Matendo 8
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
8 1-3 Sauli aliridhia kuwa kuuawa kwa Stefano lilikuwa jambo jema. Baadhi ya wacha Mungu walimzika Stefano, wakaomboleza na kumlilia kwa sauti kuu.
Matatizo Kwa waamini
Kuanzia siku hiyo Wayahudi walianza kulitesa sana kanisa na waamini katika mji wa Yerusalemu. Sauli pia alijaribu kuliharibu kanisa. Aliingia katika nyumba za waamini, akawaburuta wanaume na wanawake, na kuwafunga gerezani. Waamini wote walikimbia kutoka Yerusalemu, mitume peke yao ndiyo walibaki. Waamini walikwenda mahali tofauti tofauti katika Uyahudi na Samaria. 4 Walitawanyika kila mahali, na kila walikokwenda waliwahubiri watu Habari Njema.
Filipo Ahubiri Katika Samaria
5 Filipo[a] alikwenda katika mji mkuu wa jimbo la Samaria na kuwahubiri watu kuhusu Masihi. 6 Watu wa Samaria walimsikiliza Filipo na kuona miujiza aliyotenda. Wote walisikiliza kwa makini yale aliyosema. 7 Watu wengi miongoni mwao walikuwa na mapepo, lakini Filipo aliyakemea mapepo na yaliwatoka watu. Mapepo yalipiga kelele nyingi yalipokuwa yanawatoka watu. Walikuwepo pia watu wengi waliopooza na walemavu wa miguu pale. Filipo aliwaombea na wote walipona. 8 Kulikuwa furaha kubwa katika mji ule wa Samaria siku ile!
9 Mtu mmoja aliyeitwa Simoni alikuwa anaishi katika mji huo. Kabla Filipo hajaenda huko, Simoni alikuwa akifanya uchawi na kuwashangaza watu wote wa Samaria. Alijigamba na kujiita mtu mkuu. 10 Watu wote, kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliamini yale aliyosema Simoni. Walisema, “Mtu huyu ndiye anayeitwa ‘Nguvu Kuu ya Mungu.’” 11 Simoni aliwashangaza watu kwa muda mrefu kwa uchawi wake na watu wote wakawa wafuasi wake. 12 Lakini Filipo alipowahubiri watu Habari Njema kuhusu Ufalme wa Mungu na Nguvu za Yesu Kristo. Wanaume na wanawake waliamini alichosema Filipo na wakabatizwa. 13 Simoni mwenyewe aliamini, na baada ya kubatizwa, alikaa karibu na Filipo. Alipoona miujiza na matendo makuu ya ajabu yaliyofanyika kupitia Filipo, alishangaa.
14 Mitume mjini Yerusalemu, waliposikia kuwa watu wa Samaria wameupokea Ujumbe wa Mungu, waliwatuma Petro na Yohana kwenda kwa watu wa Samaria. 15 Petro na Yohana walipofika, waliomba ili Roho Mtakatifu awashukie waamini wa Samaria. 16 Watu hawa walikuwa wamebatizwa katika jina la Bwana Yesu, lakini Roho Mtakatifu alikuwa bado hajamshukia hata mmoja wao. Na hii ndiyo sababu Petro na Yohana waliomba. 17 Mitume hawa wawili walipoweka mikono yao juu ya watu, Roho Mtakatifu aliwashukia.
18 Simoni aliyekuwa mchawi alipoona Roho Mtakatifu anatolewa kwa watu kwa kuweka mikono juu yao. Aliwapa pesa mitume. 19 Akasema, “Nipeni na mimi nguvu hii ili nitakapoweka mikono yangu juu ya mtu yeyote, atampata Roho Mtakatifu.”
20 Petro akamwambia Simoni, “Wewe pamoja na pesa zako mwangamie kwa sababu unadhani unaweza kununua karama kutoka kwa Mungu kwa pesa. 21 Huwezi kushirikiana nasi katika kazi hii. Moyo wako si safi mbele za Mungu. 22 Badili moyo wako! Achana na mawazo haya maovu na umwombe Bwana. Yumkini atakusamehe! 23 Kwa kuwa ninaona umejaa wivu mwingi nawe ni mfungwa wa uovu.”
