Add parallel Print Page Options

Yesu Amponya Mtu Siku ya Sabato

(Mt 12:9-14; Lk 6:6-11)

Kwa mara nyingine tena Yesu alikwenda kwenye sinagogi. Huko alikuwepo mtu aliyekuwa na mkono uliolemaa. Watu wengine walikuwa wakimwangalia Yesu kwa karibu sana. Walitaka kuona ikiwa angemponya mtu yule siku ya Sabato,[a] ili wapate sababu ya kumshitaki. Yesu akamwambia yule mtu aliyekuwa na mkono uliolemaa, “Simama mbele ili kila mtu akuone.”

Ndipo Yesu akawaambia, “Je, ni halali kutenda mema ama kutenda mabaya siku ya Sabato? Je, ni halali kuyaokoa maisha ya mtu fulani ama kuyapoteza?” Lakini wao walikaa kimya.

Yesu akawatazama wote waliomzunguka kwa hasira lakini alihuzunika kwa sababu waliifanya mioyo yao kuwa migumu. Akamwambia mtu yule “nyosha mkono wako”, naye akaunyosha, na mkono wake ukapona. Kisha Mafarisayo wakaondoka na papo hapo wakaanza kupanga njama pamoja na Maherode kinyume cha Yesu kutafuta jinsi gani wanaweza kumuua.

Wengi Wamfuata Yesu

Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake hadi Ziwa Galilaya, na kundi kubwa la watu kutoka Galilaya likawafuata, pamoja na watu kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumea, na katika maeneo yote ng'ambo ya Mto Yordani na yale yanayozunguka Tiro na Sidoni. Lilikuwa kundi kubwa sana la watu. Wote walimjia Yesu kwa sababu walikuwa wamesikia mambo aliyokuwa anafanya.

Kwa sababu ya kundi, aliwaambia wanafunzi wake, kumtayarishia mashua mdogo, ili kwamba wasiweze kumsonga na kumbana. 10 Yesu alikuwa ameponya watu wengi. Hivyo wote wale waliokuwa na magonjwa waliendelea kujisogeza mbele kumwelekea ili wamguse. 11 Kila mara pepo wachafu walipomwona Yesu, walianguka chini mbele yake, na kulia kwa sauti, “Wewe ni Mwana wa Mungu!” 12 Lakini yeye aliwaamuru kila mara wasimwambie mtu yeyote yeye ni nani.

Yesu Achagua Wanafunzi Wake Kumi na Wawili

(Mt 10:1-4; Lk 6:12-16)

13 Kisha Yesu akapanda juu kwenye vilima na akawaita baadhi ya wanafunzi wake, hasa wale aliowataka wajiunge naye pale. 14 Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume. Aliwachagua ili waambatane pamoja naye, na kwamba aweze kuwatuma sehemu mbalimbali kuhubiri ujumbe wa neno la Mungu. 15 Pia aliwapa mamlaka ya kufukuza mashetani toka kwa watu. 16 Yafuatayo ni majina ya mitume kumi na wawili aliowateuwa Yesu:

Simoni ambaye Yesu alimwita Petro,

17 Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana ndugu yake (ambao wote Yesu aliwaita Boanergesi), yaani “wana wa ngurumo yenye radi”,

18 Andrea,

Filipo,

Bartholomayo,

Mathayo,

Thomaso,

Yakobo mwana wa Alfayo,

Thadayo,

Simoni Mzelote

19 na Yuda Iskariote,[b] ambaye ndiye aliyemsaliti Yesu.

Nguvu ya Yesu Inatoka kwa Mungu

(Mt 12:22-32; Lk 11:14-23; 12:10)

20 Kisha Yesu akaenda nyumbani. Kwa mara nyingine tena umati wa watu ukakusanyika, kiasi kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakupata nafasi ya kula. 21 Familia ya Yesu ilipoyasikia haya, walikwenda kumchukua kwa sababu watu walisema amerukwa na akili.

22 Walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu walikuwa wanasema, “Yeye ana Beelzebuli[c] ndani yake! Kwani anafukuza mashetani kwa nguvu ya mkuu wa mashetani!”

23 Yesu akawaita na kuanza kuzungumza nao kwa kulinganisha: “Inawezekanaje Shetani ambaye ni roho mchafu kufukuza mashetani? 24 Ikiwa basi ufalme utagawanyika katika sehemu mbili zinazopingana zenyewe kwa zenyewe, ufalme huo hautaendelea. 25 Vivyo hivyo ufalme wa Shetani ukigawanyika naye akapigana dhidi ya pepo wake wabaya, basi huo utakuwa ndio mwisho wa ufalme wake. Pia ikiwa nyumba itapingana yenyewe kwa yenyewe, nyumba hiyo haitaweza kusalimika. 26 Kwa hiyo ikiwa Shetani atajipinga mwenyewe na kugawanyika basi hataweza kuendelea na huo utakuwa mwisho wake.

