Bwana Wa Sabato

Siku moja ya sabato Yesu alikuwa akipita katika mashamba ya ngano. Wanafunzi wake wakawa wakivunja masuke ya ngano, wakayafi kicha na kula punje zake. Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnavunja sheria kwa kuvuna ngano siku ya sabato?”

Yesu akawajibu, “Ninyi hamsomi Maandiko? Hamjasoma alicho fanya Mfalme Daudi wakati yeye na wafuasi wake walipokuwa na njaa? Aliingia Hekaluni, akachukua ile mikate ya madhabahuni -ambayo huliwa na makuhani peke yao -akala, kisha akawapa na wafuasi wake wakala!” Akaongezea kusema, “Mimi Mwana wa Adamu ni Bwana wa sabato.”

Ikawa siku nyingine ya sabato Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi, na alikuwepo mtu ambaye mkono wake wa kuume uli kuwa umepooza. Walimu wa sheria na Mafarisayo wakawa wanangoja waone kama atamponya mtu siku ya sabato ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu alifahamu mawazo yao. Kwa hiyo akamwam bia yule aliyepooza mkono, ’Njoo usimame hapa mbele ili kila mtu akuone.” Yule mtu akaja mbele. Kisha Yesu akawageukia wale walimu wa sheria na Mafarisayo akasema, “Nawauliza ninyi, ni lipi lililo halali siku ya sabato - kutenda mema au kutenda mabaya? Kuokoa maisha au kuyaangamiza?” 10 Akawatazama watu wote waliokuwepo. Kisha akamwambia yule aliyepooza mkono, “Nyoosha mkono wako!” Akaunyoosha na mkono wake ukapona kabisa! 11 Wale wakuu wakakasirika sana. Wakaanza kushauriana, “Tumfa nye nini huyu Yesu?’ ’

Kuchaguliwa Kwa Mitume Kumi Na Wawili

12 Siku moja Yesu alikwenda milimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu. 13 Asubuhi akawaita wanafunzi wake, na kati yao akachagua kumi na wawili akawapa cheo cha “mitume.” Majina yao ni haya: 14 Simoni, aliyemwita Petro; Andrea, nduguye Simoni; Yakobo; Yohana; Filipo; Bartholomayo; 15 Mathayo; Tomaso; Yakobo, mwana wa Alfayo; Simoni, aliyeitwa Mzalendo; 16 Yuda, mwana wa Yakobo; na Yuda Iskariote, ambaye baadaye alimsaliti Yesu.

Yesu Aponya Wengi

17 Akashuka pamoja nao akasimama mahali penye uwanja tambar are. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu waliotoka sehemu zote za Yudea na Yerusalemu na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walikuwa wamekuja kumsiki liza na kuponywa magonjwa yao. 18 Hata wale waliokuwa wakiteswa na pepo wachafu nao walimjia akawaponya. 19 Na watu wote wali kuwa wanajitahidi kumgusa kwa maana walipofanya hivyo, nguvu zil ikuwa zikimtoka na kuwaponya wote.

20 Kisha akawatazama wanafunzi wake akasema, “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini kwa sababu Ufalme wa mbinguni ni wenu! 21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashibishwa! Mmebarikiwa ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka. 22 Mmebari kiwa ninyi watu watakapowachukia na kuwakataa na kuwatukana na kuharibu sifa yenu kwa ajili yangu. 23 Yatakapotokea haya fura hini na kuruka ruka kwa furaha kwa sababu zawadi kubwa imewekwa mbinguni kwa ajili yenu. Hata baba zao waliwatendea manabii wa zamani vivyo hivyo.

24 “Lakini ole wenu ninyi matajiri, kwa sababu mmekwisha pata furaha yenu! Ole wenu ninyi mlioshiba, maana mtaona njaa! 25 Ole wenu ninyi mnaocheka sasa, maana mtalia na kuomboleza! 26 Ole wenu mtakaposifiwa na watu, kwani ndivyo baba zao walivy owasifu manabii wa uongo.”