24 Simoni akajibu, “Niombeeni kwa Bwana, ili haya uliyosema yasinipate.”
25 Ndipo wale mitume wawili waliwaambia watu waliyoona Yesu akitenda. Wakawaambia ujumbe wa Bwana. Kisha wakarudi Yerusalemu. Wakiwa njiani kurudi, walipitia katika miji mingi ya Wasamaria na kuwahubiri watu Habari Njema.
Filipo Amfundisha Mtu Kutoka Ethiopia
26 Malaika wa Bwana alimwambia Filipo, “Jiandae na uende kusini katika barabara ya jangwani inayoteremka kutoka Yerusalemu kwenda Gaza.”
27 Filipo alijiandaa na kwenda. Akiwa njiani alimwona mwanaume kutoka Ethiopia. Alikuwa towashi na ofisa muhimu wa Kandake, malkia wa Ethiopia. Alikuwa na mweka hazina mkuu wa malkia. Mtu huyu alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu. 28 Na alikuwa anarudi Ethiopia. Alikuwa ameketi katika gari lake la kukokotwa na farasi akiwa anasoma kitabu cha nabii Isaya.
29 Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda kwenye gari hilo na uwe karibu yake.” 30 Hivyo Filipo akaenda karibu na gari, akamsikia mtu yule akisoma kutoka katika kitabu cha nabii Isaya. Filipo akamwuliza, “Unaelewa unachosoma?”
31 Yule mtu akajibu, “Nitaelewaje? Ninahitaji mtu wa kunifafanulia.” Ndipo akamwomba Filipo apande garini na aketi pamoja naye. 32 Sehemu ya Maandiko aliyokuwa anasoma ilikuwa hii:
“Alikuwa kama kondoo
anayepelekwa kwa mchinjaji.
Alikuwa kama mwana kondoo asivyopiga kelele
anapokatwa manyoya yake.
Hakusema kitu.
33 Alidhalilishwa,
na kunyimwa haki zake zote.
Maisha yake duniani yamekoma.
Hivyo hakutakuwa simulizi yoyote kuhusu wazaliwa wake.”(A)
34 Afisa[b] akamwambia Filipo, “Tafadhali niambie, nabii anazungumza kuhusu nani? Anazungumza kuhusu yeye mwenyewe au mtu mwingine?” 35 Filipo akaanza kuzungumza. Alianzia na Andiko hili na kumwambia mtu yule Habari Njema kuhusu Yesu.
36 Walipokuwa wanasafiri waliyakuta maji mahali fulani. Afisa akasema, “Tazama! Hapa kuna maji! Nini kinanizuia nisibatizwe?” 37 [c] 38 Ndipo Afisa akaamuru gari lake lisimame. Wote wawili, Filipo na Afisa, wakatelemka wakaingia kwenye maji na Filipo akambatiza towashi. 39 Walipotoka kwenye maji, Roho wa Bwana akamchukua Filipo; afisa hakumwona Filipo tena. Afisa aliendelea na safari yake kurudi nyumbani, akiwa mwenye furaha sana. 40 Lakini Filipo alionekana katika mji ulioitwa Azoto. Alikuwa akienda kwenye mji wa Kaisaria. Aliwahubiri watu Habari Njema katika miji yote wakati anasafiri kutoka Azoto kwenda Kaisaria.
Footnotes
- 8:5 Filipo Siyo mtume aliyeitwa Filipo.
- 8:34 Afisa Kwa maana ya kawaida, “towashi”. Pia katika mstari wa 36,38,39.
- 8:37 Nakala zingine za baadaye za Matendo zimeongeza mstari wa 37: Filipo akajibu, “Ikiwa unaamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa. Ofisa akasema, ‘Ninaamini kuwa Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.’”
Matendo Ya Mitume 8
Neno: Bibilia Takatifu
8 Na Sauli aliunga mkono kuuawa kwa Stefano Tangu siku hiyo waamini katika kanisa la Yerusalemu walianza kuteswa sana. Waamini wote isipokuwa mitume wakatawanyika, wakakimbilia katika majimbo ya Yudea na Samaria. 2 Watu waliomcha Mungu walimzika Stefano na kumwombolezea sana. 3 Lakini Sauli alitaka kulianga miza kanisa kabisa. Akawa akienda kila nyumba akawaburura waamini, wanaume kwa wanawake, akawatia jela.
