Mpango Wa Kumwua Yesu

26 Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake, “Mnafahamu kwamba sikukuu ya Pasaka inaanza baada ya siku mbili na mimi Mwana wa Adamu nitasalitiwa na kusulubiwa.”

Wakati huo makuhani wakuu na wazee walifanya mkutano katika ukumbi wa kuhani mkuu, jina lake, Kayafa. Wakashauriana jinsi ya kumkamata Yesu na kumwua kwa siri. Wakasema, “Lakini tusi fanye haya wakati wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia.”

Yesu Anapakwa Mafuta Bethania

Yesu alipokuwa Bethania nyumbani kwa Simoni mkoma, mwa namke mmoja alimjia akiwa na chupa ya alabasta yenye manukato ya thamani kubwa; akammiminia Yesu manukato hayo kichwani akiwa ame kaa mezani. Lakini wanafunzi wake walipoona hayo waliudhika, wakasema, “Kwa nini kupoteza manukato bure? Haya yangaliuzwa kwa bei kubwa na fedha hizo wakapewa maskini.”

10 Yesu alifahamu mawazo yao kwa hiyo akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mama? Amenifanyia jambo zuri sana. 11 Maskini mnao siku zote lakini hamtakuwa nami siku zote. 12 Aliponimimi nia haya manukato alikuwa akiandaa mwili wangu kwa mazishi. 13 Ninawaambia kweli, mahali po pote Habari Njema itakapohubi riwa ulimwenguni, jambo hili alilofanya litatajwa, kwa ukumbusho wake.”

Yuda Akubali Kumsaliti Yesu

14 Kisha mmojawapo wa wale wanafunzi kumi na wawili aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda kwa kuhani mkuu akamwambia, “Mtanilipa kiasi gani nikimtoa kwenu?” 15 Wakamlipa vipande thelathini vya fedha. 16 Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti Yesu.

Matayarisho Ya Pasaka

17 Siku ya kwanza ya sikukuu ya Mikate isiotiwa chachu wale wanafunzi walikuja kwa Yesu wakamwuliza, “Ungependa tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?”

18 Akajibu, “Nendeni kwa mtu fulani huko mjini mkamwambie, ‘Bwana anasema hivi: saa yangu imekaribia, napenda kula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu nyumbani kwako.’ ” 19 Wanafunzi waka fanya kama Yesu alivyowaambia, wakaandaa Pasaka.

20 Ilipofika jioni, Yesu aliketi mezani pamoja na wanafunzi wake. 21 Walipokuwa wakila akawaambia, “Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti.” 22 Wakasikitika sana, wakaanza kumwul iza mmoja mmoja, “Ni mimi, Bwana?” 23 Yesu akawaambia, “Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami, ndiye ata kayenisaliti. 24 Mimi Mwana wa Adamu sina budi kufa kama ilivy oandikwa katika Maandiko, lakini ole wake mtu yule atakayenisal iti. Ingalikuwa nafuu kwake kama hakuzaliwa!”

25 Kisha Yuda, yule ambaye alimsaliti akasema, “Ni mimi, Bwana?” Yesu akamjibu, “Umetamka mwenyewe.”

Bwana?” Yesu akamjibu, “Umetamka mwenyewe.”

26 Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, “Chukueni mle; huu ni mwili wangu.” 27 Kisha akachukua kikombe, akashukuru, akawapa akisema, “Kunyweni nyote katika kikombe hiki. 28 Hii ni damu yangu ya agano ambayo inamwagika kwa ajili ya wengi ili wasame hewe dhambi. 29 Ninawahakikishia kuwa sitakunywa tena maji ya mzabibu mpaka siku nitakapoyanywa pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”

Baba yangu.”

30 Walipokwisha kuimba wimbo walikwenda kwenye mlima wa Mizeituni.

Yesu Amwambia Petro Atamkana

31 Kisha Yesu akawaambia, “Usiku wa leo kila mmoja wenu atanikimbia kwa maana Maandiko yanasema, ‘Nitampiga mchungaji, na kondoo wote wa kundi lake watatawanyika.’ 32 Lakini baada ya kufufuka, nitawatangulia kwenda Galilaya.”

33 Petro akasema, “Hata kama wote watakuacha, mimi sitaku acha.”

34 Yesu akamjibu, “Ninakuambia kweli, usiku huu huu, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” 35 Lakini Petro akasema, “Hata kama itabidi nife pamoja na wewe, sitakukana.” Na wana funzi wote wakasema hivyo hivyo.

Gethsemane

36 Kisha Yesu akaenda nao mpaka kwenye bustani iitwayo Gethsemane. Akawaambia, “Kaeni hapa, mimi ninakwenda mbele zaidi kuomba.” 37 Akamchukua Petro, pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kufadhaika na kuhuzunika. 38 Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu umejaa majonzi karibu ya kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.”

