17 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Majaribu yanayowafanya watu watende dhambi hayana budi kuwepo. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha. Ingekuwa nafuu kama mtu huyo angefungiwa jiwe zito shingoni na kuzamishwa baharini kuliko kumfanya mmoja wa hawa wadogo atende dhambi. Kwa hiyo, jihadharini. Ndugu yako akikukosea mwonye; akiomba msamaha, msamehe. Hata kama akikuko sea mara saba kwa siku na kila mara aje kwako akisema, ‘Nisa mehe

Wanafunzi wakamwambia Bwana, “Tuzidishie imani.” Aka waambia, “Kama mngekuwa na imani kiasi cha punje ndogo sana ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu, ‘Ng’oka na mizizi yote ukaote baharini,’ nao ungewatii!”

Wajibu Wa Mtumishi

“Tuseme mmoja wenu ana mtumishi aliyekwenda shambani kulima au kuchunga kondoo. Je, mtumishi huyo akirudi utamwambia, ‘Karibu keti ule chakula’? Hata kidogo. Badala yake utamwambia, ‘Nitayarishie chakula na ujiandae kunihudumia ninapokula na kunywa, na baada ya hapo unaweza kula chakula chako.’ Wala hutamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza wajibu wake. 10 Hali kadhalika nanyi, baada ya kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi ni watumishi tusiostahili, tumetimiza wajibu wetu tu.”’

Yesu Atakasa Wakoma Kumi

11 Yesu alipokuwa akienda Yerusalemu alipitia kati ya Samaria na Galilaya. 12 Alipokuwa akikaribia kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma walikutana naye. 13 Wakasimama mbali wakaita kwa nguvu, “Yesu! Bwana! tuonee huruma!” 14 Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Na walipokuwa wakienda, wakapona ukoma wao. 15 Mmoja wao alipoona kwamba ame pona, akarudi kwa Yesu akimsifu Mungu kwa sauti kuu. 16 Kwa heshima kubwa akajitupa miguuni kwa Yesu akamshukuru. Yeye ali kuwa ni Msamaria .

17 Yesu akauliza, “Hawakuponywa wote kumi? Wako wapi wale tisa wengine? 18 Hakuna hata mmoja aliyekumbuka kurudi kumsifu Mungu isipokuwa huyu mgeni?” 19 Akamwambia, “Inuka, uende; imani yako imekuponya.” Ufalme Wa Mungu Utakavyokuja

20 Siku moja, Mafarisayo walipomwuliza Yesu Ufalme wa Mungu utakuja lini, aliwajibu hivi: “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuone kana, 21 wala watu hawatasema, ‘Huu hapa’ au ‘Ule kule’ kwa maana Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.”

22 Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Wakati utafika ambapo mtatamani kuiona siku yangu moja, mimi Mwana wa Adamu lakini ham taiona. 23 Watu watawaambia, ‘Yule pale’ au, ‘Huyu hapa!’ Msiwa kimbilie. 24 Kwa maana kama umeme unavyomulika mbingu kutoka upande mmoja hadi mwingine, ndivyo itakavyokuwa siku ya kuja kwangu, mimi Mwana wa Adamu. 25 Lakini kwanza itanipasa nite seke sana na kukataliwa na watu wa kizazi hiki. 26 Kama ilivy okuwa nyakati za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa siku ya kurudi kwangu, mimi Mwana wa Adamu. 27 Wakati wa Nuhu watu walikuwa wakila, wakinywa, wakioa na kuolewa mpaka siku ile Nuhu alipoingia katika safina. Ndipo mafuriko yakaja yakawaangamiza wote. 28 Hata nyakati za Lutu ilikuwa hivyo hivyo. Watu walikuwa wakila, waki nywa, wakifanya biashara, wakilima na kujenga. 29 Lakini siku ile Lutu alipoondoka Sodoma, moto ulishuka kutoka mbinguni uka waangamiza wote. 30 Ndivyo itakavyokuwa siku ambapo mimi Mwana wa Adamu nitakapotokea kwa utukufu.

