Add parallel Print Page Options

Swali Kuhusu Kufunga

(Mt 9:14-17; Mk 2:18-22)

33 Baadhi ya watu wakamwambia Yesu, “Wafuasi wa Yohana hufunga na kuomba mara kwa mara, vivyo hivyo wafuasi wa Mafarisayo. Lakini wafuasi wako hula na kunywa kila wakati.”

34 Yesu akawaambia, “Kwenye harusi huwezi kuwaambia marafiki wa bwana harusi wafunge wakati bwana harusi bado yuko pamoja nao. 35 Lakini muda ukifika na bwana harusi akaondolewa kwao. Watakuwa na huzuni, na watafunga.”

36 Yesu akawaambia mfano huu: “Hakuna anayekata kiraka kwenye vazi jipya na kukishona kwenye vazi la zamani. Ataharibu vazi jipya, na kiraka kutoka vazi jipya hakitakuwa sawa na vazi la zamani. 37 Pia hakuna mtu anayeweka divai mpya[a] katika viriba vya zamani. Divai mpya itavipasua, divai itamwagika, na viriba vitaharibika. 38 Daima mnaweka divai mpya kwenye viriba vipya. 39 Hakuna mtu ambaye baada ya kunywa divai ya zamani hutaka divai mpya. Kwa sababu husema, ‘Divai ya zamani ni nzuri.’”

Read full chapter

Footnotes

  1. 5:37 divai mpya Maji ya zabibu ambayo ndiyo yanaanza kuchachuka na hutengeneza mgandamizo ndani ya chombo kilichofungwa.

Yesu Aulizwa Habari Za Kufunga

33 Baadhi ya watu wakamwuliza Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga na kusali mara kwa mara. Mbona wanafunzi wako wanakula na kunywa tu?”

34 Yesu akawajibu, “Je, inawezekana wageni walioalikwa har usini kufunga wakati wakiwa na Bwana Harusi? 35 Lakini wakati utafika ambapo Bwana Harusi ataondolewa. Wakati huo ndipo wataka pofunga.

36 Yesu akawapa mfano akawaambia: “Hakuna mtu anayechana nguo mpya ili apate kiraka cha kuweka kwenye nguo kuu kuu. Akifa nya hivyo ataharibu ile nguo mpya na ile kuu kuu itaonekana mbaya zaidi ikiwa na kiraka kipya. 37 Wala watu hawaweki divai mpya katika viriba vilivyochakaa; ukifanya hivyo, hivyo viriba vitapa suka na divai yote itamwagika. 38 Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya. 39 Na pia hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai iliyoiva vizuri. Kwa maana husema, ‘Hii divai iliyoiva siku nyingi ni bora zaidi.’ ”

Read full chapter

Jesus Questioned About Fasting(A)

33 They said to him, “John’s disciples(B) often fast and pray, and so do the disciples of the Pharisees, but yours go on eating and drinking.”

34 Jesus answered, “Can you make the friends of the bridegroom(C) fast while he is with them? 35 But the time will come when the bridegroom will be taken from them;(D) in those days they will fast.”

36 He told them this parable: “No one tears a piece out of a new garment to patch an old one. Otherwise, they will have torn the new garment, and the patch from the new will not match the old. 37 And no one pours new wine into old wineskins. Otherwise, the new wine will burst the skins; the wine will run out and the wineskins will be ruined. 38 No, new wine must be poured into new wineskins. 39 And no one after drinking old wine wants the new, for they say, ‘The old is better.’”

Read full chapter