Kutoa Kwa Ukarimu

Tunapenda mfahamu ndugu zetu, kuhusu neema ambayo Mungu amewapa makanisa ya Makedonia. Pamoja na majaribu makali na taabu walizopata, furaha yao na umaskini wao mkuu zimezaa utajiri wa ukarimu. Ninashuhudia kwamba walitoa kwa kadiri ya uwezo wao hata na zaidi ya uwezo wao. Kwa hiari yao wenyewe, walitusihi wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu. Na hawakufanya tulivyotazamia bali walijitoa wao wenyewe kwa Bwana kwanza na ndipo wakajitoa kwetu, kufuatana na mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo tulimwagiza Tito, kwa kuwa ndiye aliyeanzisha jambo hili, akamilishe kazi hii ya neema pia kwa upande wenu. Basi, kama mlivyo mbele sana katika yote: katika imani, katika kutamka, katika juhudi na katika kutupenda, hakik isheni kuwa mnakuwa wa kwanza pia katika neema hii ya kutoa.

Siwapi amri, lakini nawaonyesha jinsi wengine walivyo tay ari kutoa ili kupima ukweli wa upendo wenu. Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye ingawa alikuwa tajiri, alikubali kuwa maskini kwa ajili yenu, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri. 10 Ushauri wangu kuhusu jambo hili ni huu. Ni vyema mkamilishe sasa jambo ambalo mlinia na mkaanza kulifanya tangu mwaka jana 11 ili wepesi wenu katika kunia ulin gane na kumaliza kwenu kutoa kwa kadiri ya mlicho nacho. 12 Kwa kuwa kama nia ya kutoa ipo, kitolewacho kinakubalika kufuatana na kile mtu alicho nacho, si kufuatana na kile ambacho mtu hana. 13 Nia yetu si kwamba wengine wasaidike wakati ninyi mnateseka bali pawe na uwiano. 14 Kwa wakati huu wingi wa vitu mlivyonavyo usaidie kutosheleza mahitaji yao, ili wakati wao wakiwa na wingi wa vitu, nao wapate kutosheleza mahitaji yenu. 15 Ndipo patakuwa na usawa, kama maandiko yanavyosema, “Aliyekusanya kwa wingi, hakubakiza kitu, na aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”

Tito Anatumwa Korintho

16 Tunamshukuru Mungu ambaye amempa Tito moyo wa kuwajali ninyi kama mimi ninavyowajali. 17 Si kwamba amekubali ombi letu tu, bali anakuja kwenu akiwa na ari na kwa hiari yake mwenyewe. 18 Pamoja naye tunamtuma ndugu ambaye anasifiwa na makanisa yote kwa huduma yake ya kuhubiri Injili. 19 Zaidi ya hayo, amechagu liwa na makanisa asafiri nasi kupeleka matoleo haya. Hii ni huduma ambayo tunafanya kwa utukufu wa Bwana na pia kuonyesha nia yetu ya kuwasaidia wengine. 20 Tumenuia kwamba mtu ye yote asiwe na sababu ya kutulaumu kuhusu jinsi tunavyosima mia matoleo haya ya ukarimu. 21 Tunajitahidi kuhakikisha kuwa tunafanya haki machoni pa Bwana na machoni penu, na wala si kama sisi tuonavyo vyema. 22 Pamoja na hawa, tunamtuma ndugu yetu ambaye tumempima mara nyingi tukamwona kuwa wa kweli na mwenye juhudi, hasa zaidi sana kwa kuwa ana imani kubwa kwenu. 23 Kumhusu Tito, yeye ni mwenzangu na mfanyakazi pamoja nami kwa ajili yenu. Kuhusu hawa ndugu wengine, wao ni wawakilishi wa makanisa, nao wanamletea Kristo utukufu. 24 Kwa hiyo, waonyesheni hawa ndugu upendo wenu na sababu inayotufanya tujivune kwa ajili yenu, ili makanisa yote yapate kuona.