27 Hakika, hakuna anayeweza kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuzichukua mali zake bila kwanza kumfunga mtu huyo mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kuiba katika nyumba hiyo.

28 Ninawaambia ukweli: Watu wanaweza kusamehewa dhambi zao zote na maneno yao yenye matusi kwa Mungu. 29 Lakini yeyote atakayemtukana Roho Mtakatifu hatasamehewa kabisa. Kwa sababu mtu anayefanya hivyo atakuwa na hatia ya dhambi isiyosamehewa milele.”

30 Yesu alisema haya kwa sababu walimu wa sheria walikuwa wanasema, “Yeye ana pepo mchafu ndani yake.”

Wafuasi wa Yesu ni Familia Yake Halisi

(Mt 12:46-50; Lk 8:19-21)

31 Kisha mama yake Yesu na nduguze wakaja. Wao walisimama nje na wakamtuma mtu aende kumwita ndani. 32 Humo lilikuwepo kundi lililoketi kumzunguka, lakini wao wakamwambia, “Tazama! Mama yako, kaka zako na dada zako wako[d] nje wanakusubiri.”

33 Yesu akauliza, “Mama yangu ni nani na kaka zangu ni akina nani?” 34 Yesu akawatazama wale walioketi kumzunguka na akasema “Hapa yupo mama yangu na wapo kaka zangu na dada zangu! 35 Yeyote anayeyafanya mapenzi ya Mungu ndiye kaka yangu, dada yangu, na mama yangu.”

Footnotes

  1. 3:2 Walitaka … siku ya Sabato Haikuruhusiwa kwa Wayahudi kufanya kazi siku ya Sabato na wengi waliamini kumponya mtu ambaye hakuwa katika hatari ya kufa ilikuwa ni kazi.
  2. 3:19 Iskariote Yaweza kuwa “kutoka Kirioti”, mji kusini mwa Yuda.
  3. 3:22 Beelzebuli Kwa maana ya kawaida, “Shetani”. Jina hili limetumika badala ya lile la Shetani.
  4. 3:32 na dada zako wako Nakala zingine za Kiyunani hazina maneno haya.

Yesu Amponya Mtu Aliyelemaa Mkono

Yesu aliingia tena katika sinagogi na mtu mmoja aliyelemaa mkono alikuwapo pia. Baadhi ya watu waliokuwa wakimtega, ili wapate sababu ya kumshtaki, walimtazama kwa makini waone kama atamponya huyo kilema siku ya sabato. Yesu akamwambia yule mwe nye mkono uliolemaa, “Njoo hapa mbele.”

Yesu akawauliza, “Ni lipi lililo halali siku ya sabato? Kufanya jema, au baya? Kusalimisha maisha au kuua?” Wakakaa kimya.

Yesu akawatazama kwa hasira, akahuzunishwa na ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akauny oosha, nao ukapona kabisa! Kisha Mafarisayo wakatoka nje, wakaenda kushauriana na kundi la wafuasi wa Herode mbinu za kum wua Yesu.

Umati Wa Watu Wamfuata Yesu

Yesu pamoja na wanafunzi wake waliondoka mahali hapo wakaenda ziwani wakifuatwa na umati mkubwa wa watu kutoka Gali laya na Yudea. Na watu kutoka Yerusalemu, Idumaya, na eneo lote la ng’ambo ya Yordani, sehemu za Tiro na Sidoni, waliposi kia mambo aliyokuwa akitenda, wakamwendea. Akawaomba wanafunzi wake wamwandalie mashua ili asisongwe na kubanwa sana na watu. 10 Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wote wenye mar adhi walikuwa wakisukumana wapate kumgusa. 11 Na kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia kwa sauti kuu, “Wewe ni Mwana wa Mungu.” 12 Lakini aliwaamuru wasimtambulishe kwa watu.

