Font Size
Marko 10:13-16
Neno: Bibilia Takatifu
Marko 10:13-16
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Anawabariki Watoto Wadogo
13 Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse lakini wanafunzi wake wakawakemea. 14 Yesu alipoona yaliyokuwa yakitokea alichukizwa, akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu kama hawa! 15 Ninawahakikishieni kwamba, mtu ye yote ambaye hataukubali Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.” 16 Akawakumbatia wale watoto wadogo, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
Read full chapter
Neno: Bibilia Takatifu (SNT)
Copyright © 1989 by Biblica