Wasaidieni Wakristo Wenzenu

Hakuna sababu ya kuwaandikia kuhusu msaada unaotolewa kwa ajili ya watu wa Mungu, kwa kuwa ninajua mlivyo tayari kutoa, nami nimekuwa nikijivuna kwa ajili yenu kwa watu wa Makedonia, nikiwaambia kuwa ninyi wa Akaya mmekuwa tayari kutoa tangu mwaka jana. Ari yenu imewachochea wengi wao kuanza kutoa. Lakini sasa nawatuma hawa ndugu ili kujivuna kwetu kuhusu mchango wenu kusije kukawa ni maneno matupu, bali muwe tayari kama nilivyosema mko tayari. Isije ikawa nitakapokuja na watu wa Makedonia nikute hamko tayari niaibike, na ninyi zaidi, kwa kuwa nilishasema mko tayari. Kwa hivyo niliona ni muhimu niwahimize hawa ndugu watangulie kuja huko kabla yangu, wafanye mipango yote ya matoleo ya zawadi mliyoahidi ili iwe tayari, si kama mchango wa kulazim ishwa bali kama zawadi ya hiari.

Kumbukeni kwamba, mtu anayepanda mbegu chache, atavuna mazao machache; na mtu anayepanda mbegu nyingi atavuna mazao mengi. Kila mtu atoe kama anavyokusudia moyoni mwake, si kwa kusita au kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mtu anayetoa kwa moyo. Na Mungu anaweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili kila wakati muwe na kila kitu kwa kiasi cha kutosha na ziada kwa ajili ya kila kazi njema. Kama Maandiko yanavyosema, “Yeye hutapanya kila mahali kuwapa maskini, haki yake hudumu milele.” 10 Na Mungu ambaye ndiye humpa mkulima mbegu za kupanda, na mkate kwa chakula, atawapa na kuzidisha mbegu mnazohitaji na kuziwezesha kukua zitoe mazao ya matendo mema ya haki. 11 Atawa fanya kuwa matajiri kwa kila hali ili mpate kuwa wakarimu kila wakati na kwa mchango wenu wa hiari kupitia kwetu, wengi wapate kumshukuru Mungu. 12 Huduma hii mnayofanya si kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watu wa Mungu, bali utaleta mbubujiko wa shukrani nyingi kwa Mungu tu. 13 Kwa kutoa kwenu, mtakuwa mnatoa uthibitisho wa uhakika wa imani yenu. Ndipo watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utii wenu unaoambatana na kukiri kwenu kwa Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wa mchango wenu kwao na kwa wen gine wote. 14 Nao watawaombea kwa upendo mwingi kwa ajili ya neema kuu mliyopewa na Mungu. 15 Tumshukuru Mungu kwa ajili ya zawadi hii isiyoelezeka.