Injili Yahubiriwa Samaria
4 Wale waamini waliotawanyika walihubiri neno la Mungu kila mahali walipokuwa. 5 Filipo naye alikwenda katika mji mmoja wa Samaria akahubiri habari za Kristo. 6 Watu wengi walipomsikiliza Filipo na kuona ishara za ajabu alizofanya, walizingatia kwa makini ujumbe wake. 7 Pepo wachafu walikuwa wakiwatoka watu wengi, huku wakipiga makelele; na wengi waliopooza na viwete, waliponywa. 8 Pakawa na furaha kuu katika mji huo.
9 Lakini katika mji huo alikuwepo mtu mmoja aitwaye Simoni, ambaye alikuwa mchawi. Kwa muda mrefu alikuwa amewapumbaza na kuwashangaza watu kwa mazingaombwe, akawa anajigamba kuwa yeye ni mtu maarufu. 10 Watu wa tabaka zote, wakubwa kwa wadogo, walivu tiwa sana naye, wakawa wanasema, “Bila shaka mtu huyu ndiye ile nguvu ya Mungu iitwayo ‘Uwezo Mkuu.’ ” 11 Wakamsikiliza kwa makini kwa sababu aliwastaajabisha kwa mazingaombwe yake. 12 Lakini watu walipoamini mahubiri ya Filipo kuhusu Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na jina la Yesu Kristo, walibatizwa, waume kwa wake. 13 Hata Simoni naye aliamini na alipokwisha batizwa aliambatana na Filipo. Alipoona ishara na miujiza aliy ofanya Filipo alistaajabu sana .
14 Basi mitume waliokuwa Yerusalemu waliposikia kuwa watu wa Samaria wameamini neno la Bwana, waliwatuma Petro na Yohana waende huko. 15 Nao walipofika waliwaombea ili wapokee Roho Mta katifu; 16 kwa maana walikuwa wamebatizwa tu katika jina la Bwana Yesu na Roho Mtakatifu alikuwa bado hajawashukia. 17 Petro na Yohana wakaweka mikono yao juu ya wale waliobatizwa, nao waka pokea Roho Mtakatifu. 18 Simoni alipoona kuwa watu walipokea Roho Mtakatifu mitume walipoweka mikono juu yao, aliwapa fedha 19 akasema, “Nipeni na mimi uwezo huu ili kila mtu nitakayeweka mikono yangu juu yake apokee Roho Mtakatifu.” 20 Petro akam jibu, “Uangamie wewe na fedha zako, kwa maana unadhani unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!” 21 Wewe huwezi kuwa na sehemu wala fungu katika jambo hili kwa kuwa moyo wako hauko sawa mbele za Mungu. 22 Kwa hiyo tubu, uache huu uovu wako; na umwombe Mungu ili kama inawezekana akusamehe makusudio maovu uliyo nayo moyoni. 23 Kwa maana ninaona wazi kwamba wewe umejawa na wivu na ni mfungwa wa dhambi. 24 Simoni akajibu, “Niombeeni kwa Bwana, ili hayo mliyosema yasije yakanipata.” 25 Nao wali pokwisha kutoa ushuhuda na kufundisha neno la Bwana, walirudi Yerusalemu; na walipokuwa wakisafiri walihubiri Habari Njema katika vijiji vingi vya Samaria.