31 “Siku hiyo, mtu akiwa darini na vitu vyake vikiwa ndani, asiteremke kuvichukua. Hali kadhalika atakayekuwa shambani asi rudi nyumbani kuchukua cho chote. 32 Kumbukeni yaliyompata mke wa Lutu! 33 Mtu ye yote anayejaribu kusalimisha maisha yake atayapoteza; na ye yote atakayekuwa tayari kuyapoteza maisha yake atayaokoa. 34 Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa wamelala kitanda kimoja; mmoja atachukuliwa, mwingine ataachwa. 35 Wana wake wawili watakuwa wanatwanga pamoja; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.” [ 36 Wanaume wawili watakuwa wanafanya kazi pamoja shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.] 37 Wakamwuliza, “Haya yatatokea wapi Bwana?” Akawaambia, “Pale ulipo mzoga, ndipo tai wanapokutanika.” Mfano Wa Hakimu Dhalimu

17 Then said he unto the disciples, It is impossible but that offences will come: but woe unto him, through whom they come!

It were better for him that a millstone were hanged about his neck, and he cast into the sea, than that he should offend one of these little ones.

Take heed to yourselves: If thy brother trespass against thee, rebuke him; and if he repent, forgive him.

And if he trespass against thee seven times in a day, and seven times in a day turn again to thee, saying, I repent; thou shalt forgive him.

And the apostles said unto the Lord, Increase our faith.

And the Lord said, If ye had faith as a grain of mustard seed, ye might say unto this sycamine tree, Be thou plucked up by the root, and be thou planted in the sea; and it should obey you.

But which of you, having a servant plowing or feeding cattle, will say unto him by and by, when he is come from the field, Go and sit down to meat?

And will not rather say unto him, Make ready wherewith I may sup, and gird thyself, and serve me, till I have eaten and drunken; and afterward thou shalt eat and drink?

Doth he thank that servant because he did the things that were commanded him? I trow not.

10 So likewise ye, when ye shall have done all those things which are commanded you, say, We are unprofitable servants: we have done that which was our duty to do.

11 And it came to pass, as he went to Jerusalem, that he passed through the midst of Samaria and Galilee.

12 And as he entered into a certain village, there met him ten men that were lepers, which stood afar off:

13 And they lifted up their voices, and said, Jesus, Master, have mercy on us.

14 And when he saw them, he said unto them, Go shew yourselves unto the priests. And it came to pass, that, as they went, they were cleansed.

15 And one of them, when he saw that he was healed, turned back, and with a loud voice glorified God,

16 And fell down on his face at his feet, giving him thanks: and he was a Samaritan.

17 And Jesus answering said, Were there not ten cleansed? but where are the nine?

18 There are not found that returned to give glory to God, save this stranger.

19 And he said unto him, Arise, go thy way: thy faith hath made thee whole.

20 And when he was demanded of the Pharisees, when the kingdom of God should come, he answered them and said, The kingdom of God cometh not with observation:

21 Neither shall they say, Lo here! or, lo there! for, behold, the kingdom of God is within you.

22 And he said unto the disciples, The days will come, when ye shall desire to see one of the days of the Son of man, and ye shall not see it.

23 And they shall say to you, See here; or, see there: go not after them, nor follow them.

24 For as the lightning, that lighteneth out of the one part under heaven, shineth unto the other part under heaven; so shall also the Son of man be in his day.

25 But first must he suffer many things, and be rejected of this generation.

26 And as it was in the days of Noe, so shall it be also in the days of the Son of man.

27 They did eat, they drank, they married wives, they were given in marriage, until the day that Noah entered into the ark, and the flood came, and destroyed them all.

28 Likewise also as it was in the days of Lot; they did eat, they drank, they bought, they sold, they planted, they builded;

29 But the same day that Lot went out of Sodom it rained fire and brimstone from heaven, and destroyed them all.

30 Even thus shall it be in the day when the Son of man is revealed.

31 In that day, he which shall be upon the housetop, and his stuff in the house, let him not come down to take it away: and he that is in the field, let him likewise not return back.

32 Remember Lot's wife.

33 Whosoever shall seek to save his life shall lose it; and whosoever shall lose his life shall preserve it.

34 I tell you, in that night there shall be two men in one bed; the one shall be taken, and the other shall be left.

35 Two women shall be grinding together; the one shall be taken, and the other left.

36 Two men shall be in the field; the one shall be taken, and the other left.

37 And they answered and said unto him, Where, Lord? And he said unto them, Wheresoever the body is, thither will the eagles be gathered together.