Paulo Atetea Huduma Yake

10 Mimi Paulo nawaandikia nikiwasihi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi ambaye ni mpole ninapokuwa pamoja nanyi, lakini mwenye ujasiri nikiwa mbali nanyi! Nawaomba msinifanye niwe mkali nitakapofika kwenu, kama ninavyotarajia kuwa mkali kwa watu fulani, ambao wanadhani kwamba nafuata kawaida za dunia katika mwenendo wangu. Ingawa tunaishi duniani lakini hatupigani kama watu wa ulimwengu. Silaha zetu si za kidunia, bali silaha zetu zina nguvu ya kimungu iwezayo kubomoa ngome. Tunaharibu hoja na mabishano yaliyo kinyume cha kumjua Mungu. Tunateka mawazo yote na kuyafanya yamtii Kristo, na tutakuwa tayari kuadhibu uasi wo wote baada ya kuhakikisha utii wenu. Tazameni vizuri mambo yaliyo mbele ya macho yenu. Kama mtu ye yote anaamini kuwa yeye ni wa Kristo, basi ajiangalie tena, kwa maana na sisi pia ni wa Kristo kama yeye alivyo. Kwa sababu hata kama tunajivunia mno madaraka tuliyo nayo, ambayo Bwana ametupatia kwa ajili ya kuwa jenga na sio kuwagandamiza, sitaona haya kuyatumia. Sitaki ionekane kama nataka kuwatisha kwa barua zangu. 10 Kwa maana wengine wanasema, “Barua zake zina uzito na ni kali lakini mtu mwenyewe ni mdhaifu na kuzungumza kwake hakuvutii.” 11 Watu kama hao wajue ya kuwa, wanavyotuona katika barua tukiwa hatupo nanyi, ndivyo tulivyo, na ndivyo tutakavyofanya tutakapo kuwa pamoja nanyi. 12 Hatuthubutu kujiweka kwenye kundi moja au kujilinganisha na hao wanaojiona kuwa wao ni wa maana sana. Wana pojilinganisha wenyewe kwa wenyewe, wanaonyesha ya kuwa hawana busara. 13 Lakini sisi hatujajivuna kupita kiasi, bali majivuno yetu yatakuwa katika mipaka ambayo Mungu ametuwekea, na mipaka hiyo inawafikia hata na ninyi. 14 Kwa maana hatupiti mipaka tunapowajumlisha katika huduma yetu kwa sababu tulikuwa wa kwanza kuwaletea Injili ya Kristo. 15 Hatupiti mipaka na kujivunia kazi ya watu wengine. Lakini matumaini yetu ni kwamba, imani yenu inavyozidi kukua, huduma yetu kwenu itaendelea kupanuka, 16 ili tuweze kuhubiri Injili hata nchi zilizopakana nanyi, bila kujivu nia kazi iliyokwisha fanywa katika sehemu ya mtu mwingine. 17 “Anayejivuna na ajivune katika Bwana.” 18 Kwa maana sio mtu anayejisifu ambaye anapata kibali, bali ni mtu ambaye Bwana anamsifu.

Kutoa Kwa Ukarimu

Tunapenda mfahamu ndugu zetu, kuhusu neema ambayo Mungu amewapa makanisa ya Makedonia. Pamoja na majaribu makali na taabu walizopata, furaha yao na umaskini wao mkuu zimezaa utajiri wa ukarimu. Ninashuhudia kwamba walitoa kwa kadiri ya uwezo wao hata na zaidi ya uwezo wao. Kwa hiari yao wenyewe, walitusihi wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu. Na hawakufanya tulivyotazamia bali walijitoa wao wenyewe kwa Bwana kwanza na ndipo wakajitoa kwetu, kufuatana na mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo tulimwagiza Tito, kwa kuwa ndiye aliyeanzisha jambo hili, akamilishe kazi hii ya neema pia kwa upande wenu. Basi, kama mlivyo mbele sana katika yote: katika imani, katika kutamka, katika juhudi na katika kutupenda, hakik isheni kuwa mnakuwa wa kwanza pia katika neema hii ya kutoa.

Siwapi amri, lakini nawaonyesha jinsi wengine walivyo tay ari kutoa ili kupima ukweli wa upendo wenu. Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye ingawa alikuwa tajiri, alikubali kuwa maskini kwa ajili yenu, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri. 10 Ushauri wangu kuhusu jambo hili ni huu. Ni vyema mkamilishe sasa jambo ambalo mlinia na mkaanza kulifanya tangu mwaka jana 11 ili wepesi wenu katika kunia ulin gane na kumaliza kwenu kutoa kwa kadiri ya mlicho nacho. 12 Kwa kuwa kama nia ya kutoa ipo, kitolewacho kinakubalika kufuatana na kile mtu alicho nacho, si kufuatana na kile ambacho mtu hana. 13 Nia yetu si kwamba wengine wasaidike wakati ninyi mnateseka bali pawe na uwiano. 14 Kwa wakati huu wingi wa vitu mlivyonavyo usaidie kutosheleza mahitaji yao, ili wakati wao wakiwa na wingi wa vitu, nao wapate kutosheleza mahitaji yenu. 15 Ndipo patakuwa na usawa, kama maandiko yanavyosema, “Aliyekusanya kwa wingi, hakubakiza kitu, na aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”