Filipo Ambatiza Afisa Wa Ethiopia
26 Malaika wa Bwana alimwambia Filipo, “Nenda upande wa kusini kwenye ile barabara itokayo Yerusalemu kuelekea Gaza.” Hii ilikuwa barabara iendayo jangwani. 27 Filipo akaondoka akaenda. Wakati huo Mwethiopia mmoja, towashi, ambaye alikuwa waziri wa fedha wa Kandake, Malkia wa Ethiopia, alikuwa anarudi nyumbani baada ya kumwabudu Mungu huko Yerusalemu. 28 Alikuwa amekaa kwenye gari la kuvutwa na farasi akielekea makwao, akisoma kitabu cha nabii Isaya. 29 Roho wa Mungu akamwambia Filipo, “Nenda kasimame karibu na lile gari.” 30 Kwa hiyo Filipo aka harakisha kulikaribia, na alipofika karibu akamsikia yule afisa akisoma katika kitabu cha nabii Isaya, akamwuliza, “Je, unaelewa unachosoma?” 31 Yule afisa akamjibu, “Nitaelewaje mtu asipo nielekeza? Akamkaribisha Filipo katika gari, akaketi pamoja naye. 32 Maneno aliyokuwa akisoma ni haya, ‘Alipelekwa kama kon doo anayetolewa kuchinjwa na kama mwana-kondoo anavyotulia anapo katwa manyoya, naye hakusema neno lo lote. 33 Aliaibishwa, aka nyimwa haki yake. Ni nani awezaye kuelezea juu ya kizazi chake? Kwa maana uhai wake umeondolewa duniani.’ 34 Yule towashi akam wuliza Filipo, “Tafadhali niambie, Isaya alikuwa akisema haya juu yake mwenyewe au juu ya mtu mwingine?” 35 Ndipo Filipo akaanza kusema naye, akitumia Maandiko haya akamweleza Habari Njema za Yesu. 36 Walipokuwa wakiendelea na safari wakafika mahali palipokuwa na maji, na yule towashi akamwambia Filipo, “ Tazama, hapa kuna maji! Kuna kitu gani cha kunizuia mimi nisiba tizwe? [ 37 Filipo akamwambia, “Kama unaamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa.” Akajibu, “Naamini kuwa Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”] 38 Akaamuru gari lisimamishwe. Wakateremka, yule towashi na Filipo, wakaenda pale kwenye maji. Filipo akamba tiza. 39 Walipotoka katika yale maji, Roho wa Bwana akamchukua Filipo na yule towashi hakumwona tena. Kwa hiyo akaendelea na safari yake akiwa amejawa na furaha. 40 Filipo akajikuta yuko Azoto; akasafiri akihubiri Injili katika miji yote mpaka alipo fika Kaisaria.
Acts 8
New International Version
8 And Saul(A) approved of their killing him.
The Church Persecuted and Scattered
On that day a great persecution broke out against the church in Jerusalem, and all except the apostles were scattered(B) throughout Judea and Samaria.(C) 2 Godly men buried Stephen and mourned deeply for him. 3 But Saul(D) began to destroy the church.(E) Going from house to house, he dragged off both men and women and put them in prison.
Philip in Samaria
4 Those who had been scattered(F) preached the word wherever they went.(G) 5 Philip(H) went down to a city in Samaria and proclaimed the Messiah there. 6 When the crowds heard Philip and saw the signs he performed, they all paid close attention to what he said. 7 For with shrieks, impure spirits came out of many,(I) and many who were paralyzed or lame were healed.(J) 8 So there was great joy in that city.
Simon the Sorcerer
9 Now for some time a man named Simon had practiced sorcery(K) in the city and amazed all the people of Samaria. He boasted that he was someone great,(L) 10 and all the people, both high and low, gave him their attention and exclaimed, “This man is rightly called the Great Power of God.”(M) 11 They followed him because he had amazed them for a long time with his sorcery. 12 But when they believed Philip as he proclaimed the good news of the kingdom of God(N) and the name of Jesus Christ, they were baptized,(O) both men and women. 13 Simon himself believed and was baptized. And he followed Philip everywhere, astonished by the great signs and miracles(P) he saw.
14 When the apostles in Jerusalem heard that Samaria(Q) had accepted the word of God,(R) they sent Peter and John(S) to Samaria. 15 When they arrived, they prayed for the new believers there that they might receive the Holy Spirit,(T) 16 because the Holy Spirit had not yet come on any of them;(U) they had simply been baptized in the name of the Lord Jesus.(V) 17 Then Peter and John placed their hands on them,(W) and they received the Holy Spirit.(X)
18 When Simon saw that the Spirit was given at the laying on of the apostles’ hands, he offered them money 19 and said, “Give me also this ability so that everyone on whom I lay my hands may receive the Holy Spirit.”
