Luka 3:10-17
Neno: Bibilia Takatifu
10 Watu wakamwuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?” 11 Aka waambia: “Aliye na nguo mbili amgawie asiye na nguo; kama una chakula wape wenye njaa.”
12 Watoza kodi nao pia walikuja ili wabatizwe; wakamwuliza, “Bwana, na sisi inatupasa tufanyeje?”
13 Akawajibu: “ Msimdhulumu mtu kwa kudai kodi zaidi ya ile iliyoamriwa.”
14 Na baadhi ya askari wakamwuliza, “Na sisi je, tufanye nini?” Akawajibu: “Msichukue fedha za watu kwa kutumia nguvu; msiwashtaki watu kwa kuwasingizia makosa; bali mtosheke na misha hara yenu!”
15 Siku hizo watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wakijiuliza mioyoni mwao kama Yohana ndiye Kristo.
16 Yohana aliwajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini anayekuja ni mkuu kuliko mimi, sistahili hata kuwa mtumwa wake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 “Yuko tayari na pepeto lake mkononi, tayari kusafisha mahali pake pa kukusanyia mazao. Nafaka safi ataiweka ghalani lakini makapi atayachoma kwa moto usiozimika.”
Read full chapter
Luka 3:10-17
Neno: Bibilia Takatifu
10 Watu wakamwuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?” 11 Aka waambia: “Aliye na nguo mbili amgawie asiye na nguo; kama una chakula wape wenye njaa.”
12 Watoza kodi nao pia walikuja ili wabatizwe; wakamwuliza, “Bwana, na sisi inatupasa tufanyeje?”
13 Akawajibu: “ Msimdhulumu mtu kwa kudai kodi zaidi ya ile iliyoamriwa.”
14 Na baadhi ya askari wakamwuliza, “Na sisi je, tufanye nini?” Akawajibu: “Msichukue fedha za watu kwa kutumia nguvu; msiwashtaki watu kwa kuwasingizia makosa; bali mtosheke na misha hara yenu!”
15 Siku hizo watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wakijiuliza mioyoni mwao kama Yohana ndiye Kristo.
16 Yohana aliwajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini anayekuja ni mkuu kuliko mimi, sistahili hata kuwa mtumwa wake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 “Yuko tayari na pepeto lake mkononi, tayari kusafisha mahali pake pa kukusanyia mazao. Nafaka safi ataiweka ghalani lakini makapi atayachoma kwa moto usiozimika.”
Read full chapterCopyright © 1989 by Biblica