Yesu Afundisha Kuhusu Talaka

19 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, aliondoka Galilaya akaenda sehemu za Yudea, ng’ambo ya mto Yordani. Umati mkubwa wa watu walimfuata, naye akawaponya huko.

Baadhi ya Mafarisayo wakamjia wakamtega kwa kumwuliza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake kwa sababu yo yote ile?”

Akawajibu, “Hamjasoma kwamba aliyewaumba tangu mwanzo ali waumba mume na mke akawaambia, ‘Kwa sababu hii mtu atamwacha baba yake na mama yake na aambatane na mkewe; na hao wawili wata kuwa mwili mmoja’? Kwa hiyo hawawi wawili tena, bali ni mwili mmoja. Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitengan ishe.”

Wakamwuliza, “Kwa nini basi Musa aliagiza kwamba mtu anaweza kumpa mkewe hati ya talaka na kumwacha?” Yesu akawa jibu, “Musa aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu mioyo yenu ni migumu. Lakini tangu mwanzo haikukusudiwa iwe hivyo. Nami nawaambieni, mtu ye yote anayemwacha mkewe, isipokuwa kwa sababu ya uasherati, akaoa mke mwingine, anazini.” [“Na mtu anayemwoa mwanamke aliyepewa talaka pia anazini.”]

10 Wanafunzi wake wakamwambia, “Kama hivi ndivyo hali ilivyo kati ya mume na mke, basi ni afadhali mtu asioe!” 11 Yesu akajibu, “Si kila mtu anaweza kupokea mafundisho haya isipokuwa wale ambao Mungu amewajalia. 12 Kwa maana wako watu wasioweza kuoa kwa sababu wamezaliwa na hali hiyo; na wengine wamefanywa hali hiyo na binadamu; na pia wako wengine ambao wameamua kutokuoa kwa ajili ya Ufalme wa mbinguni. Awezaye kuli pokea fundisho hili na alipokee.”

Yesu Awabariki Watoto Wadogo

13 Kisha watoto wadogo wakaletwa kwa Yesu ili aweke mikono yake juu yao na awaombee. Lakini wanafunzi wake wakawakemea wali owaleta. 14 Yesu akawaambia, “Waacheni watoto waje kwangu, msiwazuie; kwa maana Ufalme wa mbinguni ni wa walio kama hawa. 15 Alipokwisha wawekea mikono akaondoka.

Mtu Tajiri

16 Mtu mmoja alikuja kwa Yesu akamwuliza, “Mwalimu, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?”

17 Yesu akamjibu, “Mbona unaniuliza kuhusu jambo jema? Kuna mmoja tu aliye mwema . Lakini kama unataka kuingia uzimani, tii amri.”

18 Yule mtu akamwuliza, “Amri zipi?” Yesu akamjibu, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, 19 waheshimu baba yako na mama yako na umpende jirani yako kama nafsi yako.”

20 Yule kijana akasema, “Zote hizi nimezitii. Ninapungukiwa na nini zaidi?”

21 Yesu akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda kauze vitu vyote ulivyo navyo na fedha utakazopata uwape maskini, nawe utakuwa umejiwekea hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.” 22 Yule kijana aliposikia hayo aliondoka kwa masikitiko, kwa sababu alikuwa tajiri sana.

Hatari Za Utajiri

23 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi, “Nawaambieni kweli, itakuwa vigumu kwa mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni. 24 Tena nawaambieni, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa mbinguni.” 25 Wanafunzi wake waliposikia haya walishangaa sana, wakamwuliza, “Ni nani basi anaweza kuokoka?” 26 Lakini Yesu akawatazama akawaambia, “Kwa binadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu kila kitu kinawezekana.” 27 Ndipo Petro aka mwambia, “Na sisi tulioacha kila kitu tukakufuata tutapata nini?”