Yesu Achagua Mitume Kumi Na Wawili

13 Yesu alipanda mlimani akawaita wale aliowataka, nao wakaja. 14 Akawachagua kumi na wawili wafuatane naye na awatume kuhubiri na 15 wawe na mamlaka ya kufukuza pepo. 16 Hawa ndio aliowachagua: Simoni, ambaye alimwita Petro, 17 Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo ambao aliwaita Boanerge, yaani wana wa ngurumo; 18 Andrea; Filipo; Bartholomayo; Mathayo; Tomaso; Yakobo, mwana wa Alfayo; Thadayo; Simoni, Mkanaani; na 19 Yuda

Yesu Na Beelzebuli

20 Yesu akarudi nyumbani. Umati wa watu ukamfuata tena, hata yeye na wanafunzi wake wakashindwa kula chakula. 21 Ndugu zake walipopata habari walikuja kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”

22 Walimu wa sheria waliotoka Yerusalemu walikuwa wakisema, “Amepagawa na Beelzebuli, mkuu wa mashetani; na ni kwa uwezo wa Beelzebuli anawafukuza mashetani.”

Beelzebuli anawafukuza mashetani.”

23 Basi Yesu akawaita akazungumza nao kwa mifano: “Shetani awezaje kufukuza shetani? 24 Ikiwa utawala wa nchi umegawanyika wenyewe, hauwezi kudumu. 25 Hali kadhalika kama jamaa moja ime gawanyika yenyewe kwa yenyewe, jamaa hiyo haiwezi kudumu. 26 Na kama shetani akijipiga vita yeye mwenyewe hatatimiza cho chote ila mwisho wake umekaribia. 27 Pia hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumwibia vitu vyake vyote pasipo kwanza kumfunga huyo mwenye nyumba mwenye nguvu. Akisha mfunga, ndipo anaweza kumwibia kila kitu.

28 “Nawaambieni kweli, dhambi zote watendazo wanadamu na maneno yote ya kufuru wasemayo, watasamehewa. 29 Lakini ye yote anayemtukana Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” 30 Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema ana pepo mchafu.

Mama Na Ndugu Wa Yesu

31 Mama yake Yesu na ndugu zake wakafika wakasimama nje wakamtuma mtu amwite. 32 Umati wa watu waliokuwa wameketi kum zunguka wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wana kutafuta.”

33 Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni akina nani?”

34 Akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka, akasema, “Hawa ndio mama zangu na ndugu zangu. 35 Mtu ye yote anayetenda mapenzi ya Mungu ndiye ndugu yangu na dada yangu na mama yangu.”

And he entered again into the synagogue; and there was a man there which had a withered hand.

And they watched him, whether he would heal him on the sabbath day; that they might accuse him.

And he saith unto the man which had the withered hand, Stand forth.

And he saith unto them, Is it lawful to do good on the sabbath days, or to do evil? to save life, or to kill? But they held their peace.

And when he had looked round about on them with anger, being grieved for the hardness of their hearts, he saith unto the man, Stretch forth thine hand. And he stretched it out: and his hand was restored whole as the other.

And the Pharisees went forth, and straightway took counsel with the Herodians against him, how they might destroy him.

But Jesus withdrew himself with his disciples to the sea: and a great multitude from Galilee followed him, and from Judaea,

And from Jerusalem, and from Idumaea, and from beyond Jordan; and they about Tyre and Sidon, a great multitude, when they had heard what great things he did, came unto him.

And he spake to his disciples, that a small ship should wait on him because of the multitude, lest they should throng him.

10 For he had healed many; insomuch that they pressed upon him for to touch him, as many as had plagues.

11 And unclean spirits, when they saw him, fell down before him, and cried, saying, Thou art the Son of God.

12 And he straitly charged them that they should not make him known.

13 And he goeth up into a mountain, and calleth unto him whom he would: and they came unto him.

14 And he ordained twelve, that they should be with him, and that he might send them forth to preach,

15 And to have power to heal sicknesses, and to cast out devils:

16 And Simon he surnamed Peter;

17 And James the son of Zebedee, and John the brother of James; and he surnamed them Boanerges, which is, The sons of thunder:

18 And Andrew, and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and James the son of Alphaeus, and Thaddaeus, and Simon the Canaanite,

19 And Judas Iscariot, which also betrayed him: and they went into an house.

20 And the multitude cometh together again, so that they could not so much as eat bread.

21 And when his friends heard of it, they went out to lay hold on him: for they said, He is beside himself.

22 And the scribes which came down from Jerusalem said, He hath Beelzebub, and by the prince of the devils casteth he out devils.

23 And he called them unto him, and said unto them in parables, How can Satan cast out Satan?

24 And if a kingdom be divided against itself, that kingdom cannot stand.

25 And if a house be divided against itself, that house cannot stand.

26 And if Satan rise up against himself, and be divided, he cannot stand, but hath an end.

27 No man can enter into a strong man's house, and spoil his goods, except he will first bind the strong man; and then he will spoil his house.

