Matendo 1
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka Aandika Kitabu Kingine
1 Mpendwa Theofilo:
Katika kitabu cha kwanza niliandika kuhusu kila kitu ambacho Yesu alitenda na kufundisha tangu mwanzo 2 mpaka siku alipochukuliwa juu mbinguni. Kabla hajaondoka, alizungumza na mitume aliowachagua kwa msaada wa Roho Mtakatifu kuhusu mambo waliyotakiwa kufanya. 3 Hii ilikuwa baada ya kifo chake, ambapo aliwathibitishia kwa namna nyingi kuwa alikuwa hai. Mitume walimwona Yesu mara nyingi kwa muda wa siku arobaini baada ya kufufuka kutoka kwa wafu. Naye Yesu alizungumza nao kuhusu ufalme wa Mungu. 4 Wakati mmoja Yesu alipokuwa akila pamoja nao, aliwaambia wasiondoke Yerusalemu. Aliwaambia, “Kaeni hapa mpaka mtakapopokea kile ambacho Baba aliahidi kutuma. Kumbukeni, niliwaambia juu yake. 5 Yohana aliwabatiza watu kwa maji, lakini baada ya siku chache mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
Yesu Achukuliwa Juu Mbinguni
6 Mitume walipokuwa pamoja, walimwuliza Yesu, “Bwana, huu ni wakati wako wa kuwarudishia Waisraeli ufalme wao tena?”
7 Yesu akawaambia, “Baba peke yake ndiye mwenye mamlaka ya kuamua tarehe na nyakati. Si juu yenu kujua. 8 Lakini Roho Mtakatifu atawajia na kuwapa nguvu. Nanyi mtakuwa mashahidi wangu. Mtawahubiri watu kuhusu mimi kila mahali, kuanzia humu Yerusalemu, Uyahudi yote, katika Samaria na hatimaye kila mahali ulimwenguni.”
9 Baada ya kusema haya, alichukuliwa juu mbinguni. Walipokuwa wanaangalia juu angani, wingu lilimficha na hawakuweza kumwona. 10 Walikuwa bado wanatazama angani alipokuwa anakwenda. Ghafla malaika wawili waliovaa mavazi meupe wakasimama pembeni mwao. 11 Wakasema, “Enyi watu wa Galilaya, kwa nini mmesimama hapa na mnatazama angani? Mlimwona Yesu akichukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni. Atarudi katika namna hii hii kama mlivyomwona akienda.”
Mtume Mpya Achaguliwa
12 Ndipo mitume walirudi Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni, ulio umbali wa kama kilomita moja[a] kutoka Yerusalemu. 13 Walipoingia mjini, walikwenda kwenye chumba cha ghorofani walikokuwa wanakaa. Hawa ndiyo wale waliokuwepo: Petro, Yohana, Yakobo, na Andrea, Filipo, Thomasi, Bartholomayo, Mathayo, Yakobo (mwana wa Alfayo), na Simoni Mzelote, na Yuda (mwana wa Yakobo).
14 Mitume hawa wote walikuwa pamoja na waliomba kwa nia moja. Baadhi ya wanawake, Mariamu mama wa Yesu na wadogo zake Bwana Yesu walikuwepo pale pamoja na mitume.
15 Baada ya siku chache waamini waliokuwa kama mia moja na ishirini walikutana pamoja. Petro alisimama na kusema, 16-17 “Kaka na dada zangu, katika Maandiko Roho Mtakatifu alisema kupitia Daudi kwamba jambo fulani lazima litatokea. Alizungumza kuhusu Yuda, yule aliyekuwa katika kundi letu wenyewe. Yuda alihudumu pamoja nasi. Roho alisema Yuda atawaongoza watu kumkamata Yesu.”
18 (Kwa kufanya hili Yuda alilipwa pesa. Alinunulia shamba pesa hizo. Lakini aliangukia kichwa chake, mwili wake ukapasuka, na matumbo yake yote yakamwagika nje. 19 Na watu wote wa Yerusalemu wanalijua hili. Ndiyo maana waliliita shamba hilo Akeldama, ambalo maana yake kwa Kiaramu ni “Shamba la Damu”.)
20 Petro akasema, “Katika kitabu cha Zaburi, jambo hili limeandikwa kuhusu Yuda:
‘Watu wasipakaribie mahali pake;
Yeyote asiishi hapo.’(A)
Pia imeandikwa kuwa:
‘Mtu mwingine achukue kazi yake.’(B)
21-22 Hivyo ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi ili awe shahidi wa ufufuo wa Bwana Yesu. Ni lazima awe mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana Yesu alipokuwa pamoja nasi. Ni lazima awe yule ambaye amekuwa pamoja nasi tangu Yohana alipokuwa anabatiza watu mpaka siku ambayo Bwana Yesu alichukuliwa kutoka kwetu na kwenda mbinguni.”
