Add parallel Print Page Options

Gavana Pilato Amhoji Yesu

(Mt 27:1-2,11-14; Lk 23:1-5; Yh 18:28-38)

15 Asubuhi na mapema, Mara tu ilipofika asubuhi viongozi wa makuhani, viongozi wazee wa Kiyahudi, walimu wa sheria, na baraza kuu lote la Wayahudi liliamua jambo la kufanya kwa Yesu. Walimfunga Yesu, wakamwondoa pale, na wakamkabidhi kwa Pilato.

Na Pilato akamwuliza: “Je, wewe ni Mfalme wa Wayahudi?”

Yesu akajibu “Hayo ni maneno yako mwenyewe.”

Na viongozi wa makuhani wakamshitaki Yesu kwa mambo mengi. Kwa hiyo Pilato akamwuliza Yesu swali lingine. Akasema, “Wewe hata kujibu hujibu? Angalia una mashitaka mengi wanayokuletea!”

Lakini Yesu hakujibu kitu chochote, na Pilato akastaajabu.

Pilato Ajaribu Kumwachia Huru Yesu

(Mt 27:15-31; Lk 23:13-25; Yh 18:39-19:16)

Kila mwaka wakati wa Sherehe ya Pasaka Pilato atamweka huru mfungwa mmoja atakayechaguliwa na watu. Mtu mmoja aliyeitwa Baraba alikuwa gerezani amefungwa pamoja na waasi. Watu hawa walifanya mauaji wakati wa fujo.

Watu walikuja Kwa Pilato na kumwomba amweke huru mfungwa kama alivyofanya siku zote. Yeye akawauliza, “Je, mnataka nimwache huru mfalme wa Wayahudi?” 10 Pilato alilisema hili kwa sababu alijua kuwa viongozi wa makuhani walimleta kwake kwa ajili ya wivu tu. 11 Lakini wale viongozi wa makuhani walimchochea amwache Baraba badala ya Yesu.

12 Lakini Pilato akawauliza watu tena, “Kwa hiyo nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”

13 Wakapiga kelele “Muue kwenye msalaba.”

14 Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini? Je, amefanya kosa gani?”

Lakini wote wakapiga kelele zaidi, “Muue kwenye msalaba!”

15 Pilato alitaka kuwaridhisha watu, kwa hiyo alimweka huru Baraba kwa ajili yao. Akaamuru maaskari wampige Yesu viboko na kisha akamtoa kwao ili akauawe kwenye msalaba.

16 Maaskari wakamwongoza Yesu hadi ndani ya baraza la jumba la gavana (lililojulikana kama Praitorio). Huko wakakiita pamoja kikosi cha maaskari. 17 Wakamvalisha Yesu joho la zambarau na wakafuma taji ya miiba na kumvisha kichwani. 18 Kisha wakaanza kumpigia saluti wakisema: “Heshima kwa Mfalme wa Wayahudi!” 19 Wakampiga tena na tena kichwani kwa fimbo na wakamtemea mate. Kisha wakapiga magoti mbele yake na kujifanya wanampa heshima kama mfalme. 20 Walipomaliza kumkejeli walimvua joho lile la kizambarau, na kumvisha mavazi yake mwenyewe. Baada ya hapo wakamtoa nje ili waweze kumsulubisha.

Read full chapter