Matayo 27:46-50
Neno: Bibilia Takatifu
46 Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kuu, “Eli, Eli lama sabakthani?” Yaani, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona ume niacha?”
47 Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama hapo waliposikia haya walisema, “Anamwita Eliya!” 48 Mmoja wao akaenda mbio akaleta sponji akaichovya kwenye siki akaiinua kwa mwanzi akamwekea mdo moni. 49 Lakini wengine wakasema, “Hebu tuone kama Eliya ata kuja kumwokoa.” [Na mwingine akachukua mkuki akamchoma ubavuni, pakatoka maji na damu].
50 Yesu akalia tena kwa sauti kuu, kisha akakata roho.
Read full chapter
Mathayo 27:46-50
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
46 Yapata saa tisa alasiri Yesu alilia kwa sauti kuu akisema, “Eloi, Eloi, lema sabakthani?” yaani “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha peke yangu?”(A)
47 Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hili wakasema, “Anamwita Eliya.”[a]
48 Mtu mmoja alikimbia haraka akaenda kuchukua sponji, akaijaza siki, akaifunga kwenye fimbo na akanyoosha fimbo ili kumpa Yesu sponji ili anywe siki. 49 Lakini wengine walisema, “Usimjali. Tunataka tuone ikiwa Eliya atakuja kumsaidia.”
50 Yesu akalia kwa sauti kuu tena, kisha akafa.[b]
Read full chapterCopyright © 1989 by Biblica
Copyright © 2017 by Bible League International