Yesu Afundisha Kuhusu Talaka

10 Yesu akaondoka mahali pale akavuka mto wa Yordani, akaenda sehemu ya Yudea. Umati wa watu ukamfuata tena na kama kawaida yake akawafundisha.

Baadhi ya Mafarisayo wakamjia wakitaka kumtega, wakamwul iza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake?”

Yesu akawajibu, “Musa aliwaamuruje?” Wakamjibu, “Musa aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”

Yesu akawaambia, “Musa aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mume na mke. Na kwa sababu hii mume atamwacha baba yake na mama yake na hao wawili, watakuwa mwili mmoja.’ Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena bali mwili mmoja. Basi, alichokiun ganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”

10 Baadaye waliporudi nyumbani , wanafunzi wa Yesu walimwul iza kuhusu jambo hili.

11 Akawajibu, “Mtu ye yote anayempa mkewe talaka na kuoa mke mwingine, anazini kwa yule mke aliyempa talaka. 12 Na mwa namke anayempa mumewe talaka na kuolewa na mume mwingine, anazini pia.”

Read full chapter