? Mnadhani ni kwa uwezo wetu au utakatifu wetu tumemwezesha mtu huyu kutembea? 13 Sivyo! Mungu wa Ibrahimu na Isaka na Yakobo na wa baba zetu amemtukuza mtumishi wake Yesu kwa muujiza huu. Ninyi mlimtoa ahukumiwe kifo na mkamkana mbele ya Pilato ijapokuwa Pilato alitaka kufuta mashtaka na kumwachilia. 14 Ninyi mlimkataa aliyekuwa Mtakatifu na Mwenye Haki mkaomba mpewe yule muuaji. 15 Hivyo mkamwua aliye chanzo cha Uzima, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu. Sisi ni mashahidi wa mambo haya. 16 Imani katika jina la Yesu imempa nguvu huyu mtu ambaye mnamwona na kumfahamu. Ni kwa jina la Yesu na imani inay opatikana kwake ambayo imemponya huyu mtu kabisa, kama ninyi wenyewe mnavyoona.
17 “Na sasa ndugu zangu, najua ya kuwa mambo mliyomtendea Yesu, ninyi na viongozi wenu, mliyafanya kwa kutokujua. 18 Lakini Mungu alikuwa ametabiri kwa njia ya manabii wake wote kwamba Kristo angeteswa, na hivi ndivyo alivyotimiza utabiri huo. 19 Kwa hiyo tubuni mumgeukie Mungu, ili azifute dhambi zenu, 20 na mpate nguvu za kiroho kutoka kwa Bwana. Naye atampeleka Kristo, yaani Yesu, ambaye alichaguliwa tangu awali kwa ajili yenu. 21 Yeye hana budi kukaa mbinguni mpaka wakati Mungu ataka pofanya kila kitu kuwa kipya tena, kama alivyotamka tangu zamani, kwa kupitia kwa manabii wake watakatifu. 22 Kama Musa alivy osema, ‘Bwana Mungu atawateulia nabii kati ya ndugu zenu kama alivyoniteua mimi. Mtamtii huyo kwa kila jambo atakalowaambia. 23 Mtu ye yote ambaye hatamsikiliza huyo nabii, atatengwa daima na watu wake na kuangamizwa.’
24 “Manabii wote tangu wakati wa Samweli na kuendelea pia walitabiri kuhusu siku hizi. 25 Ninyi ni wana wa manabii na wa ile ahadi ambayo Mungu aliwapa baba zenu, alipomwambia Abrahamu, ‘Kutokana na uzao wako familia zote ulimwenguni zitabarikiwa.’ 26 Mungu alipomfufua mtumishi wake alimtuma kwenu kwanza ili awaletee baraka kwa kuwawezesha kuacha uovu wenu.”
Petro Na Yohana Wakamatwa
4 Walipokuwa bado wanasema na watu, makuhani, mkuu wa walinzi wa Hekalu na Masadukayo waliwajia wakiwa 2 wamekasirika kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wakiwafundisha watu kwamba kufu fuka kwa Yesu kunadhihirisha kwamba wafu watafufuka. 3 Wakawaka mata wakawaweka jela mpaka kesho yake kwa maana ilikuwa jioni. 4 Lakini wengi wa wale waliosikia mahubiri yao waliamini; idadi ya wanaume walioamini ilikuwa kama elfu tano.
5 Siku ya pili yake viongozi wa Kiyahudi, wazee na waandishi wa sheria walikusanyika Yerusalemu. 6 Walikuwepo Kuhani Mkuu Anasi, Kayafa , Yohana, Aleksanda na ndugu zake Kuhani Mkuu. 7 Wakawaleta wale mitume wawili katikati yao wakawauliza, “Ni kwa uwezo gani au mmetumia jina la nani kufanya jambo hili?” 8 Petro, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu akajibu, “Waheshimiwa viongozi na wazee wa watu, 9 kama mnatuhoji kuhusu mambo mema aliyotendewa kilema, na jinsi alivyoponywa, tungependa ninyi na watu wote wa 10 Israeli mfahamu kwamba, ni kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulubisha lakini Mungu akam fufua kutoka kwa wafu, kwa uwezo wa Yesu, huyu mtu anasimama mbele yenu akiwa mzima kabisa. 11 Huyu Yesu ndiye ‘lile jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilikataa, ambalo limekuwa jiwe kuu la pembeni.’ 12 Wokovu unapatikana kwake tu; kwa maana hakuna jina jingine duniani ambalo wamepewa wanadamu kuwaokoa ila jina la Yesu, na ni kwa jina hilo peke yake tunaweza kuokolewa!”
