Font Size
Yohana 13:36-14:1
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yohana 13:36-14:1
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Asema Petro Atamkana
(Mt 26:31-35; Mk 14:27-31; Lk 22:31-34)
36 Simoni Petro akamwuliza Yesu, “Bwana, unaenda wapi?”
Yesu akajibu, “Kule niendako hamwezi kunifuata sasa. Lakini mtanifuata baadaye.”
37 Petro akauliza, “Bwana, kwa nini nisikufuate sasa? Mimi niko radhi kufa kwa ajili yako!”
38 Yesu akajibu, “Je, ni kweli utayatoa maisha yako kwa ajili yangu? Hakika nakwambia, kabla jogoo hajawika, utasema mara tatu kwamba hunijui mimi.”
Yesu Awafariji Wafuasi Wake
14 Yesu akasema, “Msisumbuke. Mwaminini Mungu, na mniamini na mimi.
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
© 2017 Bible League International