20 Peter answered: “May your money perish with you, because you thought you could buy the gift of God with money!(Y) 21 You have no part or share(Z) in this ministry, because your heart is not right(AA) before God. 22 Repent(AB) of this wickedness and pray to the Lord in the hope that he may forgive you for having such a thought in your heart. 23 For I see that you are full of bitterness and captive to sin.”
24 Then Simon answered, “Pray to the Lord for me(AC) so that nothing you have said may happen to me.”
25 After they had further proclaimed the word of the Lord(AD) and testified about Jesus, Peter and John returned to Jerusalem, preaching the gospel in many Samaritan villages.(AE)
Philip and the Ethiopian
26 Now an angel(AF) of the Lord said to Philip,(AG) “Go south to the road—the desert road—that goes down from Jerusalem to Gaza.” 27 So he started out, and on his way he met an Ethiopian[a](AH) eunuch,(AI) an important official in charge of all the treasury of the Kandake (which means “queen of the Ethiopians”). This man had gone to Jerusalem to worship,(AJ) 28 and on his way home was sitting in his chariot reading the Book of Isaiah the prophet. 29 The Spirit told(AK) Philip, “Go to that chariot and stay near it.”
30 Then Philip ran up to the chariot and heard the man reading Isaiah the prophet. “Do you understand what you are reading?” Philip asked.
31 “How can I,” he said, “unless someone explains it to me?” So he invited Philip to come up and sit with him.
32 This is the passage of Scripture the eunuch was reading:
“He was led like a sheep to the slaughter,
and as a lamb before its shearer is silent,
so he did not open his mouth.
33 In his humiliation he was deprived of justice.
Who can speak of his descendants?
For his life was taken from the earth.”[b](AL)
34 The eunuch asked Philip, “Tell me, please, who is the prophet talking about, himself or someone else?” 35 Then Philip began(AM) with that very passage of Scripture(AN) and told him the good news(AO) about Jesus.
36 As they traveled along the road, they came to some water and the eunuch said, “Look, here is water. What can stand in the way of my being baptized?”(AP) [37] [c] 38 And he gave orders to stop the chariot. Then both Philip and the eunuch went down into the water and Philip baptized him. 39 When they came up out of the water, the Spirit of the Lord suddenly took Philip away,(AQ) and the eunuch did not see him again, but went on his way rejoicing. 40 Philip, however, appeared at Azotus and traveled about, preaching the gospel in all the towns(AR) until he reached Caesarea.(AS)
Acts 8
Names of God Bible
8 Saul approved of putting Stephen to death.
On that day widespread persecution broke out against the church in Jerusalem. Most believers, except the apostles, were scattered throughout Judea and Samaria.
2 Devout men buried Stephen as they mourned loudly for him.
3 Saul tried to destroy the church. He dragged men and women out of one home after another and threw them into prison.
Some Samaritans Become Believers
4 The believers who were scattered went from place to place, where they spread the word. 5 Philip went to the city of Samaria and told people about the Messiah. 6 The crowds paid close attention to what Philip said. They listened to him and saw the miracles that he performed. 7 Evil spirits screamed as they came out of the many people they had possessed. Many paralyzed and lame people were cured. 8 As a result, that city was extremely happy.
9 A man named Simon lived in that city. He amazed the people of Samaria with his practice of magic. He claimed that he was great. 10 Everyone from children to adults paid attention to him. They said, “This man is the power of God, and that power is called great.” 11 They paid attention to Simon because he had amazed them for a long time with his practice of magic. 12 However, when Philip spread the Good News about the kingdom of God and the one named Yeshua Christ, men and women believed him and were baptized. 13 Even Simon believed, and after he was baptized, he became devoted to Philip. Simon was amazed to see the miracles and impressive things that were happening.
14 When the apostles in Jerusalem heard that the Samaritans had accepted the word of God, they sent Peter and John to them. 15 Peter and John went to Samaria and prayed that the Samaritans would receive the Holy Spirit. 16 (Before this the Holy Spirit had not come to any of the Samaritans. They had only been baptized in the name of the Lord Yeshua.) 17 Then Peter and John placed their hands on them, and the Samaritans received the Holy Spirit.