23 Kisha waliwasimamisha watu wawili mbele ya kundi. Mmoja aliitwa Yusufu Barsaba, ambaye pia aliitwa Yusto. Mwingine aliitwa Mathiasi. 24-25 Wakaomba wakisema, “Bwana unajua mioyo ya watu wote. Tuonyeshe kati ya watu hawa wawili uliyemchagua kufanya kazi hii. Yuda aliiacha na kuifuata njia yake. Bwana tuonyeshe ni nani achukue sehemu yake kama mtume!” 26 Kisha wakapiga kura kumchagua mmoja kati ya watu hao wawili. Kura ikaonesha Mathiasi ndiye Bwana anamtaka. Hivyo akawa mtume pamoja na wale wengine kumi na moja.
Footnotes
- 1:12 kilomita moja Ama mwendo wa Sabato, ambao ni sawa na umbali wa kilomita moja: Waisraeli hawakuruhusiwa kusafiri zaidi ya futi 3,600 (kati ya yadi 1,000-1,200) siku ya Sabato. Umbali huu ulitokana na umbali kati ya sanduku la Agano na watu waliokuwa wakilifuata (tazama Yos 3:4). Pia ilichukuliwa kuwa ni umbali ambao mtu alitakiwa kuwalisha wanyama wake (Hes 35:4,5).
Acts 1
New International Version
Jesus Taken Up Into Heaven
1 In my former book,(A) Theophilus, I wrote about all that Jesus began to do and to teach(B) 2 until the day he was taken up to heaven,(C) after giving instructions(D) through the Holy Spirit to the apostles(E) he had chosen.(F) 3 After his suffering, he presented himself to them and gave many convincing proofs that he was alive. He appeared to them(G) over a period of forty days and spoke about the kingdom of God.(H) 4 On one occasion, while he was eating with them, he gave them this command: “Do not leave Jerusalem, but wait(I) for the gift my Father promised, which you have heard me speak about.(J) 5 For John baptized with[a] water,(K) but in a few days you will be baptized with[b] the Holy Spirit.”(L)
6 Then they gathered around him and asked him, “Lord, are you at this time going to restore(M) the kingdom to Israel?”
7 He said to them: “It is not for you to know the times or dates the Father has set by his own authority.(N) 8 But you will receive power when the Holy Spirit comes on you;(O) and you will be my witnesses(P) in Jerusalem, and in all Judea and Samaria,(Q) and to the ends of the earth.”(R)
9 After he said this, he was taken up(S) before their very eyes, and a cloud hid him from their sight.
10 They were looking intently up into the sky as he was going, when suddenly two men dressed in white(T) stood beside them. 11 “Men of Galilee,”(U) they said, “why do you stand here looking into the sky? This same Jesus, who has been taken from you into heaven, will come back(V) in the same way you have seen him go into heaven.”
Matthias Chosen to Replace Judas
12 Then the apostles returned to Jerusalem(W) from the hill called the Mount of Olives,(X) a Sabbath day’s walk[c] from the city. 13 When they arrived, they went upstairs to the room(Y) where they were staying. Those present were Peter, John, James and Andrew; Philip and Thomas, Bartholomew and Matthew; James son of Alphaeus and Simon the Zealot, and Judas son of James.(Z) 14 They all joined together constantly in prayer,(AA) along with the women(AB) and Mary the mother of Jesus, and with his brothers.(AC)
15 In those days Peter stood up among the believers (a group numbering about a hundred and twenty) 16 and said, “Brothers and sisters,[d](AD) the Scripture had to be fulfilled(AE) in which the Holy Spirit spoke long ago through David concerning Judas,(AF) who served as guide for those who arrested Jesus. 17 He was one of our number(AG) and shared in our ministry.”(AH)
18 (With the payment(AI) he received for his wickedness, Judas bought a field;(AJ) there he fell headlong, his body burst open and all his intestines spilled out. 19 Everyone in Jerusalem heard about this, so they called that field in their language(AK) Akeldama, that is, Field of Blood.)
20 “For,” said Peter, “it is written in the Book of Psalms:
and,
21 Therefore it is necessary to choose one of the men who have been with us the whole time the Lord Jesus was living among us, 22 beginning from John’s baptism(AN) to the time when Jesus was taken up from us. For one of these must become a witness(AO) with us of his resurrection.”
23 So they nominated two men: Joseph called Barsabbas (also known as Justus) and Matthias. 24 Then they prayed,(AP) “Lord, you know everyone’s heart.(AQ) Show us(AR) which of these two you have chosen 25 to take over this apostolic ministry, which Judas left to go where he belongs.” 26 Then they cast lots, and the lot fell to Matthias; so he was added to the eleven apostles.(AS)
Footnotes
- Acts 1:5 Or in
- Acts 1:5 Or in
- Acts 1:12 That is, about 5/8 mile or about 1 kilometer
- Acts 1:16 The Greek word for brothers and sisters (adelphoi) refers here to believers, both men and women, as part of God’s family; also in 6:3; 11:29; 12:17; 16:40; 18:18, 27; 21:7, 17; 28:14, 15.
- Acts 1:20 Psalm 69:25
- Acts 1:20 Psalm 109:8
© 2017 Bible League International
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.