預言聖殿被毀

13 耶穌走出聖殿的時候,有一個門徒對祂說:「老師,你看!這是多麼大的石頭,多麼宏偉的建築啊!」

耶穌說:「你看見這宏偉的建築了嗎?將來它要被完全拆毀,找不到兩塊疊在一起的石頭。」

耶穌面向聖殿坐在橄欖山上,彼得、雅各、約翰和安得烈私下來問祂: 「請告訴我們,這些事什麼時候會發生?有什麼預兆?」

耶穌對他們說:「你們要小心,免得被人迷惑。 將有很多人冒我的名來,說,『我是基督』,欺騙許多人。

「你們聽見戰爭爆發、戰訊頻傳時,不要驚慌,因為這些事必然發生,只是末日還沒有到。

「民族將與民族互鬥,國家將與國家相爭,各處將有地震和饑荒。這些只是災難[a]的開始。

「你們要小心,因為你們將被送上法庭,將在會堂裡受鞭打,又將為了我的緣故在官長和君王面前做見證。 10 不過,福音一定要先傳遍天下。 11 你們被拘捕,受審訊的時候,不用預先考慮怎樣辯解,到時候賜給你們什麼話,你們就說什麼話,因為那時候說話的不是你們自己,而是聖靈。

12 「那時,人必把自己的弟兄置於死地,父親必把兒子置於死地,兒女必反叛父母,置他們於死地。 13 你們將為我的名而被眾人憎恨,但堅忍到底的必定得救。

大災難

14 「當你們看見『那帶來毀滅的可憎之物』站在不當站的地方時(讀者須會意),住在猶太地區的人要逃到山上去; 15 在屋頂上的人不要下來,不要進房屋收拾行李; 16 在田間的人不要回家取外衣。 17 那時,孕婦和哺育嬰兒的母親們可就遭殃了! 18 你們要祈求上帝使這些事不要在冬天發生, 19 因為那是上帝創造天地以來空前絕後的大災難。 20 如果主不縮短災期,恐怕沒有人能活命,但為了祂所揀選的子民,祂已經縮短災期。 21 那時,如果有人對你們說,『看啊!基督在這裡』,或說,『基督在那裡』,你們不要相信。 22 因為假基督和假先知將出現,行各種神蹟奇事,如果可能,甚至會迷惑上帝揀選的子民。 23 你們要小心,我已經把一切預先告訴你們了。

人子降臨

24 「大災難過後,
太陽昏暗,
月亮無光,
25 星宿隕落,
天體震動。

26 那時,世人必看到人子駕著雲、帶著極大的能力和榮耀降臨。 27 祂必差遣天使從四面八方、天涯海角招聚祂揀選的人。

28 「你們可以從無花果樹學個道理。當無花果樹發芽長葉的時候,你們就知道夏天快來了。 29 同樣,當你們看見這些事情發生時,就知道人子快來了,就在門口。 30 我實在告訴你們,這個世代還沒有過去,這一切都要發生。 31 天地都要過去,我的話卻永遠長存。

32 「但沒有人知道那日子和時辰何時來到,連天上的天使和人子都不知道,只有天父知道。 33 你們要小心,警醒禱告,因為你們不知道那日子何時來到。

34 「這就好像一個人在出遠門之前,把家中的事交給僕人,讓他們各做各的工作,又吩咐守門的人要警醒。 35 所以你們要警醒,因為你們不知道主人什麼時候回來,可能是黃昏,可能是夜半,也可能是黎明或早上。 36 別讓他突然回來時看到你們在睡覺。 37 我勸你們也勸所有的人,要警醒!」

Footnotes

  1. 13·8 災難」希臘文是「生產之痛」。

Yesu Anatabiri Kubomolewa Kwa Hekalu

13 Alipokuwa akitoka nje ya Hekalu, mmojawapo wa wanafunzi wake akamwambia, “Mwalimu, ona jinsi mawe haya na majengo haya yalivyo maridadi!”

Yesu akamjibu, “Unayaona majengo haya yalivyo makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, yote yatabomo lewa.”