Tito Anatumwa Korintho

16 Tunamshukuru Mungu ambaye amempa Tito moyo wa kuwajali ninyi kama mimi ninavyowajali. 17 Si kwamba amekubali ombi letu tu, bali anakuja kwenu akiwa na ari na kwa hiari yake mwenyewe. 18 Pamoja naye tunamtuma ndugu ambaye anasifiwa na makanisa yote kwa huduma yake ya kuhubiri Injili. 19 Zaidi ya hayo, amechagu liwa na makanisa asafiri nasi kupeleka matoleo haya. Hii ni huduma ambayo tunafanya kwa utukufu wa Bwana na pia kuonyesha nia yetu ya kuwasaidia wengine. 20 Tumenuia kwamba mtu ye yote asiwe na sababu ya kutulaumu kuhusu jinsi tunavyosima mia matoleo haya ya ukarimu. 21 Tunajitahidi kuhakikisha kuwa tunafanya haki machoni pa Bwana na machoni penu, na wala si kama sisi tuonavyo vyema. 22 Pamoja na hawa, tunamtuma ndugu yetu ambaye tumempima mara nyingi tukamwona kuwa wa kweli na mwenye juhudi, hasa zaidi sana kwa kuwa ana imani kubwa kwenu. 23 Kumhusu Tito, yeye ni mwenzangu na mfanyakazi pamoja nami kwa ajili yenu. Kuhusu hawa ndugu wengine, wao ni wawakilishi wa makanisa, nao wanamletea Kristo utukufu. 24 Kwa hiyo, waonyesheni hawa ndugu upendo wenu na sababu inayotufanya tujivune kwa ajili yenu, ili makanisa yote yapate kuona.

Wasaidieni Wakristo Wenzenu

Hakuna sababu ya kuwaandikia kuhusu msaada unaotolewa kwa ajili ya watu wa Mungu, kwa kuwa ninajua mlivyo tayari kutoa, nami nimekuwa nikijivuna kwa ajili yenu kwa watu wa Makedonia, nikiwaambia kuwa ninyi wa Akaya mmekuwa tayari kutoa tangu mwaka jana. Ari yenu imewachochea wengi wao kuanza kutoa. Lakini sasa nawatuma hawa ndugu ili kujivuna kwetu kuhusu mchango wenu kusije kukawa ni maneno matupu, bali muwe tayari kama nilivyosema mko tayari. Isije ikawa nitakapokuja na watu wa Makedonia nikute hamko tayari niaibike, na ninyi zaidi, kwa kuwa nilishasema mko tayari. Kwa hivyo niliona ni muhimu niwahimize hawa ndugu watangulie kuja huko kabla yangu, wafanye mipango yote ya matoleo ya zawadi mliyoahidi ili iwe tayari, si kama mchango wa kulazim ishwa bali kama zawadi ya hiari.

