1-2 提阿非罗大人,已经有很多人根据最初的目击者和传道者给我们的口述,把我们中间发生的事记载下来。 我把一切事情从头至尾仔细查考之后,决定按次序写出来, 使你知道自己所学的道都是有真凭实据的。

天使预告施洗者约翰出生

犹太王希律执政期间,亚比雅的班里有位祭司名叫撒迦利亚,他妻子伊丽莎白是亚伦的后裔。 夫妻二人遵行主的一切诫命和条例,无可指责,在上帝眼中是义人。 但他们没有孩子,因为伊丽莎白不能生育,二人又年纪老迈。

有一天,轮到撒迦利亚他们那一班祭司当值, 他们按照祭司的规矩抽签,抽中撒迦利亚到主的殿里去烧香。 10 众百姓都在外面祷告。 11 那时,主的天使在香坛的右边向撒迦利亚显现, 12 撒迦利亚见了,惊慌害怕起来。

13 天使对他说:“撒迦利亚,不要害怕,你的祷告已蒙垂听。你的妻子伊丽莎白要为你生一个儿子,你要给他取名叫约翰。 14 你必欢喜快乐,许多人也会因为他的诞生而欣喜雀跃, 15 因为他将成为主伟大的仆人。他必滴酒不沾,并且在母腹里就被圣灵充满。 16 他将劝导许多以色列人回心转意,归顺主——他们的上帝。 17 他将以先知以利亚的心志和能力做主的先锋,使父亲的心转向儿女,使叛逆的人回转、顺从义人的智慧,为主预备合用的子民。”

18 撒迦利亚对天使说:“我已经老了,我的妻子也上了年纪,我如何知道这是真的呢?” 19 天使回答说:“我是侍立在上帝面前的加百列,奉命来向你报这喜讯。 20 我说的这些话到时候必定应验。但因为你不肯相信我的话,所以这事成就以前,你将变成哑巴,不能说话。”

21 人们在等候撒迦利亚,见他在圣殿里迟迟不出来,都感到奇怪。 22 后来他出来了,却成了哑巴,不能说话,只能打手势,大家意识到他在圣殿里看见了异象。 23 撒迦利亚供职期满,就回家去了。 24 不久,伊丽莎白果然怀了孕,她有五个月闭门不出。 25 她说:“主真是眷顾我,除掉了我不生育的羞耻。”

天使预告耶稣降生

26 伊丽莎白怀孕六个月的时候,天使加百列又奉上帝的命令到加利利的拿撒勒, 27 去见一位童贞女,她叫玛丽亚。玛丽亚已经和大卫的后裔约瑟订了婚。

28 天使到了玛丽亚那里,说:“恭喜你,蒙大恩的女子,主与你同在!”

29 玛丽亚听了觉得十分困惑,反复思想这话的意思。

30 天使对她说:“玛丽亚,不要害怕,你在上帝面前已经蒙恩了。 31 你要怀孕生子,并给祂取名叫耶稣。 32 祂伟大无比,将被称为至高者的儿子,主上帝要把祂祖先大卫的王位赐给祂。 33 祂要永远统治以色列[a],祂的国度永无穷尽。”

34 玛丽亚对天使说:“这怎么可能呢?我还是童贞女。”

35 天使回答说:“圣灵要临到你身上,至高者的能力要荫庇你,所以你要生的那圣婴必称为上帝的儿子。 36 看啊,你的亲戚伊丽莎白年纪老迈,一向不能生育,现在已经怀男胎六个月了。 37 因为上帝无所不能。”

38 玛丽亚说:“我是主的婢女,愿你所说的话在我身上成就。”于是天使离开了她。

玛丽亚看望伊丽莎白

39 不久,玛丽亚便动身赶到犹太山区的一座城, 40 进了撒迦利亚的家,向伊丽莎白请安。 41 伊丽莎白一听见玛丽亚的问安,腹中的胎儿便跳动起来,伊丽莎白被圣灵充满, 42 高声喊着说:“在妇女中你是最蒙福的!你腹中的孩子也是蒙福的! 43 我主的母亲来探望我,我怎么敢当呢? 44 我一听到你问安的声音,腹中的孩子就欢喜跳动。 45 相信主所说的话必实现的女子有福了!”

