Matayo 28:1-7
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Afufuka
28 Baada ya Sabato, alfajiri mapema siku ile ya Jumapili, Mari amu Magdalena na yule Mariamu mwingine walikwenda kuliangalia kaburi. 2 Ghafla pakatokea tetemeko kubwa la ardhi; kwa sababu Malaika wa Bwana alikuja kutoka mbinguni akalisogeza lile jiwe, akalikalia. 3 Malaika huyo alifanana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji. 4 Wale walinzi wa kaburi walipomwona walitetemeka kwa hofu, wakawa kama wamekufa.
5 Lakini yule malaika akawaambia wale wanawake, “Msiogope. Ninajua kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa. 6 Hayupo hapa. Amefu fuka kama alivyosema. Njooni muone pale alipokuwa amelazwa. 7 Kisha nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake hivi, amefufuka kutoka kwa wafu naye amewatangulia kwenda Galilaya, mtamwona huko. Sasa nimekwisha waambia.”
Read full chapter
Matayo 28:1-7
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Afufuka
28 Baada ya Sabato, alfajiri mapema siku ile ya Jumapili, Mari amu Magdalena na yule Mariamu mwingine walikwenda kuliangalia kaburi. 2 Ghafla pakatokea tetemeko kubwa la ardhi; kwa sababu Malaika wa Bwana alikuja kutoka mbinguni akalisogeza lile jiwe, akalikalia. 3 Malaika huyo alifanana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji. 4 Wale walinzi wa kaburi walipomwona walitetemeka kwa hofu, wakawa kama wamekufa.
5 Lakini yule malaika akawaambia wale wanawake, “Msiogope. Ninajua kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa. 6 Hayupo hapa. Amefu fuka kama alivyosema. Njooni muone pale alipokuwa amelazwa. 7 Kisha nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake hivi, amefufuka kutoka kwa wafu naye amewatangulia kwenda Galilaya, mtamwona huko. Sasa nimekwisha waambia.”
Read full chapterCopyright © 1989 by Biblica