18 Simon saw that the Spirit was given to the Samaritans when the apostles placed their hands on them. So he offered Peter and John money 19 and said, “Give me this power so that anyone I place my hands on will receive the Holy Spirit.”
20 Peter told Simon, “May your money be destroyed with you because you thought you could buy God’s gift. 21 You won’t have any share in this because God can see how twisted your thinking is. 22 So change your wicked thoughts, and ask the Lord if he will forgive you for thinking like this. 23 I can see that you are bitter with jealousy and wrapped up in your evil ways.”
24 Simon answered, “Pray to the Lord for me that none of the things you said will happen to me.”
25 After they had boldly spoken about the message of the Lord, they spread the Good News in many Samaritan villages on their way back to Jerusalem.
Philip Tells an Ethiopian about Jesus
26 An angel from the Lord said to Philip, “Get up, and take the desert road that goes south from Jerusalem to Gaza.” 27 So Philip went.
An Ethiopian man who had come to Jerusalem to worship was on his way home. The man was a eunuch, a high-ranking official in charge of all the treasures of Queen Candace of Ethiopia. 28 As the official rode along in his carriage, he was reading the prophet Isaiah out loud.
29 The Spirit said to Philip, “Go to that carriage, and stay close to it.”
30 Philip ran to the carriage and could hear the official reading the prophet Isaiah out loud. Philip asked him, “Do you understand what you’re reading?”
31 The official answered, “How can I understand unless someone guides me?” So he invited Philip to sit with him in his carriage.
32 This was the part of the Scriptures that the official was reading:
“He was led like a lamb to the slaughter.
He was like a sheep that is silent
when its wool is cut off.
He didn’t open his mouth.
33 When he humbled himself,
he was not judged fairly.
Who from his generation
will talk about his life on earth being cut short?”
34 The official said to Philip, “I would like to know who the prophet is talking about. Is he talking about himself or someone else?” 35 Then Philip spoke. Starting with that passage, Philip told the official the Good News about Yeshua.
36 As they were going along the road, they came to some water. The official said to Philip, “Look, there’s some water. What can keep me from being baptized?”[a] 38 The official ordered the carriage to stop. He and Philip stepped into the water, and Philip baptized him. 39 When they had stepped out of the water, the Spirit of the Lord suddenly took Philip away. The official joyfully continued on his way and didn’t see Philip again.
40 Philip found himself in the city of Azotus. He traveled through all the cities and spread the Good News until he came to the city of Caesarea.
Footnotes
- Acts 8:36 Some manuscripts and translations add verse 37: “Philip said to the official, ‘If you believe with all your heart, you can be baptized.’ The official answered, ‘I believe Yeshua Christ is the Son of God.’”
Acts 8
English Standard Version
Saul Ravages the Church
8 And (A)Saul (B)approved of his execution.
And there arose on that day a great persecution against the church in Jerusalem, and (C)they were all scattered throughout the regions of Judea and Samaria, except the apostles. 2 Devout men buried Stephen and made great lamentation over him. 3 But (D)Saul was ravaging the church, and entering house after house, he (E)dragged off men and women and committed them to prison.
Philip Proclaims Christ in Samaria
4 Now (F)those who were scattered went about preaching the word. 5 (G)Philip went down to the city[a] of Samaria and proclaimed to them the Christ. 6 (H)And the crowds with one accord paid attention to what was being said by Philip, when they heard him (I)and saw the signs that he did. 7 For (J)unclean spirits, crying out with a loud voice, came out of many who had them, and many who were paralyzed or lame were healed. 8 So (K)there was much joy in that city.
Simon the Magician Believes
9 But there was a man named Simon, (L)who had previously practiced magic in the city and amazed the people of Samaria, (M)saying that he himself was somebody great. 10 They all paid attention to him, from the least to the greatest, saying, (N)“This man is the power of God that is called (O)Great.” 11 And they paid attention to him because for a long time he had (P)amazed them with his magic. 12 But when (Q)they believed Philip as he preached good news (R)about the kingdom of God and the name of Jesus Christ, (S)they were baptized, both men and women. 13 Even Simon himself believed, and after being baptized he continued with Philip. And (T)seeing signs and (U)great miracles[b] performed, (V)he was amazed.