39 Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi akaomba, “Baba yangu, kama inawezekana, niondolee kikombe hiki cha mateso, lakini si kama nipendavyo bali kama upendavyo wewe.”

40 Akarudi kwa wanafunzi wake, akawakuta wamelala. Akamwul iza Petro, “Hamkuweza kukesha nami hata kwa saa moja? 41 Kesheni muombe, msije mkaingia katika majaribu. Kwa maana roho i radhi lakini mwili ni dhaifu.” 42 Akaenda tena mara ya pili, akaomba, “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kion dolewe pasipo mimi kukinywea, mapenzi yako yafanyike.” 43 Ali porudi tena aliwakuta wamelala kwa maana macho yao yalikuwa mazito. 44 Kwa hiyo akawaacha akaenda tena mara ya tatu, akaomba vile vile.

45 Kisha akarudi kwa wale wanafunzi akawaambia, “Bado mme lala na kupumzika? Angalieni, saa imefika ambapo mimi Mwana wa Adamu sina budi kukabidhiwa mikononi mwa wenye dhambi. 46 Amkeni, twendeni! Yule anayenisaliti atafika sasa hivi!”

Yesu Akamatwa

47 Alipokuwa anazungumza, Yuda, mmojawapo wa wale kumi na wawili, akafika,akifuatana na umati wa watu wenye mapanga na mar ungu. Walikuwa wametumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.

48 Yuda alikuwa amepatana na hao watu kuwa, ‘Nitakayembusu ndiye, mkamateni.’ 49 Basi alipofika, alimwendea Yesu moja kwa moja, akamsalimia, “Salaam, Rabi!” Akambusu. 50 Yesu akamjibu, “Rafiki, umekuja kufanya nini hapa?” Basi wale watu wakasogea, wakamkamata Yesu. 51 Ndipo mmojawapo wa wafuasi wa Yesu ali poona hivyo, akachukua panga lake, akampiga nalo mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio. 52 Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote watumiao upanga watakufa kwa upanga. 53 Unadhani siwezi kumwomba Baba yangu aniletee mara moja majeshi kumi na mbili ya malaika? 54 Lakini nikifanya hivyo yatatimiaje Maandiko yale yasemayo kwamba mambo haya lazima yato kee?”

55 Wakati huo Yesu akawaambia ule umati, “Mmekuja kunika mata kama mnyang’anyi kwa mapanga na marungu? Mbona siku zote nilikaa Hekaluni na kufundisha lakini hamkunikamata? 56 Lakini haya yametokea ili Maandiko ya manabii yatiimie.” Ndipo wana funzi wake wote wakamwacha, wakakimbia.

Yesu Ashtakiwa Mbele Ya Baraza

57 Wale waliomkamata Yesu wakampeleka nyumbani kwa Kayafa, kuhani mkuu, ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee walikuwa wamekutanika.

58 Lakini Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa kuhani mkuu akaingia ndani pamoja na walinzi aone litakalotokea. 59 Basi makuhani wakuu na baraza zima wakatafuta ushahidi wa uongo ili wamwue Yesu, 60 lakini hawakupata, ingawa mashahidi wengi wa uongo walijitokeza. Hatimaye wakajitokeza watu wawili, 61 wakasema: “Huyu mtu alisema, ‘Nina uwezo wa kuvunja Hekalu la Mungu na kulijenga tena katika muda wa siku tatu .’ ”

62 Kisha kuhani mkuu akasimama, akamwambia Yesu, “Huna jibu? Husikii huo ushahidi waliotoa watu hao?” 63 Lakini Yesu hakusema neno. Basi kuhani mkuu akamwambia, “Nakuapisha kwa jina la Mungu aliye hai, tuambie kama wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu.”

Mungu.”

64 Yesu akajibu, “Umetamka mwenyewe. Lakini nina waambieni nyote kwamba baada ya hapa, mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kulia wa Mungu mwenye uweza na akija juu ya mawingu ya mbin guni.”

65 Aliposikia maneno hayo, kuhani mkuu alirarua mavazi yake akasema, “Amekufuru! Tunahitaji ushahidi gani zaidi? Si mmemsi kia akikufuru? 66 Mnaamuaje?” Wakajibu, “Anastahili kufa!”

67 Kisha wakamtemea mate usoni; wengine wakampiga ngumi na makofi, 68 wakasema, “Hebu toa unabii wewe Kristo! Ni nani ame kupiga?”

69 Wakati huo Petro alikuwa amekaa uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.” 70 Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui usemalo.”