28 Yesu akawajibu, “Ninawahakikishia kwamba, katika dunia mpya, wakati mimi Mwana wa Adamu nitakapoketi kwenye kiti changu cha utukufu cha enzi, ninyi mlionifuata pia mtaketi katika viti vya enzi kumi na viwili, mkiyahukumu yale makabila kumi na mawili ya Israeli. 29 Na kila mtu aliyeacha nyumba au ndugu zake au dada zake au baba au mama au watoto wake au mashamba kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia zaidi ya hayo, na atarithi uzima wa milele. 30 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”

Divorce(A)

19 When Jesus had finished saying these things,(B) he left Galilee and went into the region of Judea to the other side of the Jordan. Large crowds followed him, and he healed them(C) there.

Some Pharisees came to him to test him. They asked, “Is it lawful for a man to divorce his wife(D) for any and every reason?”

“Haven’t you read,” he replied, “that at the beginning the Creator ‘made them male and female,’[a](E) and said, ‘For this reason a man will leave his father and mother and be united to his wife, and the two will become one flesh’[b]?(F) So they are no longer two, but one flesh. Therefore what God has joined together, let no one separate.”

“Why then,” they asked, “did Moses command that a man give his wife a certificate of divorce and send her away?”(G)

Jesus replied, “Moses permitted you to divorce your wives because your hearts were hard. But it was not this way from the beginning. I tell you that anyone who divorces his wife, except for sexual immorality, and marries another woman commits adultery.”(H)

10 The disciples said to him, “If this is the situation between a husband and wife, it is better not to marry.”

11 Jesus replied, “Not everyone can accept this word, but only those to whom it has been given.(I) 12 For there are eunuchs who were born that way, and there are eunuchs who have been made eunuchs by others—and there are those who choose to live like eunuchs for the sake of the kingdom of heaven. The one who can accept this should accept it.”

The Little Children and Jesus(J)

13 Then people brought little children to Jesus for him to place his hands on them(K) and pray for them. But the disciples rebuked them.

14 Jesus said, “Let the little children come to me, and do not hinder them, for the kingdom of heaven belongs(L) to such as these.”(M) 15 When he had placed his hands on them, he went on from there.

The Rich and the Kingdom of God(N)

16 Just then a man came up to Jesus and asked, “Teacher, what good thing must I do to get eternal life(O)?”(P)

17 “Why do you ask me about what is good?” Jesus replied. “There is only One who is good. If you want to enter life, keep the commandments.”(Q)

18 “Which ones?” he inquired.

Jesus replied, “‘You shall not murder, you shall not commit adultery,(R) you shall not steal, you shall not give false testimony, 19 honor your father and mother,’[c](S) and ‘love your neighbor as yourself.’[d](T)

20 “All these I have kept,” the young man said. “What do I still lack?”

21 Jesus answered, “If you want to be perfect,(U) go, sell your possessions and give to the poor,(V) and you will have treasure in heaven.(W) Then come, follow me.”

22 When the young man heard this, he went away sad, because he had great wealth.

23 Then Jesus said to his disciples, “Truly I tell you, it is hard for someone who is rich(X) to enter the kingdom of heaven. 24 Again I tell you, it is easier for a camel to go through the eye of a needle than for someone who is rich to enter the kingdom of God.”

25 When the disciples heard this, they were greatly astonished and asked, “Who then can be saved?”

26 Jesus looked at them and said, “With man this is impossible, but with God all things are possible.”(Y)

27 Peter answered him, “We have left everything to follow you!(Z) What then will there be for us?”

28 Jesus said to them, “Truly I tell you, at the renewal of all things, when the Son of Man sits on his glorious throne,(AA) you who have followed me will also sit on twelve thrones, judging the twelve tribes of Israel.(AB) 29 And everyone who has left houses or brothers or sisters or father or mother or wife[e] or children or fields for my sake will receive a hundred times as much and will inherit eternal life.(AC) 30 But many who are first will be last, and many who are last will be first.(AD)

Notas al pie

  1. Matthew 19:4 Gen. 1:27
  2. Matthew 19:5 Gen. 2:24
  3. Matthew 19:19 Exodus 20:12-16; Deut. 5:16-20
  4. Matthew 19:19 Lev. 19:18
  5. Matthew 19:29 Some manuscripts do not have or wife.