14 Now when (W)the apostles at Jerusalem heard that (X)Samaria had received the word of God, they sent to them Peter and John, 15 who came down and prayed for them (Y)that they might receive the Holy Spirit, 16 for (Z)he had not yet (AA)fallen on any of them, but (AB)they had only been baptized in the name of the Lord Jesus. 17 Then (AC)they laid their hands on them and (AD)they received the Holy Spirit. 18 Now when Simon saw that the Spirit was given through the laying on of the apostles' hands, he offered them money, 19 saying, “Give me this power also, so that anyone on whom I lay my hands may receive the Holy Spirit.” 20 But Peter said to him, (AE)“May your silver perish with you, because you thought you could obtain the gift of God (AF)with money! 21 You have neither part nor lot in this matter, for (AG)your heart is not right before God. 22 Repent, therefore, of this wickedness of yours, and pray to the Lord that, (AH)if possible, the intent of your heart may be forgiven you. 23 For I see that you are in (AI)the gall[c] of bitterness and in (AJ)the bond of iniquity.” 24 And Simon answered, (AK)“Pray for me to the Lord, that nothing of what you have said may come upon me.”
25 Now when they had testified and spoken the word of the Lord, they returned to Jerusalem, (AL)preaching the gospel to many villages of the Samaritans.
Philip and the Ethiopian Eunuch
26 Now (AM)an angel of the Lord said to Philip, “Rise and go toward the south[d] to the road that goes down from Jerusalem to Gaza.” This is a desert place. 27 And he rose and went. And there was an (AN)Ethiopian, a (AO)eunuch, a court official of Candace, queen of the Ethiopians, (AP)who was in charge of all her treasure. (AQ)He had come to Jerusalem to worship 28 and was returning, seated in his chariot, and he was reading the prophet Isaiah. 29 And the Spirit said to Philip, “Go over and join this chariot.” 30 So Philip ran to him and heard him reading Isaiah the prophet and asked, “Do you understand what you are reading?” 31 And he said, (AR)“How can I, unless someone (AS)guides me?” And (AT)he invited Philip to come up and sit with him. 32 Now the passage of the Scripture that he was reading was this:
(AU)“Like a sheep he was led to the slaughter
and like a lamb before its shearer is silent,
so he opens not his mouth.
33 In his (AV)humiliation justice was denied him.
Who can describe his generation?
For his life is taken away from the earth.”
34 And the eunuch said to Philip, “About whom, I ask you, does the prophet say this, about himself or about someone else?” 35 Then Philip opened his mouth, and (AW)beginning with this Scripture (AX)he told him the good news about Jesus. 36 And as they were going along the road they came to some water, and the eunuch said, “See, here is water! (AY)What prevents me from being baptized?”[e] 38 And he commanded the chariot to stop, and they both went down into the water, Philip and the eunuch, and he baptized him. 39 And when they came up out of the water, (AZ)the Spirit of the Lord (BA)carried Philip away, and the eunuch saw him no more, and went on his way rejoicing. 40 But Philip found himself at Azotus, and as he passed through he preached the gospel to all the towns until he came to Caesarea.
Footnotes
- Acts 8:5 Some manuscripts a city
- Acts 8:13 Greek works of power
- Acts 8:23 That is, a bitter fluid secreted by the liver; bile
- Acts 8:26 Or go at about noon
- Acts 8:36 Some manuscripts add all or most of verse 37: And Philip said, “If you believe with all your heart, you may.” And he replied, “I believe that Jesus Christ is the Son of God.”
© 2017 Bible League International
Copyright © 1989 by Biblica
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.
The Names of God Bible (without notes) © 2011 by Baker Publishing Group.
The ESV® Bible (The Holy Bible, English Standard Version®), © 2001 by Crossway, a publishing ministry of Good News Publishers. ESV Text Edition: 2025.