Wapendeni Adui Zenu

27 “Sikieni niwaambie, wapendeni adui zenu. Watendeeni mema wanaowachukia. 28 Wabarikini wanaowalaani, waombeeni mema wanaowaumiza. 29 Mtu akikupiga kofi, mgeuzie na shavu la pili. Mtu akikunyang’anya koti lako, usimzuie kuchukua na shati lako pia. 30 Aombae mpe, na mtu akichukua mali yako usidai urudishiwe. 31 Watendee wengine unavyopenda nao wakutendee. 32 Je, kuna sifa gani mnapowapenda watu wawapendao? Hata wasiomjua Mungu huwapenda wawapendao. 33 Tena kuna sifa gani mnapowatendea mema wale wanaowatendea mema? Hata wasiomjua Mungu hufanyiana hivyo. 34 Tena mnapowakopesha wale tu ambao mnategemea kuwa watawalipa, kuna sifa gani? Hata watu wasiomjua Mungu huwakopesha wenye dhambi wenzao wakiwa na hakika ya kurudishiwa mali yao yote. 35 Bali, wapendeni adui zenu, watendeeni mema. Wakopesheni bila kutegemea kurudishiwa mlichokopesha. Ndipo mtapata zawadi kubwa nanyi mtakuwa wana wa Mungu Aliye Juu. Yeye ni mwema kwa watu wasio na shukrani na watu waovu. 36 Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.”

Msiwahukumu Wengine

37 “Msiwahukumu wengine nanyi hamtahukumiwa. Msilaani, nanyi hamtalaaniwa. Wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa. 38 Muwe wepesi wa kutoa nanyi mtapokea. Kipimo mtakachotoa mtar udishiwa kikiwa kimejaa na kushindiliwa na kutikiswa na kufurika. Kwa kuwa jinsi mtakavyotoa, ndivyo mtakavyopata.”

Kwa kuwa jinsi mtakavyotoa, ndivyo mtakavyopata.”

39 Pia akawapa mfano akasema, “Je, kipofu anaweza kumwon goza kipofu mwenzake? Si wote wawili watatumbukia shimoni? 40 Mwanafunzi hawezi kuwa mjuzi kuliko mwalimu wake, ila akihi timu, anaweza kuwa bingwa kama mwalimu wake. 41 Mbona unatazama sana kipande kilichoko katika jicho la mwenzako nawe huoni pande lililoko ndani ya jicho lako? 42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu yangu, hebu, nikusaidie kutoa kipande hicho ndani ya jicho lako,’ wakati wewe mwenyewe huoni pande hilo lililoko ndani ya jicho lako? Mnafiki wewe! Ondoa kwanza pande hilo ndani ya jicho lako, na ndipo utakapoweza kuona vizuri na kuondoa kipande kili choko ndani ya jicho la ndugu yako.

43 “Hakuna mti bora uzaao matunda hafifu wala hakuna mti hafifu uzaao matunda bora. 44 Kila mti hutambuliwa kwa matunda yake. Tini hazichumwi kwenye michongoma wala zabibu hazichumwi kwenye majani mwitu. 45 Hali kadhalika mtu mwema hutambulikana kwa matendo yake mazuri yatokayo katika moyo mwema. Mtu mwovu pia hutenda maovu yatokanayo na uovu uliojaa ndani ya moyo wake. Mtu hunena yale yaliyojaa moyoni mwake.

46 “Kwa nini mnaniita, ‘Bwana, Bwana’ nanyi hamfanyi ninay owaambia?

47 Nitawaambieni alivyo mtu anayesikia na kufanya ninay osema. 48 Yeye ni kama mtu aliyejenga nyumba akachimba chini na kujenga msingi kwenye mwamba. Mafuriko yalipotokea, yakaikumba ile nyumba wala haikutikisika, kwani ilikuwa na msingi imara. 49 Lakini yeye ayasikiaye maneno yangu na asiyafuate, ni kama mtu aliyejenga nyumba juu ya mchanga bila kuweka msingi. Mafuriko yalipoikumba nyumba ile, ilianguka mara, na kuporomoka kabisa.”

Jesus Is Lord of the Sabbath(A)

One Sabbath Jesus was going through the grainfields, and his disciples began to pick some heads of grain, rub them in their hands and eat the kernels.(B) Some of the Pharisees asked, “Why are you doing what is unlawful on the Sabbath?”(C)

Jesus answered them, “Have you never read what David did when he and his companions were hungry?(D) He entered the house of God, and taking the consecrated bread, he ate what is lawful only for priests to eat.(E) And he also gave some to his companions.” Then Jesus said to them, “The Son of Man(F) is Lord of the Sabbath.”

On another Sabbath(G) he went into the synagogue and was teaching, and a man was there whose right hand was shriveled. The Pharisees and the teachers of the law were looking for a reason to accuse Jesus, so they watched him closely(H) to see if he would heal on the Sabbath.(I) But Jesus knew what they were thinking(J) and said to the man with the shriveled hand, “Get up and stand in front of everyone.” So he got up and stood there.

Then Jesus said to them, “I ask you, which is lawful on the Sabbath: to do good or to do evil, to save life or to destroy it?”

10 He looked around at them all, and then said to the man, “Stretch out your hand.” He did so, and his hand was completely restored. 11 But the Pharisees and the teachers of the law were furious(K) and began to discuss with one another what they might do to Jesus.