71 Kisha alipotoka nje, mlangoni mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwapo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.” 72 Akakana tena kwa kiapo akisema, “Simfa hamu mtu huyo!” 73 Baada ya muda mfupi wale waliokuwa wamesi mama pale walimwendea Petro wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao kwa maana namna yako ya kusema ni kama yao.” 74 Ndipo Petro akalaani na kuapa, akawaambia, “Simfahamu mtu huyo!” Wakati huo huo jogoo akawika. 75 Na Petro akakumbuka Yesu alivyomwambia, “Kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu.” Akaenda nje, akalia kwa uchungu.

The Plot Against Jesus(A)

26 When Jesus had finished saying all these things,(B) he said to his disciples, “As you know, the Passover(C) is two days away—and the Son of Man will be handed over to be crucified.”

Then the chief priests and the elders of the people assembled(D) in the palace of the high priest, whose name was Caiaphas,(E) and they schemed to arrest Jesus secretly and kill him.(F) “But not during the festival,” they said, “or there may be a riot(G) among the people.”

Jesus Anointed at Bethany(H)(I)

While Jesus was in Bethany(J) in the home of Simon the Leper, a woman came to him with an alabaster jar of very expensive perfume, which she poured on his head as he was reclining at the table.

When the disciples saw this, they were indignant. “Why this waste?” they asked. “This perfume could have been sold at a high price and the money given to the poor.”

10 Aware of this, Jesus said to them, “Why are you bothering this woman? She has done a beautiful thing to me. 11 The poor you will always have with you,[a](K) but you will not always have me. 12 When she poured this perfume on my body, she did it to prepare me for burial.(L) 13 Truly I tell you, wherever this gospel is preached throughout the world, what she has done will also be told, in memory of her.”

Judas Agrees to Betray Jesus(M)

14 Then one of the Twelve—the one called Judas Iscariot(N)—went to the chief priests 15 and asked, “What are you willing to give me if I deliver him over to you?” So they counted out for him thirty pieces of silver.(O) 16 From then on Judas watched for an opportunity to hand him over.

The Last Supper(P)(Q)(R)

17 On the first day of the Festival of Unleavened Bread,(S) the disciples came to Jesus and asked, “Where do you want us to make preparations for you to eat the Passover?”(T)

18 He replied, “Go into the city to a certain man and tell him, ‘The Teacher says: My appointed time(U) is near. I am going to celebrate the Passover with my disciples at your house.’” 19 So the disciples did as Jesus had directed them and prepared the Passover.

20 When evening came, Jesus was reclining at the table with the Twelve. 21 And while they were eating, he said, “Truly I tell you, one of you will betray me.”(V)

22 They were very sad and began to say to him one after the other, “Surely you don’t mean me, Lord?”

23 Jesus replied, “The one who has dipped his hand into the bowl with me will betray me.(W) 24 The Son of Man will go just as it is written about him.(X) But woe to that man who betrays the Son of Man! It would be better for him if he had not been born.”

25 Then Judas, the one who would betray him,(Y) said, “Surely you don’t mean me, Rabbi?”(Z)

Jesus answered, “You have said so.”

26 While they were eating, Jesus took bread, and when he had given thanks, he broke it(AA) and gave it to his disciples, saying, “Take and eat; this is my body.”

27 Then he took a cup,(AB) and when he had given thanks, he gave it to them, saying, “Drink from it, all of you. 28 This is my blood of the[b] covenant,(AC) which is poured out for many for the forgiveness of sins.(AD) 29 I tell you, I will not drink from this fruit of the vine from now on until that day when I drink it new with you(AE) in my Father’s kingdom.”

30 When they had sung a hymn, they went out to the Mount of Olives.(AF)

Jesus Predicts Peter’s Denial(AG)

31 Then Jesus told them, “This very night you will all fall away on account of me,(AH) for it is written:

“‘I will strike the shepherd,
    and the sheep of the flock will be scattered.’[c](AI)

32 But after I have risen, I will go ahead of you into Galilee.”(AJ)

33 Peter replied, “Even if all fall away on account of you, I never will.”

34 “Truly I tell you,” Jesus answered, “this very night, before the rooster crows, you will disown me three times.”(AK)

35 But Peter declared, “Even if I have to die with you,(AL) I will never disown you.” And all the other disciples said the same.

Gethsemane(AM)

36 Then Jesus went with his disciples to a place called Gethsemane, and he said to them, “Sit here while I go over there and pray.” 37 He took Peter and the two sons of Zebedee(AN) along with him, and he began to be sorrowful and troubled. 38 Then he said to them, “My soul is overwhelmed with sorrow(AO) to the point of death. Stay here and keep watch with me.”(AP)

39 Going a little farther, he fell with his face to the ground and prayed, “My Father, if it is possible, may this cup(AQ) be taken from me. Yet not as I will, but as you will.”(AR)

40 Then he returned to his disciples and found them sleeping. “Couldn’t you men keep watch with me(AS) for one hour?” he asked Peter. 41 “Watch and pray so that you will not fall into temptation.(AT) The spirit is willing, but the flesh is weak.”