46 玛丽亚说:
“我的心尊主为大,
47 我的灵因我的救主上帝而欢喜,
48 因祂眷顾我这卑微的婢女,
从今以后,
世世代代都要称我是有福的。
49 全能者在我身上行了奇事,
祂的名是神圣的。
50 祂怜悯敬畏祂的人,
直到世世代代。
51 祂伸出臂膀,施展大能,
驱散心骄气傲的人。
52 祂使当权者失势,
叫谦卑的人升高。
53 祂使饥饿的得饱足,
叫富足的空手而去。
54 祂扶助了自己的仆人以色列,
55 祂要施怜悯给亚伯拉罕和他的子孙,
直到永远,
正如祂对我们祖先的应许。”

56 玛丽亚和伊丽莎白同住了约三个月,便回家去了。

施洗者约翰出生

57 伊丽莎白的产期到了,生下一个儿子。 58 亲戚和邻居听见主向她大施怜悯,都和她一同欢乐。 59 到了第八天,他们来给孩子行割礼,想照他父亲的名字给他取名叫撒迦利亚。

60 但伊丽莎白说:“不!要叫他约翰。”

61 他们说:“你们家族中没有人用这个名字啊!” 62 他们便向他父亲打手势,问他要给孩子起什么名字。 63 撒迦利亚就要了一块写字板,写上:“他的名字叫约翰。”大家看了都很惊奇。 64 就在那时,撒迦利亚恢复了说话的能力,便开口赞美上帝。 65 住在周围的人都很惧怕,这消息很快就传遍了整个犹太山区。 66 听见的人都在想:“这孩子将来会怎样呢?因为主与他同在。”

撒迦利亚的预言

67 孩子的父亲撒迦利亚被圣灵充满,便预言说:

68 “主——以色列的上帝当受称颂,
因祂眷顾、救赎了自己的子民,
69 在祂仆人大卫的家族中为我们兴起了一位大能的拯救者[b]
70 正如祂从亘古借着祂圣先知们的口所说的。
71 祂要从仇敌和一切恨我们之人手中拯救我们。
72 祂怜悯我们的祖先,
持守自己的圣约,
73 就是祂对我们的先祖亚伯拉罕所起的誓,
74 要把我们从仇敌手中拯救出来,
75 使我们一生一世在圣洁和公义中坦然无惧地事奉祂。
76 至于你,我的儿子啊!
你将要被称为至高者的先知,
因为你要走在主的前面,
为祂预备道路,
77 使百姓因罪得赦免而明白救恩的真谛。
78 由于上帝的怜悯,
清晨的曙光必从高天普照我们,
79 照亮那些生活在黑暗中和死亡阴影下的人,
带领我们走平安的道路。”

80 那孩子渐渐长大,心灵强健,在向以色列人公开露面之前,一直住在旷野。

Footnotes

  1. 1:33 以色列”希腊文是“雅各的家”。
  2. 1:69 拯救者”希腊文是“拯救的角”。

Luka Aandika Kuhusu Maisha ya Yesu

Mheshimiwa Theofilo:[a]

Watu wengine wengi wamejaribu kuandika juu ya mambo yaliyotokea katikati yetu ili kuukamilisha mpango wa Mungu. Mambo hayo waliyoyaandika yanalingana na yale tuliyosikia kutoka kwa watu walioyaona tangu mwanzo. Na walimtumikia Mungu kwa kuwaambia wengine ujumbe wake. Nimechunguza kila kitu kwa makini tangu mwanzo. Na nimeona kuwa ni vyema nikuandikie kwa mpangilio mzuri. Nimefanya hivi ili uwe na uhakika kuwa yale uliyofundishwa ni ya kweli.

