Paulo Ahubiri Thesalonike

17 Walisafiri kupitia Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalo nike, ambako kulikuwa na sinagogi la Wayahudi. Paulo aliingia ndani ya sinagogi kama ilivyokuwa kawaida yake, na kwa muda wa majuma matatu akawa akihojiana na Wayahudi akitumia Maandiko kuwaonyesha wazi kwamba ilikuwa ni lazima Kristo ateswe na afu fuke kutoka kwa wafu, akamalizia kwa kusema, “Huyu Yesu ambaye nawaambia habari zake, ndiye Kristo.” Baadhi yao wakakubaliana nao, wakajiunga na Paulo na Sila. Pia umati mkubwa wa Wagiriki waliomcha Mungu, na baadhi ya wanawake viongozi wakaungana nao. Lakini Wayahudi wengi waliwaonea Paulo na Sila wivu, waka chochea baadhi ya wazururaji waovu waanzishe fujo mji mzima; kisha wakashambulia nyumba ya Yasoni ambamo Paulo na Sila wali kuwa wakikaa, ili wawatoe nje. Walipokuta hawako huko, wakawa kamata Yasoni na baadhi ya ndugu waamini wakawaleta mbele ya viongozi wa mji wakipiga kelele: “Hawa watu ambao wamepindua dunia nzima wamefika huku na huyu Yasoni amewakaribisha. Wao wanavunja sheria ya Kaisari kwa kusema eti kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu.” Mashtaka haya ya Wayahudi yaliwafadhaisha watu wote pamoja na wale viongozi wa mji. Kwa hiyo wakataka dhamana kutoka kwa Yasoni na waamini wenzake kabla ya kuwaachilia waende zao.

10 Giza lilipoingia, wale ndugu waamini waliwatoa Paulo na Sila wakaondoka kwenda Beroya, na walipowasili wakaingia katika Sinagogi la Wayahudi. 11 Watu wa Beroya walikuwa waungwana zaidi kuliko watu wa Thesalonike. Walisikiliza neno la Mungu kwa hamu wakachambua Maandiko kila siku ili waone kama waliyokuwa wakiam biwa na Paulo ni kweli. 12 Wengi wao waliamini, ikiwa ni pamoja na wanawake maarufu wa Kigiriki na wanaume wengi. 13 Lakini wale Wayahudi wa Thesalonike waliposikia kuwa Paulo anahubiri neno la Mungu huko Beroya, walikuja wakaanza kuwashawishi watu na kuwa chochea waanzishe vurugu. 14 Na ndugu wa Beroya wakafanya haraka wakamsafirisha Paulo kuelekea bandarini , lakini Sila na Timotheo walibaki Beroya. 15 Wale waliomsindikiza Paulo walienda naye mpaka Athene. Ndipo wakarudi Beroya wakiwa na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba, Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.

Paulo Ahubiri Huko Athene

16 Paulo alipokuwa akiwangojea wenzake huko Athene alisikit ishwa sana kuona jinsi mji ulivyojaa miungu ya sanamu. 17 Kwa hiyo akawa akienda katika sinagogi kujadiliana na Wayahudi na Wagiriki waliomcha Mungu na katika mahali pa soko ambako aliongea na watu aliokutana nao. 18 Huko sokoni alikutana na vikundi viwili vya wanafalsafa waitwao Waepikureo na Wastoiko. Baadhi yao wakamdhihaki wakisema, “Huyu mpayukaji asiyejua kitu anajaribu kusema nini?” Wengine wakasema, “Anaelekea kuwa mhubiri wa miungu wageni.” Walisema hivi kwa sababu Paulo alikuwa akihubiri juu ya Yesu na ufufuo. 19 Wakamkamata wakampeleka kwenye baraza la Areopago wakamwambia, “Tungependa kufahamu haya mafundisho mapya unayotangaza. 20 Mambo tunayosikia kuwa unafundisha ni mageni kwetu nasi tungependa kuelewa maana yake.” 21 Waathene na hata wageni walikuwa na tabia ya kutumia wakati wao wote katika mazungumzo ya mambo yo yote ambayo yanaonekana kuwa mageni au mapya.

Hotuba Ya Paulo Kwenye Areopago

22 Kwa hiyo Paulo alisimama kati kati ya Areopago akasema, “Ndugu wa Athene! Nimeona katika kila jambo kuwa ninyi ni watu wa dini hasa. 23 Kwa kuwa nilipokuwa nikitembea mjini niliona sehemu nyingi za kuabudia. Niliona pia madhabahu moja iliyoan dikwa, ‘Kwa Mungu asiyejulikana.’ Huyo Mungu mnayemwabudu bila kumfahamu, ndiye ninayemtangaza kwenu. 24 Mungu aliyeumba dunia na vitu vyote vilivyomo, ambaye pia ni Bwana wa mbingu na nchi, haishi katika mahekalu yaliyojengwa na wanadamu. 25 Wala hahu dumiwi kwa mikono ya wanadamu kana kwamba anahitaji cho chote; kwa sababu yeye ndiye anayewapa watu wote uhai na pumzi na kila kitu. 26 Yeye aliumba mataifa yote ya wanadamu waishi juu ya nchi kutokana na mtu mmoja. Pia amepanga muda wa maisha ya watu wote, akaweka na mipaka ya mahali watakapoishi 27 ili wamtafute Mungu na wamfahamu. Lakini Yeye hayuko mbali nasi kwa maana 28 ‘Tunaishi na kuenenda na kuwa na uhai ndani yake,’ na kama mtunga mashairi wenu alivyosema, ‘Sisi ni uzao wa Mungu.’ 29 Kwa kuwa sisi ni wa uzao wa Mungu hatupaswi kudhani kuwa yeye ni kama sanamu ya dhahabu au fedha au jiwe iliyotengenezwa kwa akili na ufundi wa mwanadamu. 30 Mungu alisamehe ujinga huo wa zamani, lakini sasa anaamuru watu wote watubu, waachane na miungu ya sanamu. 31 Kwa kuwa amepanga siku ambayo atahukumu ulimwengu kwa haki akimtumia mtu aliyemchagua, ambaye amemhakikisha kwa watu wote kwa kumfufua kutoka kwa wafu.” 32 Waathene waliposikia juu ya ufufuo wa wafu, baadhi yao wakamdhihaki; lakini wengine wal isema, “Tutataka kusikia tena juu ya habari hii.” 33 Kwa hiyo Paulo akaondoka. 34 Lakini baadhi ya watu walimfuata Paulo wakaamini. Kati yao alikuwepo Dionisio, Mwareopago, na mwanamke mmoja aliyeitwa Damari na wengine.