Kumbukeni kwamba, mtu anayepanda mbegu chache, atavuna mazao machache; na mtu anayepanda mbegu nyingi atavuna mazao mengi. Kila mtu atoe kama anavyokusudia moyoni mwake, si kwa kusita au kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mtu anayetoa kwa moyo. Na Mungu anaweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili kila wakati muwe na kila kitu kwa kiasi cha kutosha na ziada kwa ajili ya kila kazi njema. Kama Maandiko yanavyosema, “Yeye hutapanya kila mahali kuwapa maskini, haki yake hudumu milele.” 10 Na Mungu ambaye ndiye humpa mkulima mbegu za kupanda, na mkate kwa chakula, atawapa na kuzidisha mbegu mnazohitaji na kuziwezesha kukua zitoe mazao ya matendo mema ya haki. 11 Atawa fanya kuwa matajiri kwa kila hali ili mpate kuwa wakarimu kila wakati na kwa mchango wenu wa hiari kupitia kwetu, wengi wapate kumshukuru Mungu. 12 Huduma hii mnayofanya si kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watu wa Mungu, bali utaleta mbubujiko wa shukrani nyingi kwa Mungu tu. 13 Kwa kutoa kwenu, mtakuwa mnatoa uthibitisho wa uhakika wa imani yenu. Ndipo watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utii wenu unaoambatana na kukiri kwenu kwa Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wa mchango wenu kwao na kwa wen gine wote. 14 Nao watawaombea kwa upendo mwingi kwa ajili ya neema kuu mliyopewa na Mungu. 15 Tumshukuru Mungu kwa ajili ya zawadi hii isiyoelezeka.

Paulo Atetea Huduma Yake

10 Mimi Paulo nawaandikia nikiwasihi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi ambaye ni mpole ninapokuwa pamoja nanyi, lakini mwenye ujasiri nikiwa mbali nanyi! Nawaomba msinifanye niwe mkali nitakapofika kwenu, kama ninavyotarajia kuwa mkali kwa watu fulani, ambao wanadhani kwamba nafuata kawaida za dunia katika mwenendo wangu. Ingawa tunaishi duniani lakini hatupigani kama watu wa ulimwengu. Silaha zetu si za kidunia, bali silaha zetu zina nguvu ya kimungu iwezayo kubomoa ngome. Tunaharibu hoja na mabishano yaliyo kinyume cha kumjua Mungu. Tunateka mawazo yote na kuyafanya yamtii Kristo, na tutakuwa tayari kuadhibu uasi wo wote baada ya kuhakikisha utii wenu. Tazameni vizuri mambo yaliyo mbele ya macho yenu. Kama mtu ye yote anaamini kuwa yeye ni wa Kristo, basi ajiangalie tena, kwa maana na sisi pia ni wa Kristo kama yeye alivyo. Kwa sababu hata kama tunajivunia mno madaraka tuliyo nayo, ambayo Bwana ametupatia kwa ajili ya kuwa jenga na sio kuwagandamiza, sitaona haya kuyatumia. Sitaki ionekane kama nataka kuwatisha kwa barua zangu. 10 Kwa maana wengine wanasema, “Barua zake zina uzito na ni kali lakini mtu mwenyewe ni mdhaifu na kuzungumza kwake hakuvutii.” 11 Watu kama hao wajue ya kuwa, wanavyotuona katika barua tukiwa hatupo nanyi, ndivyo tulivyo, na ndivyo tutakavyofanya tutakapo kuwa pamoja nanyi. 12 Hatuthubutu kujiweka kwenye kundi moja au kujilinganisha na hao wanaojiona kuwa wao ni wa maana sana. Wana pojilinganisha wenyewe kwa wenyewe, wanaonyesha ya kuwa hawana busara. 13 Lakini sisi hatujajivuna kupita kiasi, bali majivuno yetu yatakuwa katika mipaka ambayo Mungu ametuwekea, na mipaka hiyo inawafikia hata na ninyi. 14 Kwa maana hatupiti mipaka tunapowajumlisha katika huduma yetu kwa sababu tulikuwa wa kwanza kuwaletea Injili ya Kristo. 15 Hatupiti mipaka na kujivunia kazi ya watu wengine. Lakini matumaini yetu ni kwamba, imani yenu inavyozidi kukua, huduma yetu kwenu itaendelea kupanuka, 16 ili tuweze kuhubiri Injili hata nchi zilizopakana nanyi, bila kujivu nia kazi iliyokwisha fanywa katika sehemu ya mtu mwingine. 17 “Anayejivuna na ajivune katika Bwana.” 18 Kwa maana sio mtu anayejisifu ambaye anapata kibali, bali ni mtu ambaye Bwana anamsifu.