42 He went away a second time and prayed, “My Father, if it is not possible for this cup to be taken away unless I drink it, may your will be done.”(AU)

43 When he came back, he again found them sleeping, because their eyes were heavy. 44 So he left them and went away once more and prayed the third time, saying the same thing.

45 Then he returned to the disciples and said to them, “Are you still sleeping and resting? Look, the hour(AV) has come, and the Son of Man is delivered into the hands of sinners. 46 Rise! Let us go! Here comes my betrayer!”

Jesus Arrested(AW)

47 While he was still speaking, Judas,(AX) one of the Twelve, arrived. With him was a large crowd armed with swords and clubs, sent from the chief priests and the elders of the people. 48 Now the betrayer had arranged a signal with them: “The one I kiss is the man; arrest him.” 49 Going at once to Jesus, Judas said, “Greetings, Rabbi!”(AY) and kissed him.

50 Jesus replied, “Do what you came for, friend.”[d](AZ)

Then the men stepped forward, seized Jesus and arrested him. 51 With that, one of Jesus’ companions reached for his sword,(BA) drew it out and struck the servant of the high priest, cutting off his ear.(BB)

52 “Put your sword back in its place,” Jesus said to him, “for all who draw the sword will die by the sword.(BC) 53 Do you think I cannot call on my Father, and he will at once put at my disposal more than twelve legions of angels?(BD) 54 But how then would the Scriptures be fulfilled(BE) that say it must happen in this way?”

55 In that hour Jesus said to the crowd, “Am I leading a rebellion, that you have come out with swords and clubs to capture me? Every day I sat in the temple courts teaching,(BF) and you did not arrest me. 56 But this has all taken place that the writings of the prophets might be fulfilled.”(BG) Then all the disciples deserted him and fled.

Jesus Before the Sanhedrin(BH)

57 Those who had arrested Jesus took him to Caiaphas(BI) the high priest, where the teachers of the law and the elders had assembled. 58 But Peter followed him at a distance, right up to the courtyard of the high priest.(BJ) He entered and sat down with the guards(BK) to see the outcome.

59 The chief priests and the whole Sanhedrin(BL) were looking for false evidence against Jesus so that they could put him to death. 60 But they did not find any, though many false witnesses(BM) came forward.

Finally two(BN) came forward 61 and declared, “This fellow said, ‘I am able to destroy the temple of God and rebuild it in three days.’”(BO)

62 Then the high priest stood up and said to Jesus, “Are you not going to answer? What is this testimony that these men are bringing against you?” 63 But Jesus remained silent.(BP)

The high priest said to him, “I charge you under oath(BQ) by the living God:(BR) Tell us if you are the Messiah,(BS) the Son of God.”(BT)

64 “You have said so,”(BU) Jesus replied. “But I say to all of you: From now on you will see the Son of Man sitting at the right hand of the Mighty One(BV) and coming on the clouds of heaven.”[e](BW)

65 Then the high priest tore his clothes(BX) and said, “He has spoken blasphemy! Why do we need any more witnesses? Look, now you have heard the blasphemy. 66 What do you think?”

“He is worthy of death,”(BY) they answered.

67 Then they spit in his face and struck him with their fists.(BZ) Others slapped him 68 and said, “Prophesy to us, Messiah. Who hit you?”(CA)

Peter Disowns Jesus(CB)

69 Now Peter was sitting out in the courtyard, and a servant girl came to him. “You also were with Jesus of Galilee,” she said.

70 But he denied it before them all. “I don’t know what you’re talking about,” he said.

71 Then he went out to the gateway, where another servant girl saw him and said to the people there, “This fellow was with Jesus of Nazareth.”

72 He denied it again, with an oath: “I don’t know the man!”

73 After a little while, those standing there went up to Peter and said, “Surely you are one of them; your accent gives you away.”

74 Then he began to call down curses, and he swore to them, “I don’t know the man!”

Immediately a rooster crowed. 75 Then Peter remembered the word Jesus had spoken: “Before the rooster crows, you will disown me three times.”(CC) And he went outside and wept bitterly.

Footnotes

  1. Matthew 26:11 See Deut. 15:11.
  2. Matthew 26:28 Some manuscripts the new
  3. Matthew 26:31 Zech. 13:7
  4. Matthew 26:50 Or “Why have you come, friend?”
  5. Matthew 26:64 See Psalm 110:1; Daniel 7:13.