Malaika Amjulisha Zakaria Kuhusu Kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji

Herode alipokuwa mfalme wa Uyahudi, alikuwepo kuhani mmoja aliyeitwa Zakaria, aliyekuwa mmoja wa makuhani wa kikundi[b] cha Abiya. Mkewe alikuwa mzaliwa wa ukoo wa Haruni, na jina lake alikuwa Elizabeti. Wote wawili Zakaria na Elizabeti walikuwa wema waliompendeza Mungu na daima walifanya yote yaliyoamriwa na Bwana na kila mara walifuata maagizo yake kwa ukamilifu. Lakini hawakuwa na watoto kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa, na wote wawili walikuwa wazee sana.

Ilipofika zamu ya kundi la Zakaria kuhudumu Hekaluni, yeye mwenyewe alikuwepo ili kuhudumu kama kuhani mbele za Mungu kwa ajili kundi. Makuhani walikuwa wanapiga kura kumchagua mmoja wao atakayeingia katika Hekalu la Bwana ili kufukiza uvumba. Na Zakaria alichaguliwa wakati huu. 10 Wakati wa kufukiza uvumba ulipofika watu wote walikusanyika nje ya Hekalu wakiomba.

11 Zakaria akiwa ndani ya Hekalu alitokewa na malaika wa Bwana akiwa amesimama mbele yake upande wa kulia wa madhabahu ya uvumba. 12 Zakaria alipomwona malaika aliogopa, na akaingiwa na hofu. 13 Lakini Malaika akamwambia, “Usiogope, Zakaria. Mungu amelisikia ombi lako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana. 14 Utafurahi sana, na watu wengine wengi watamfurahia pamoja nawe. 15 Atakuwa mkuu kwa ajili ya Bwana. Kamwe asinywe mvinyo wala kitu chochote kile kitakachomlewesha. Atajazwa Roho Mtakatifu tangu akiwa tumboni mwa mama yake.

16 Naye atawafanya Waisraeli wengi wamrudie Bwana Mungu wao. 17 Atamtangulia Bwana ili kuwaandaa watu kuupokea ujio wake. Atakuwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha wazazi na watoto wao na kuwafanya wale wasiomtii Mungu kubadilika na kuanza kumtii Mungu.”

18 Zakaria akamwambia malaika, “Nitajuaje kuwa haya unayosema ni ya kweli? Maana mimi ni mzee na mke wangu ana umri mkubwa pia.”

19 Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, ambaye daima husimama mbele za Mungu nikiwa tayari. Amenituma kuzungumza nawe na kukujulisha habari hizi njema. 20 Sasa sikiliza! Hautaweza kuzungumza mpaka siku ambayo mambo haya yatatokea kwa sababu hukuyaamini yale niliyokwambia. Lakini nilichosema hakika kitatokea.”

21 Watu waliokuwa nje ya Hekalu wakimngojea Zakaria walishangaa kwa sababu alikaa kwa muda mrefu ndani ya Hekalu. 22 Zakaria alipotoka nje hakuweza kuzungumza nao. Aliwafanyia watu ishara kwa mikono yake. Hivyo watu walitambua kuwa alikuwa ameona maono alipokuwa Hekaluni. 23 Zamu ya utumishi wake ilipokwisha alirudi nyumbani.

24 Wakati fulani baadaye, Elizabeti, mke wa Zakaria akawa mjamzito. Alikaa katika nyumba yake na hakutoka nje kwa miezi mitano. Alisema, 25 “Na sasa, hatimaye Bwana amenisaidia kwa kuniondolea aibu yangu.”

Malaika Atangaza Kuzaliwa kwa Yesu

26-27 Mwezi wa sita wa ujauzito wa Elizabeti, Mungu alimtuma malaika Gabrieli kwa msichana mmoja bikira aliyeishi Nazareti, mji wa Galilaya. Msichana huyo alikuwa amechumbiwa na Yusufu mzaliwa katika ukoo wa Daudi. Jina la bikira huyo lilikuwa Mariamu. 28 Malaika alimwendea na kusema “Salamu! Bwana yu pamoja nawe; Kwa kuwa neema yake iko juu yako.”