Ujasiri Wa Petro Na Yohana Washangaza Watu
13 Wale viongozi na wazee walipoona ujasiri wa Petro na Yohana na kufahamu ya kuwa walikuwa watu wa kawaida wasio na elimu walishangaa sana. Wakatambua kwamba hawa watu walikuwa na Yesu. 14 Lakini kwa kuwa walimwona yule kilema aliyeponywa ame simama nao hawakuweza kusema lo lote kupinga maneno yao. 15 Wakawaamuru watoke nje ya ule ukumbi. 16 Kisha wakaanza kuulizana, “Tuwafanye nini watu hawa? Hatuwezi kukanusha muujiza huu mkubwa walioufanya ambao ni dhahiri kwa kila mtu Yerusalemu. 17 Lakini tunaweza kuzuia jambo hili lisiendelee kuenezwa kwa watu kama tukiwakanya wasiseme tena na mtu ye yote kwa jina la Yesu.” 18 Kwa hiyo wakawaita tena ndani wakawaamuru wasiseme au kufundisha watu tena kwa jina la Yesu.
Bora Kumtii Mungu Kuliko Wanadamu
19 Ndipo Petro na Yohana wakawajibu, “Ninyi amueni wenyewe lililo bora kutenda mbele za Mungu: kuwatii ninyi au kumtii Mungu. 20 Lakini sisi hatuwezi kuacha kusema yale tuliyoyaona na kuyasikia.”
21 Wale viongozi wakawaonya tena kwa vitisho, kisha waka waacha waende. Hawakuona njia ya kuwaadhibu kwa kuwa waliwaogopa wale watu ambao walishuhudia ule muujiza uliotendeka, nao wali kuwa wakimsifu Mungu. 22 Na yule mtu aliyeponywa alikuwa na umri wa zaidi ya miaka arobaini.
23 Mara Petro na Yohana walipoachiliwa, walirudi kwa waamini wenzao wakawaeleza waliyoambiwa na makuhani wakuu na wazee. 24 Waamini wote waliposikia maneno yao walimwomba Mungu kwa pamoja wakasema, “Wewe Bwana Mtukufu, uliyeumba mbingu na nchi na bahari na kila kiumbe kilichopo, 25 wewe ulitamka kwa njia ya Roho wako mtakatifu kupitia kwa baba yetu Daudi mtumishi wako, aliposema, ‘Mbona mataifa wanaghadhabika, na watu wanawaza mambo yasiyo na maana? 26 Wafalme wa dunia wamejiandaa na watawala wamekusanyika wampinge Bwana na Masihi wake.’ 27 Ndiyo sababu katika mji huu Herode na Pontio Pilato walikutana na Waisraeli wote na watu wa mataifa juu ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, 28 wakaamua kumfanyia yale yote ambayo wewe ulikuwa umekusudia tangu awali na kupanga kwa uweza wako yatendeke.
29 “Sasa Bwana, sikia vitisho vyao na utuwezeshe sisi wat umishi wako kuhubiri neno lako kwa ujasiri mkuu; 30 na unyooshe mkono wako ili tuweze kuponya wagonjwa na kutenda ishara na miu jiza kwa jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.” 31 Walipokwisha kusali, nyumba waliyokuwa wamekutania ikatikisika na wote wakaja zwa na Roho Mtakatifu, wakahubiri neno la Mungu kwa ujasiri. 32 Waamini wote walikuwa na nia moja na moyo mmoja, wala hakuna aliyeona mali aliyokuwa nayo kuwa yake, bali walishirikiana vitu vyote kwa pamoja. 33 Na kwa uwezo mkubwa mitume wakashuhudia kwa ujasiri habari za kufufuka kwa Bwana Yesu. Mungu akawapa wote neema kuu. 34 Wala hakuwepo mtu ye yote miongoni mwa waamini aliyepungukiwa na kitu kwa sababu wale waliokuwa na mashamba na nyumba waliuza vyote wakaleta fedha waliyopata 35 kwa wale mitume; kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
36 Ndivyo ilivyokuwa kwamba Yusufu ambaye mitume walimwita Barnaba, maana yake Mwana wa Faraja, wa ukoo wa Lawi kutoka kisiwa cha Kipro 37 aliuza shamba alilokuwa nalo akaleta fedha alizopata kwa wale mitume.