The Twelve Apostles(L)

12 One of those days Jesus went out to a mountainside to pray, and spent the night praying to God.(M) 13 When morning came, he called his disciples to him and chose twelve of them, whom he also designated apostles:(N) 14 Simon (whom he named Peter), his brother Andrew, James, John, Philip, Bartholomew, 15 Matthew,(O) Thomas, James son of Alphaeus, Simon who was called the Zealot, 16 Judas son of James, and Judas Iscariot, who became a traitor.

Blessings and Woes(P)

17 He went down with them and stood on a level place. A large crowd of his disciples was there and a great number of people from all over Judea, from Jerusalem, and from the coastal region around Tyre and Sidon,(Q) 18 who had come to hear him and to be healed of their diseases. Those troubled by impure spirits were cured, 19 and the people all tried to touch him,(R) because power was coming from him and healing them all.(S)

20 Looking at his disciples, he said:

“Blessed are you who are poor,
    for yours is the kingdom of God.(T)
21 Blessed are you who hunger now,
    for you will be satisfied.(U)
Blessed are you who weep now,
    for you will laugh.(V)
22 Blessed are you when people hate you,
    when they exclude you(W) and insult you(X)
    and reject your name as evil,
        because of the Son of Man.(Y)

23 “Rejoice in that day and leap for joy,(Z) because great is your reward in heaven. For that is how their ancestors treated the prophets.(AA)

24 “But woe to you who are rich,(AB)
    for you have already received your comfort.(AC)
25 Woe to you who are well fed now,
    for you will go hungry.(AD)
Woe to you who laugh now,
    for you will mourn and weep.(AE)
26 Woe to you when everyone speaks well of you,
    for that is how their ancestors treated the false prophets.(AF)

Love for Enemies(AG)

27 “But to you who are listening I say: Love your enemies, do good to those who hate you,(AH) 28 bless those who curse you, pray for those who mistreat you.(AI) 29 If someone slaps you on one cheek, turn to them the other also. If someone takes your coat, do not withhold your shirt from them. 30 Give to everyone who asks you, and if anyone takes what belongs to you, do not demand it back.(AJ) 31 Do to others as you would have them do to you.(AK)

32 “If you love those who love you, what credit is that to you?(AL) Even sinners love those who love them. 33 And if you do good to those who are good to you, what credit is that to you? Even sinners do that. 34 And if you lend to those from whom you expect repayment, what credit is that to you?(AM) Even sinners lend to sinners, expecting to be repaid in full. 35 But love your enemies, do good to them,(AN) and lend to them without expecting to get anything back. Then your reward will be great, and you will be children(AO) of the Most High,(AP) because he is kind to the ungrateful and wicked. 36 Be merciful,(AQ) just as your Father(AR) is merciful.

Judging Others(AS)

37 “Do not judge, and you will not be judged.(AT) Do not condemn, and you will not be condemned. Forgive, and you will be forgiven.(AU) 38 Give, and it will be given to you. A good measure, pressed down, shaken together and running over, will be poured into your lap.(AV) For with the measure you use, it will be measured to you.”(AW)

39 He also told them this parable: “Can the blind lead the blind? Will they not both fall into a pit?(AX) 40 The student is not above the teacher, but everyone who is fully trained will be like their teacher.(AY)

41 “Why do you look at the speck of sawdust in your brother’s eye and pay no attention to the plank in your own eye? 42 How can you say to your brother, ‘Brother, let me take the speck out of your eye,’ when you yourself fail to see the plank in your own eye? You hypocrite, first take the plank out of your eye, and then you will see clearly to remove the speck from your brother’s eye.

A Tree and Its Fruit(AZ)

43 “No good tree bears bad fruit, nor does a bad tree bear good fruit. 44 Each tree is recognized by its own fruit.(BA) People do not pick figs from thornbushes, or grapes from briers. 45 A good man brings good things out of the good stored up in his heart, and an evil man brings evil things out of the evil stored up in his heart. For the mouth speaks what the heart is full of.(BB)

The Wise and Foolish Builders(BC)

46 “Why do you call me, ‘Lord, Lord,’(BD) and do not do what I say?(BE) 47 As for everyone who comes to me and hears my words and puts them into practice,(BF) I will show you what they are like. 48 They are like a man building a house, who dug down deep and laid the foundation on rock. When a flood came, the torrent struck that house but could not shake it, because it was well built. 49 But the one who hears my words and does not put them into practice is like a man who built a house on the ground without a foundation. The moment the torrent struck that house, it collapsed and its destruction was complete.”