Yesu Anawaambia Wafuasi Wake Wajiandae Kwa Mateso

Alipokuwa ameketi kwenye mlima wa Mizeituni akiliangalia Hekalu, Petro, Yakobo na Yohana walimwuliza faraghani, “Tafadhali tuambie, mambo haya yatatokea lini, na ni ishara gani zitaonyesha kuwa karibu yatatimia?” Yesu akaanza kuwaeleza: “Jihadharini mtu asije akawadanganya. Wengi wata kuja wakilitumia jina langu na kusema, ‘Mimi ndiye’ na wata wadanganya wengi. Na mkisikia habari za vita na uvumi juu ya vita, msishtuke. Mambo haya hayana budi kutokea, lakini mwisho utakuwa bado. Mataifa yatapigana na falme kushambuliana. Matetemeko ya ardhi yatatokea sehemu mbalimbali na kutakuwa na njaa. Lakini huu utakuwa kama maumivu ya mwanzo tu ya uchungu wa uzazi. Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watu watawapeleka mahakamani na mtapigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ndipo mtaweza kutoa ushuhuda kuhusu Habari Njema. 10 Lakini kabla mwisho kufika, Habari Njema itahubiriwa kwa mataifa yote. 11 “Mtakapokamatwa na kupelekwa mahakamani, msihangaike kuhusu mtakalosema. Semeni lo lote litakalowajia wakati huo, kwa sababu maneno mtakayosema si yenu bali yatatoka kwa Roho Mtaka tifu.

12 “Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe; baba atamsaliti mwanae. Watoto watawaasi wazazi wao na kusababisha wauawe. 13 Kila mtu atawachukia kwa ajili yangu; lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokolewa.

14 “Mtakapoona ile ‘sanamu ya chukizo’ imesimama mahali isipostahili - msomaji na aelewe maana yake -basi wale walioko Yudea wakimbilie milimani. 15 Mtu aliyeko juu ya nyumba asiter emke kuingia ndani kuchukua cho chote. 16 Aliyeko shambani asi rudi nyumbani kuchukua koti lake. 17 Ole wao akina mama waja wazito na watakaokuwa wakinyonyesha siku hizo! 18 Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa masika. 19 Kwa maana siku hizo itaku wapo dhiki kuu ambayo haijapata kutokea tangu dunia ilipoumbwa, wala haitatokea tena. 20 Na kama Bwana hakuufupisha muda huo wa dhiki, hakuna mtu ambaye angesalimika; lakini kwa ajili ya watu wake aliowachagua, ameufupisha muda huo.

21 “Na wakati huo mtu akiwaambia, ‘Tazama, Kristo huyu hapa’ au , ‘Tazama, yule pale,’ msiamini. 22 Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo nao watafanya ishara na miujiza ili kuwadanganya hata wale waliochaguliwa na Mungu, kama ikiwezekana. 23 Kwa hiyo jihadharini kwa maana nimewaambia mambo haya kabla hayajatokea.”

Kuja Kwa Mwana Wa Adamu

24 “Siku hizo, baada ya hiyo dhiki, jua litatiwa giza na mwezi hautatoa mwanga wake. 25 Nyota zitaanguka kutoka mbinguni na nguvu za anga zitatikisika. 26 Ndipo watu wote wataniona mimi Mwana wa Adamu nikija katika mawingu kwa nguvu nyingi na utu kufu. 27 Nami nitawatuma malaika wawakusanye watu wangu kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho wa nchi hadi mwisho wa mbi ngu.

28 “Sasa jifunzeni jambo hili kutoka kwa mtini: mwonapo matawi ya mtini yakianza kulainika na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. 29 Hali kadhalika mtaka poyaona mambo haya yanatokea, tambueni kwamba mimi Mwana wa Adamu, ni karibu kuja. 30 Ninawaambieni hakika, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo haya kutokea. 31 Mbingu na nchi zita toweka, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”

Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa

32 “Hakuna ajuaye siku hiyo itakuwa lini au saa ngapi; hata malaika mbinguni hawajui wala mimi Mwana sijui, isipokuwa Mungu Baba peke yake. 33 “Jiandaeni, muwe macho. Kwa maana hamjui wakati mambo haya yatakapotokea. 34 Ni kama mtu anayesafiri na kuwaachia wat umishi wake madaraka, kila mtu na wajibu wake; kisha akamwambia mlinzi wa mlango awe macho. 35 Kesheni basi, kwa sababu hamjui ni lini bwana mwenye nyumba atarudi. Anaweza akaja jioni, au usiku wa manane au alfajiri au mapambazuko. 36 Kama akija gha fla, pasipo ninyi kumtazamia, asije awakute mmelala. 37 Na haya ninayowaambia ninyi nawaambia watu wote: Kesheni!”