Anania Na Safira
5 Pia mtu mmoja jina lake Anania na mkewe Safira waliuza mali yao. 2 Lakini Anania, kwa makubaliano na mkewe akaficha sehemu ya fedha alizopata, akaleta kiasi kilichobakia kwa mitume.
3 Petro akamwambia, “Anania, mbona shetani ametawala moyo wako kiasi cha kukubali kumdanganya Roho Mtakatifu, ukaficha sehemu ya fedha ulizopata? 4 Kabla hujauza hilo shamba lilikuwa mali yako. Na hata baada ya kuliuza , fedha ulizopata zilikuwa zako. Kwa nini basi umeamua moyoni mwako kufanya jambo kama hili? Ujue hukumdanganya mtu ila umemdanganya Mungu.”
Ujue hukumdanganya mtu ila umemdanganya Mungu.”
5 Anania aliposikia maneno haya akaanguka chini akafa. Na wote waliosikia maneno haya wakajawa na hofu. 6 Vijana wakaingia wakaufunga mwili wake wakamchukua nje kumzika.
7 Na baada ya muda wa saa tatu mkewe Anania akaingia, naye hakuwa na habari ya mambo yaliyotokea. 8 Petro akamwuliza, “Niambie, je? Mliuza shamba lenu kwa kiasi hiki?” Akajibu, “Ndio, tuliuza kwa kiasi hicho.”
9 Ndipo Petro akamwambia, “Imekuwaje wewe na mumeo mkaamua kumjaribu Roho Mtakatifu wa Bwana? Tazama, vijana waliomzika mumeo wako mlangoni nao watakuchukua nje.”
10 Na mara akaanguka chini akafa. Wale vijana walipoingia wakamwona kuwa amekufa, wakamchukua wakamzika karibu na mumewe. 11 Waamini wote na watu wote waliosikia habari hizi wakajawa na hofu kuu.
Mitume Wafanya Miujiza Mingi Na Maajabu
12 Mitume walifanya miujiza mingi na ishara za ajabu. Na waamini wote walikuwa wakikusanyika katika ukumbi wa Sulemani. 13 Hakuna mtu mwingine aliyethubutu kujiunga nao lakini watu wote waliwaheshimu sana. 14 Hata hivyo watu wengi zaidi, wanaume kwa wanawake walikuwa wakiongezeka katika kundi la waliomwamini Bwana. 15 Hata walikuwa wakiwabeba wagonjwa wakawalaza kwenye mikeka barabarani ili Petro alipokuwa akipita kivuli chake kiwa guse angalau baadhi yao, wapone. 16 Pia watu walikusanyika kutoka katika miji iliyokuwa karibu na Yerusalemu wakileta wagonjwa na watu waliopagawa na pepo wachafu, hao wote wakapo nywa.
Mitume Washitakiwa
17 Kuhani mkuu na wale waliomuunga mkono, yaani Masadukayo, walijawa na wivu, 18 wakawakamata mitume na kuwatia gerezani.
19 Lakini usiku ule malaika wa Bwana akaja akawafungulia milango ya gereza akawatoa nje akawaambia, 20 “Nendeni mkasi mame Hekaluni mkawaambie watu habari za maisha haya mapya!”