28 Verily I say unto you, All sins shall be forgiven unto the sons of men, and blasphemies wherewith soever they shall blaspheme:

29 But he that shall blaspheme against the Holy Ghost hath never forgiveness, but is in danger of eternal damnation.

30 Because they said, He hath an unclean spirit.

31 There came then his brethren and his mother, and, standing without, sent unto him, calling him.

32 And the multitude sat about him, and they said unto him, Behold, thy mother and thy brethren without seek for thee.

33 And he answered them, saying, Who is my mother, or my brethren?

34 And he looked round about on them which sat about him, and said, Behold my mother and my brethren!

35 For whosoever shall do the will of God, the same is my brother, and my sister, and mother.

Healing on the Sabbath(A)

And (B)He entered the synagogue again, and a man was there who had a withered hand. So they (C)watched Him closely, whether He would (D)heal him on the Sabbath, so that they might [a]accuse Him. And He said to the man who had the withered hand, [b]“Step forward.” Then He said to them, “Is it lawful on the Sabbath to do good or to do evil, to save life or to kill?” But they kept silent. And when He had looked around at them with anger, being grieved by the (E)hardness of their hearts, He said to the man, “Stretch out your hand.” And he stretched it out, and his hand was restored [c]as whole as the other. (F)Then the Pharisees went out and immediately plotted with (G)the Herodians against Him, how they might destroy Him.

A Great Multitude Follows Jesus(H)

But Jesus withdrew with His disciples to the sea. And a great multitude from Galilee followed Him, (I)and from Judea and Jerusalem and Idumea and beyond the Jordan; and those from Tyre and Sidon, a great multitude, when they heard how (J)many things He was doing, came to Him. So He told His disciples that a small boat should be kept ready for Him because of the multitude, lest they should crush Him. 10 For He healed (K)many, so that as many as had afflictions pressed about Him to (L)touch Him. 11 (M)And the unclean spirits, whenever they saw Him, fell down before Him and cried out, saying, (N)“You are the Son of God.” 12 But (O)He sternly warned them that they should not make Him known.

The Twelve Apostles(P)

13 (Q)And He went up on the mountain and called to Him those He Himself wanted. And they came to Him. 14 Then He appointed twelve, [d]that they might be with Him and that He might send them out to preach, 15 and to have [e]power [f]to heal sicknesses and to cast out demons: 16 [g]Simon, (R)to whom He gave the name Peter; 17 James the son of Zebedee and John the brother of James, to whom He gave the name Boanerges, that is, “Sons of Thunder”; 18 Andrew, Philip, Bartholomew, Matthew, Thomas, James the son of Alphaeus, Thaddaeus, Simon the Cananite; 19 and Judas Iscariot, who also betrayed Him. And they went into a house.

A House Divided Cannot Stand(S)

20 Then the multitude came together again, (T)so that they could not so much as eat bread. 21 But when His (U)own people heard about this, they went out to lay hold of Him, (V)for they said, “He is out of His mind.”

22 And the scribes who came down from Jerusalem said, (W)“He has Beelzebub,” and, “By the (X)ruler of the demons He casts out demons.”

23 (Y)So He called them to Himself and said to them in parables: “How can Satan cast out Satan? 24 If a kingdom is divided against itself, that kingdom cannot stand. 25 And if a house is divided against itself, that house cannot stand. 26 And if Satan has risen up against himself, and is divided, he cannot stand, but has an end. 27 (Z)No one can enter a strong man’s house and plunder his goods, unless he first binds the strong man. And then he will plunder his house.

The Unpardonable Sin(AA)

28 (AB)“Assuredly, I say to you, all sins will be forgiven the sons of men, and whatever blasphemies they may utter; 29 but he who blasphemes against the Holy Spirit never has forgiveness, but is subject to eternal condemnation” 30 because they (AC)said, “He has an unclean spirit.”

Jesus’ Mother and Brothers Send for Him(AD)

31 (AE)Then His brothers and His mother came, and standing outside they sent to Him, calling Him. 32 And a multitude was sitting around Him; and they said to Him, “Look, Your mother and Your brothers [h]are outside seeking You.”

33 But He answered them, saying, “Who is My mother, or My brothers?” 34 And He looked around in a circle at those who sat about Him, and said, “Here are My mother and My brothers! 35 For whoever does the (AF)will of God is My brother and My sister and mother.”

Footnotes

  1. Mark 3:2 bring charges against
  2. Mark 3:3 Lit. Arise into the midst
  3. Mark 3:5 NU omits as whole as the other
  4. Mark 3:14 NU adds whom He also named apostles
  5. Mark 3:15 authority
  6. Mark 3:15 NU omits to heal sicknesses and
  7. Mark 3:16 NU and He appointed the twelve: Simon . . .
  8. Mark 3:32 NU, M add and Your sisters