In Thessalonica

17 When Paul and his companions had passed through Amphipolis and Apollonia, they came to Thessalonica,(A) where there was a Jewish synagogue. As was his custom, Paul went into the synagogue,(B) and on three Sabbath(C) days he reasoned with them from the Scriptures,(D) explaining and proving that the Messiah had to suffer(E) and rise from the dead.(F) “This Jesus I am proclaiming to you is the Messiah,”(G) he said. Some of the Jews were persuaded and joined Paul and Silas,(H) as did a large number of God-fearing Greeks and quite a few prominent women.

But other Jews were jealous; so they rounded up some bad characters from the marketplace, formed a mob and started a riot in the city.(I) They rushed to Jason’s(J) house in search of Paul and Silas in order to bring them out to the crowd.[a] But when they did not find them, they dragged(K) Jason and some other believers(L) before the city officials, shouting: “These men who have caused trouble all over the world(M) have now come here,(N) and Jason has welcomed them into his house. They are all defying Caesar’s decrees, saying that there is another king, one called Jesus.”(O) When they heard this, the crowd and the city officials were thrown into turmoil. Then they made Jason(P) and the others post bond and let them go.

In Berea

10 As soon as it was night, the believers sent Paul and Silas(Q) away to Berea.(R) On arriving there, they went to the Jewish synagogue.(S) 11 Now the Berean Jews were of more noble character than those in Thessalonica,(T) for they received the message with great eagerness and examined the Scriptures(U) every day to see if what Paul said was true.(V) 12 As a result, many of them believed, as did also a number of prominent Greek women and many Greek men.(W)

13 But when the Jews in Thessalonica learned that Paul was preaching the word of God at Berea,(X) some of them went there too, agitating the crowds and stirring them up. 14 The believers(Y) immediately sent Paul to the coast, but Silas(Z) and Timothy(AA) stayed at Berea. 15 Those who escorted Paul brought him to Athens(AB) and then left with instructions for Silas and Timothy to join him as soon as possible.(AC)

In Athens

16 While Paul was waiting for them in Athens, he was greatly distressed to see that the city was full of idols. 17 So he reasoned in the synagogue(AD) with both Jews and God-fearing Greeks, as well as in the marketplace day by day with those who happened to be there. 18 A group of Epicurean and Stoic philosophers began to debate with him. Some of them asked, “What is this babbler trying to say?” Others remarked, “He seems to be advocating foreign gods.” They said this because Paul was preaching the good news(AE) about Jesus and the resurrection.(AF) 19 Then they took him and brought him to a meeting of the Areopagus,(AG) where they said to him, “May we know what this new teaching(AH) is that you are presenting? 20 You are bringing some strange ideas to our ears, and we would like to know what they mean.” 21 (All the Athenians(AI) and the foreigners who lived there spent their time doing nothing but talking about and listening to the latest ideas.)

22 Paul then stood up in the meeting of the Areopagus(AJ) and said: “People of Athens! I see that in every way you are very religious.(AK) 23 For as I walked around and looked carefully at your objects of worship, I even found an altar with this inscription: to an unknown god. So you are ignorant of the very thing you worship(AL)—and this is what I am going to proclaim to you.

24 “The God who made the world and everything in it(AM) is the Lord of heaven and earth(AN) and does not live in temples built by human hands.(AO) 25 And he is not served by human hands, as if he needed anything. Rather, he himself gives everyone life and breath and everything else.(AP) 26 From one man he made all the nations, that they should inhabit the whole earth; and he marked out their appointed times in history and the boundaries of their lands.(AQ) 27 God did this so that they would seek him and perhaps reach out for him and find him, though he is not far from any one of us.(AR) 28 ‘For in him we live and move and have our being.’[b](AS) As some of your own poets have said, ‘We are his offspring.’[c]

29 “Therefore since we are God’s offspring, we should not think that the divine being is like gold or silver or stone—an image made by human design and skill.(AT) 30 In the past God overlooked(AU) such ignorance,(AV) but now he commands all people everywhere to repent.(AW) 31 For he has set a day when he will judge(AX) the world with justice(AY) by the man he has appointed.(AZ) He has given proof of this to everyone by raising him from the dead.”(BA)

32 When they heard about the resurrection of the dead,(BB) some of them sneered, but others said, “We want to hear you again on this subject.” 33 At that, Paul left the Council. 34 Some of the people became followers of Paul and believed. Among them was Dionysius, a member of the Areopagus,(BC) also a woman named Damaris, and a number of others.

Footnotes

  1. Acts 17:5 Or the assembly of the people
  2. Acts 17:28 From the Cretan philosopher Epimenides
  3. Acts 17:28 From the Cilician Stoic philosopher Aratus