21 Waliposikia haya wakaenda Hekaluni alfajiri wakaanza kufundisha watu. Kuhani Mkuu alipowasili pamoja na wenzake wakaitisha mkutano wa baraza na wazee wote wa Israeli wakatuma wale mitume waletwe kutoka gerezani. 22 Lakini wale maafisa wal iotumwa walipoingia gerezani hawakuwakuta wale mitume mle. Kwa hiyo wakarudi kutoa ripoti kwa baraza. 23 Wakasema, “Tumekuta milango ya jela imefungwa sawasawa, na maaskari wa gereza wamesi mama nje ya milango, lakini tulipofungua milango hakuwepo mtu ye yote ndani.”
24 Mkuu wa kikosi cha Walinzi wa Hekalu na makuhani wakuu waliposikia ripoti hiyo wakashangaa sana wasijue mambo haya yan geishia wapi. 25 Ndipo mtu mmoja akaja akawaambia, “Wale watu mliowatia gerezani wako Hekaluni wakiwafundisha watu.”
26 Ndipo yule mkuu wa kikosi cha walinzi wa Hekalu na wale maofisa wakaenda wakawaleta mitume lakini hawakuwadhuru kwa sababu waliogopa wangelipigwa mawe na watu. 27 Baada ya kuwaleta wakawaweka mbele ya baraza. Kuhani mkuu akaanza kuwahoji,
28 “Tuliwakanya msifundishe kwa jina la huyu mtu, lakini ninyi mmeeneza mafundisho yenu Yerusalemu yote, na tena mmeamua kuwa sisi tuna hatia juu ya kifo chake.”
29 Petro na wale mitume wengine wakajibu, “Imetupasa kumtii Mungu na sio wanadamu. 30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu ambaye ninyi mlimwua kwa kumtundika kwenye msalaba. 31 Mungu alimwinua, akamweka mkono wake wa kuume awe Mtawala na Mwokozi ili awape wana wa Israeli toba na msamaha wa dhambi. 32 Nasi tu mashahidi wa mambo haya pamoja na Roho Mtakatifu aliyetolewa na Mungu kwa watu wanaomtii.”
Mungu kwa watu wanaomtii.”
33 Wajumbe wa baraza la wazee waliposikia haya walijawa na ghadhabu, wakataka kuwaua wale mitume. 34 Lakini mmoja wao, Far isayo aitwaye Gamalieli ambaye alikuwa mwalimu wa sheria aliyeh eshimiwa na watu wote, akasimama akaamuru wale mitume watolewe nje kwa muda.
35 Ndipo alipowaambia wajumbe wa baraza, “Wazee wa Israeli, fikirini kwa uangalifu mtakalowatendea watu hawa! 36 Kumbukeni kuwa sio zamani sana tangu alipotokea mtu aliyeitwa Theuda ambaye alijidai kuwa yeye ni mtu maarufu, akapata wafuasi mia nne wal ioambatana naye. Lakini aliuawa na wafuasi wake wote wakatawany ika, kazi yake ikawa bure. 37 “Baada yake alitokea Yuda Mgali laya wakati ule wa sensa, akapata wafuasi wengi; lakini naye akauawa nalo kundi lake likatawanyika.
38 “Kwa hiyo, kwa kesi hii nawashauri waacheni watu hawa wala msiwatendee lo lote, kwa maana kama mpango wao na kazi yao ni mambo ya wanadamu hayatafika po pote; 39 lakini ikiwa ni kazi ya Mungu hamtaweza kuwazuia. Badala yake huenda mkajikuta mnam pinga Mungu!”
40 Wakapokea ushauri wa Gamalieli; wakawaita mitume ndani na baada ya kuwachapa viboko wakawaamuru wasifundishe kwa jina la Yesu. Wakawaachia waende zao. 41 Wale mitume walitoka barazani wamejaa furaha kwa sababu Mungu aliwapa heshima ya kupata aibu ya kuchapwa viboko kwa ajili ya jina la Yesu. 42 Na kila siku Hek aluni na nyumbani walizidi kuhubiri na kufundisha bila kukoma, juu ya Habari Njema kwamba Yesu ndiye Kristo.