29 Lakini, Mariamu alichanganyikiwa kutokana na yale aliyosema malaika. Akajiuliza, “Salamu hii ina maana gani?”

30 Malaika akamwambia, “Usiogope Mariamu, kwa kuwa neema ya Mungu iko juu yako. 31 Sikiliza! Utapata mimba na kuzaa mtoto mwanamume, nawe utamwita jina lake Yesu. 32 Mtoto huyo atakuwa Mkuu na watu watamwita Mwana wa Mungu Aliye Mkuu Sana na Bwana Mungu atamfanya kuwa mfalme kama Daudi baba yake. 33 Naye ataitawala nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

34 Mariamu akamwambia malaika, “Jambo hili litatokeaje? Kwa maana mimi bado ni bikira.”

35 Malaika akamwambia Mariamu, “Roho Mtakatifu atakujia, na nguvu zake Mungu Mkuu zitakufunika. Na hivyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu na ataitwa Mwana wa Mungu. 36 Pia sikiliza hili: Jamaa yako Elizabeti ni mjamzito. Ijapokuwa ni mzee sana, atazaa mtoto wa kiume. Kila mtu alidhani hataweza kuzaa, lakini sasa huu ni mwezi wa sita wa ujauzito wake. 37 Mungu anaweza kufanya jambo lolote!”

38 Mariamu akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, basi jambo hili litokee kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka.

Mariamu Amtembelea Elizabeti

39 Mariamu akajiandaa na kwenda haraka katika mji mmoja ulio vilimani katika jimbo la Yuda. 40 Alikwenda nyumbani kwa Zakaria, alipofika akamsalimu Elizabeti. 41 Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akirukaruka, na Elizabeti akajazwa Roho Mtakatifu.

42 Kisha akapaza sauti na kumwambia Mariamu, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na mtoto utakayemzaa amebarikiwa. 43 Lakini jambo hili kuu limetokeaje kwangu, hata mama wa Bwana wangu aje kwangu? 44 Kwa maana sauti ya salamu yako ilipofika masikioni mwangu, mtoto aliye ndani yangu amerukaruka kwa furaha. 45 Umebarikiwa wewe uliyeamini kuwa mambo aliyokuambia Bwana yatatokea.”

Mariamu Amsifu Mungu

46 Mariamu akasema,

“Moyo wangu unamwadhimisha Bwana,
47     kwa maana, Yeye, Mungu na Mwokozi
    wangu amenipa furaha kuu!
48 Kwa maana ameonesha kunijali,
    mimi mtumishi wake, nisiye kitu.
Na kuanzia sasa watu wote
    wataniita mbarikiwa.
49 Kwa kuwa Mwenye Nguvu amenitendea mambo makuu.
    Jina lake ni takatifu.
50 Na huwapa rehema zake wale wamchao,
    kutoka kizazi hadi kizazi.
51 Ameonesha nguvu ya mkono wake;
    Amewatawanya wanaojikweza.
52 Amewaangusha watawala kutoka katika viti vyao vya enzi,
    na kuwakweza wanyenyekevu.
53 Amewashibisha wenye njaa kwa mambo mema,
    na amewatawanya matajiri bila ya kuwapa kitu.
54 Amemsaidia Israeli, watu aliowachagua ili wamtumikie.
    Amekumbuka kuonesha rehema;
55 Maana ndivyo alivyowaahidi baba zetu,
    Ibrahimu na wazaliwa wake.”

56 Mariamu alikaa na Elizabeti kwa muda wa kama miezi mitatu, kisha alirudi nyumbani kwake.

Kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji

57 Wakati ulipotimia kwa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto wa kiume. 58 Majirani na jamaa zake waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa mwema kwake, walifurahi pamoja naye.

59 Mtoto alipofikisha umri wa siku nane, walikuja kumtahiri.[c] Walipotaka kumwita mtoto Zakaria kutokana na jina la baba yake. 60 Mama yake akasema, “Hapana, mtoto ataitwa Yohana.”