Uchaguzi Wa Wahudumu
6 Siku hizo, wakati idadi ya waamini ilipokuwa ikiongezeka sana palitokea manung’uniko. Wayahudi walioongea lugha ya Kigi riki walilalamika kuwa wakati wa kugawa chakula, wajane walioon gea Kiebrania walipendelewa na wajane wao walibaguliwa. 2 Wale mitume kumi na wawili waliitisha kikao cha wanafunzi wote, wakasema, “Si sawa sisi tuache kazi ya kuhubiri neno la Mungu tuanze kugawa chakula. 3 Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba mion goni mwenu; watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ili tuwakabidhi kazi hii. 4 Na sisi tutatumia wakati wetu kwa kuomba na kufundisha neno la Bwana.”
5 Uamuzi huu ukawaridhisha wote nao wakawachagua Stefano, mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu; na Filipo, Prokoro, Nika nori, na Timoni, Parmena na Nikolao mwongofu wa kutoka Antiokia. 6 Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.
7 Na neno la Mungu likazidi kuenea; idadi ya wanafunzi ika zidi kuongezeka sana katika Yerusalemu, na hata makuhani wengi wakamwamini Yesu.
Stefano Akamatwa
8 Na Stefano akiwa amejawa na neema na nguvu za Mungu alifa nya maajabu makubwa na ishara kati ya watu.
9 Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa la ‘Watu Huru,’ na wengine kutoka masinagogi ya Kirene na Aleksandria, pamoja na baadhi kutoka Kilikia na Asia, wakajaribu kubishana na Stefano. 10 Lakini hawakuweza kushindana naye kwa sababu ya hekima yake na Roho aliyemwezesha kusema.
11 Ndipo wakawashawishi watu fulani ambao walisema, “Tulim sikia akisema maneno ya kufuru juu ya Musa na Mungu.”
Stefano Afikishwa Mbele Ya Baraza
12 Wakawachochea watu, wazee na waandishi wa sheria nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza. 13 Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walisema, “Mtu huyu siku zote anasema maneno ya kashfa juu ya Hekalu hili takatifu na juu ya sheria za Musa. 14 Kwa maana tumemsikia akisema kwamba eti huyu Yesu wa Nazareti ataharibu hili Hekalu takatifu na atabadilisha mila zote tulizopewa na Musa.” 15 Watu wote waliokuwa katika baraza hilo walimtazama Stefano kwa makini wakaona uso wake unang’aa kama uso wa malaika! Hotuba Ya Stefano
7 Ndipo kuhani mkuu alimwuliza Stefano, “Je, mashtaka haya ni ya kweli?” 2 Stefano akajibu, “Ndugu zangu na baba zangu, nisikilizeni! Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Ibrahimu, ali pokuwa Mesopotamia, kabla hajahamia Harani, 3 akamwambia, ‘Ondoka kutoka katika nchi yako na kutoka kwa jamii yako uende katika nchi nitakayokuonyesha.’ 4 Ndipo alipotoka katika nchi ya Wakal dayo akaenda kukaa Harani. Baba yake alipokufa, Mungu akamtoa huko akamweka katika nchi hii ambayo mnaishi sasa. 5 Lakini Mungu hakumpa urithi wo wote katika nchi hii, hakumpa hata mita moja ya ardhi. Bali Mungu alimwahidi kuwa yeye na uzao wake wangeirithi hii nchi, ingawa wakati huo Ibrahimu hakuwa na mtoto. 6 Mungu alimwambia maneno haya, ‘Wazao wako wataishi ugenini, ambapo watafanywa kuwa watumwa na kutendewa maovu kwa kipindi cha miaka mia nne. 7 Lakini nitalihukumu taifa ambalo watalitumikia, na baada ya haya watatoka katika nchi hiyo ili waje kuniabudu mahali hapa.’
8 “Mungu akampa Ibrahimu agano la tohara. Basi Ibrahimu akawa baba wa Isaka; naye akamtahiri Isaka siku ya nane baada ya kuzaliwa kwake. Isaka akawa baba wa Yakobo, naye Yakobo akawa baba wa babu zetu kumi na wawili. 9 Hawa babu zetu walimwonea Yusufu ndugu yao wivu, wakamwuza utumwani Misri. Lakini Mungu alikuwa pamoja naye. 10 Akamwokoa katika mateso yote yaliyom pata, na akampa fadhili na hekima mbele ya Farao, Mfalme wa Misri, ambaye alimfanya waziri mkuu wa nchi nzima na mtawala wa nyumba ya mfalme.
11 “Kukawa na njaa na dhiki kubwa nchi yote ya Misri na Kanaani, na babu zetu wakawa hawana chakula. 12 Lakini Yakobo aliposikia kwamba kule Misri kulikuwa na nafaka, aliwatuma wanawe, wakaenda huko kwa mara yao ya kwanza. 13 Nao walipotumwa mara ya pili, Yusufu alijitambulisha kwa ndugu zake, na akawatam bulisha ndugu zake kwa Farao. 14 Yusufu akatuma Yakobo baba yake aletwe Misri pamoja na ukoo mzima, wakiwa ni watu sabini na watano; na 15 Yakobo akaenda Misri. Naye akafa huko, yeye na wanawe, yaani babu zetu, 16 na miili yao ikachukuliwa na kuzikwa huko Shekemu katika kaburi ambalo Ibrahimu alinunua kutoka kwa wana wa Hamori. 17 Ulipokaribia wakati Mungu aliopanga kutimiza ahadi yake, kwa Ibrahimu, idadi ya watu iliongezeka sana huko Misri. 18 Ndipo akatokea mfalme mpya wa Misri ambaye hakumfahamu wala kumtambua Yusufu. 19 Huyu mfalme aliwafanyia hila watu wa taifa letu na akawalazimisha babu zetu wawatupe watoto wao wachanga ili wafe.
20 “Musa alizaliwa wakati huo, naye alikuwa mtoto mzuri sana machoni pa Mungu. Akalelewa na wazazi wake kwa muda wa miezi mitatu. 21 Waliposhindwa kumficha zaidi, wakamweka nje na binti Farao akamchukua akamtunza kama mtoto wake mwenyewe. 22 Musa akafundishwa hekima yote ya Wamisri akawa mtu shujaa kwa maneno na matendo yake. 23 Musa alipokuwa na umri wa miaka arobaini akawa na hamu ya kuwatembelea ndugu zake Waisraeli. 24 Alipoona mmoja wao akionewa na Mmisri, akamwua yule Mmisri kulipiza kisasi. 25 Alidhani kuwa ndugu zake wangeelewa kwamba Mungu ali kuwa akiwaokoa kwa msaada wake, lakini wao hawakuelewa. 26 Kwa hiyo siku ya pili alipoona Waisraeli wanagombana alijaribu kuwa patanisha, akawaambia, ‘Jamani, ninyi ni ndugu. Mbona mnaoneana wenyewe kwa wenyewe?’ 27 Lakini yule aliyekuwa akimwonea mwen zake akamsukumia Musa kando, akamwuliza, ‘Ni nani aliyekuweka uwe mtawala na mwamuzi kati yetu? 28 Je, unataka kuniua kama ulivy omwua yule Mmisri jana?’ 29 Musa aliposikia maneno haya alikim bia akatoka Misri akaenda kuishi kama mkimbizi sehemu za Midiani. Huko akawa baba wa watoto wawili wa kiume. 30 “Baada ya miaka arobaini, malaika wa Mungu akamtokea jangwani karibu na Mlima Sinai katika kichaka kilichokuwa kina waka moto. 31 Musa alishangazwa na kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto; na aliposogea karibu ili aone vizuri, akasikia sauti ya Bwana ikisema, 32 ‘Mimi ni Mungu wa baba zako; Mungu wa Ibrahimu, na wa Isaka na wa Yakobo.’ Musa alitetemeka kwa hofu akaogopa kutazama.
33 “Mungu akamwambia, ‘Vua viatu vyako kwa maana hapo uli posimama ni mahali patakatifu. 34 Nimeona mateso ya watu wangu walioko Misri, na nimesikia kilio chao, nami nimeshuka ili niwaokoe. Basi sasa nitakutuma Misri.’ 35 Huyu Musa ndiye wali yemkataa wakisema, ‘Ni nani aliyekufanya uwe mtawala na mwamuzi wetu?’ Mungu alimtuma kama mtawala na mkombozi kwa njia ya yule malaika aliyemtokea katika kile kichaka. 36 Aliwaongoza wana wa Israeli kutoka Misri, baada ya kufanya maajabu na ishara nyingi huko Misri na katika bahari ya Shamu, na katika jangwa kwa muda wa miaka arobaini.