61 Lakini wao wakamwambia, “Hakuna jamaa yako hata mmoja mwenye jina hilo.” 62 Ndipo wakamfanyia ishara baba yake wakimwuliza jina alilotaka kumpa mtoto.

63 Zakaria akataka ubao wa kuandikia,[d] Kisha akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangaa. 64 Mara hiyo hiyo mdomo wake ulifunguliwa na ulimi wake ukaachia, akaanza kuzungumza na kumsifu Mungu. 65 Majirani zao wakajawa hofu na watu katika sehemu zote za vilima katika jimbo la Yuda wakawa wanazungumza kuhusu jambo hili. 66 Watu wote waliosikia kuhusu mambo haya walijiuliza, wakisema, “Mtoto huyu atakuwa wa namna gani?” Kwa kuwa nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.

Zakaria Amsifu Mungu

67 Kisha Zakaria, baba yake Yohana, akajaa Roho Mtakatifu, akatabiri, akisema:

68 “Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli,
    kwa kuwa amekuja kuwasaidia
    watu wake na kuwaweka huru.
69 Na ametuletea sisi Mwokozi Mwenye Nguvu,
    kutoka katika ukoo wa mtumishi wake Daudi.
70 Hivi ndivyo alivyoahidi
    kupitia manabii wake watakatifu tangu zamani.
71 Aliahidi kwa Agano kuwa atatuokoa na adui zetu
    na milki za wote wanaotuchukia.
72 Ili kuonesha rehema kwa baba zetu,
    na kulikumbuka agano lake takatifu aliloagana nao.
73 Agano hili ni kiapo alichomwapia
    baba yetu Ibrahimu.
74 Alipoahidi kutuokoa kutoka katika nguvu za adui zetu,
    ili tuweze kumwabudu Yeye bila hofu.
75 Katika namna iliyo takatifu na yenye haki
    mbele zake siku zote za maisha yetu.

76 Sasa wewe, mtoto mdogo,
    utaitwa nabii wa Mungu Aliye Juu Sana,
kwa sababu utamtangulia Bwana
    kuandaa njia yake.
77 Utawaambia watu wake kwamba wataokolewa
    kwa kusamehewa dhambi zao.

78 Kwa rehema ya upendo wa Mungu wetu,
    siku mpya[e] itachomoza juu yetu kutoka mbinguni.
79 Kuwaangazia wale wanaoishi katika giza,
    kwa hofu ya mauti,
na kuongoza hatua zetu
    katika njia ya amani.”

80 Na hivyo mtoto Yohana akakua na kuwa na nguvu katika roho. Kisha akaishi maeneo yasiyo na watu mpaka wakati alipotokea hadharani akihubiri ujumbe wa Mungu kwa watu wa Israeli.

Footnotes

  1. 1:1 Theofilo Theofilo ndiye aliyemdhamini Luka katika mradi wa utafiti na uandishi wa kitabu hiki na kingine (Matendo ya Mitume). Ijapokuwa ni kama aliandikiwa yeye, makusudi ya mwandishi na Roho Mtakatifu ni kuwa watu wote wakisome. Theofilo maana yake ni “Mpendwa wa Mungu”.
  2. 1:5 makuhani wa kikundi Makuhani wa Kiyahudi waligawanywa katika vikundi 24. Tazama 1 Mambo ya Nyakati sura ya 24. Vikundi hivi 24 vya Makuhani vilihudumu katika Hekalu mjini Yerusalemu kwa zamu (mzunguko). Kila kikundi kilikuwa na zamu kwa wiki nzima, aghalabu wiki mbili kwa mwaka.
  3. 1:59 kumtahiri Yaani, kumfanyia tohara kama ilivyokuwa katika sheria ya Musa.
  4. 1:63 ubao wa kuandikia Ni ubao uliokuwa umepakwa nta au mpira ili usiloe.
  5. 1:78 siku mpya Kwa maana ya kawaida, “Alfajiri”, imetumika hapa kama ishara ikimaanisha Masihi, Bwana.