37 “Huyu Musa ndiye aliyewaambia wana wa Israeli, ‘Mungu atawateulia nabii kutoka miongoni mwa ndugu zenu kama alivyoni teua mimi.’ 38 Huyu Musa alikuwa katika kusanyiko la wana wa Israeli jangwani pamoja na baba zetu na yule malaika aliyezun gumza naye kwenye Mlima wa Sinai; akapokea maneno yaliyo hai ili atupatie.
39 “Lakini baba zetu walikataa kumtii Musa, wakamsusia, na mioyoni mwao wakarudi Misri. 40 Wakamwambia Haruni, ‘Tufanyie miungu watakaotuongoza; kwa maana huyu Musa aliyetutoa Misri hat ujui yaliyompata.’ 41 Siku hizo wakatengeneza kinyago mfano wa ndama, wakakitolea sadaka za kuteketezwa, kisha wakafanya sherehe kushangilia kitu walichotengeneza kwa mikono yao wenyewe. 42 Ndipo Mungu akaondoka kati yao, akawaacha waabudu sayari za angani kama miungu yao: jua, mwezi na nyota. Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii, ‘ Je, nyumba ya Israeli, mlinitolea sadaka za wanyama wa kuteketezwa kwa miaka arobaini jangwani? La! 43 Tazama mlibeba hema ya Moleki, na sanamu ya nyota wa Refani, miungu mliyotengeneza ili muiabudu. Kwa hiyo nitawapeleka utum wani, mbali kuliko Babiloni.’
44 “Baba zetu walikuwa na ile hema ya ushuhuda pamoja nao jangwani. Nayo ilikuwa imetengenezwa kama malaika alivyomwelekeza Musa itengenezwe; na kwa mshono ambao Musa alikuwa ameonyeshwa. 45 Nao baba zetu wakaileta hiyo hema wakiongozwa na Yoshua wali poiteka nchi kutoka kwa yale mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao. Na hivi ndivyo ilivyokuwa mpaka wakati wa mfalme Daudi 46 ambaye alipendwa na Mungu, naye akaomba apewe ruhusa amjengee Mungu wa Yakobo makao. 47 Lakini mfalme Sulemani ndiye aliyem jengea Mungu nyumba. 48 Hata hivyo Mungu aliye Mkuu sana hakai kwenye nyumba iliyojengwa kwa mikono na binadamu. Kama nabii alivyosema, 49 ‘Mbingu ni kiti changu cha Enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu: mtanijengea nyumba ya namna gani? Auliza Bwana. Au mahali pangu pa kupumzikia ni wapi? 50 Je, si mimi niliyeumba vitu vyote hivi?’
51 “Ninyi watu wenye shingo ngumu! Wenye mioyo ya kipagani! Mmekuwa viziwi kwa neno la Mungu wala hamchoki kumpinga Roho Mta katifu! Kama walivyofanya baba zetu nanyi leo mnafanya vivyo hivyo. 52 Je, kuna nabii hata mmoja ambaye baba zetu hawa kumtesa? Waliwaua hata wale waliotabiri habari za kuja kwake yule Mwenye Haki, ambaye ninyi mmemsaliti kisha mkamwua. 53 Ninyi mlizipokea sheria za Mungu zilizoletwa kwenu na malaika lakini hamkuzitii.”
Stefano Auawa Kwa Kupigwa Mawe
54 Basi wale viongozi waliposikia maneno haya walijawa na hasira, wakasaga meno yao kwa ghadhabu. 55 Lakini Stefano akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, alitazama mbinguni, akaona utukufu wa Mungu, akamwona Yesu amesimama upande wa kulia wa Mungu.” 56 Akasema, “Tazameni! Naona mbingu zimefunguka na Mwana wa Adamu amesimama upande wa kulia wa Mungu.”
Adamu amesimama upande wa kulia wa Mungu.”
57 Wao wakapiga makelele, wakaziba masikio yao wasimsikie, wakamrukia kwa pamoja.
Copyright © 1989 by Biblica