Kutoka kwa Paulo mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu. Kwa Kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watu wote wa Mungu walioko Akaya yote.

Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.

Faraja Katika Mateso

Ashukuriwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja zote. Yeye anatufariji katika mateso yetu yote ili tuweze kuwafariji wale walio katika mateso yo yote, tukitumia faraja ambayo sisi tumepokea kutoka kwa Mungu. Kama vile tunavyoshiriki mateso ya Kristo yaliyo mengi, ndivyo na far aja yetu inavyomiminika kwa wengine. Kama tunateseka ni kwa faraja yenu na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa faraja yenu, ambayo mnapata wakati mkivumilia kwa subira mateso hayo hayo tunayopata sisi. Matumaini yetu kwenu ni imara; kwa maana tunajua ya kuwa kama mnavyoshiriki katika mateso yetu, mtashiriki pia katika faraja yetu.

Hatupendi mkose kujua, ndugu wapendwa, kuhusu mateso tuliy oyapata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo ambayo ilikuwa zaidi ya uwezo wetu kuvumilia, kiasi kwamba tulikata tamaa kwamba tungeishi. Kwa hakika tulijisikia kana kwamba tumehukumiwa kifo. Lakini hii ilitokea ili tusijitegemee wenyewe bali tumtege mee Mungu ambaye anawafufua wafu. 10 Alituokoa katika hatari hiyo ya kifo, na atatuokoa. Tumeweka tumaini letu juu yake kwamba ataendelea kutuokoa. 11 Ninyi pia mtusaidie kwa maombi ili wengi wamshukuru Mungu kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka tulizopokea kama majibu ya maombi ya wengi.

Paulo Abadili Mipango Yake

12 Hii ndio sababu tunajivuna. Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeishi katika ulimwengu, na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, kwa utakatifu na ukweli utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya mwanadamu bali kwa neema ya Mungu. 13 Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma na kuyaelewa. Natumaini mtaelewa kikamilifu, 14 yale ambayo sasa mnayaelewa kwa sehemu, ili siku ile ya Bwana Yesu muweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu.

15 Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilipanga kuwatembelea kwanza ili mpate baraka mara mbili. 16 Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia, na kurudi kwenu tena nikitoka Makedonia ili mnisaidie katika safari yangu ya kwenda Uyahudi. 17 Je, nilikuwa kigeugeu nilipotaka kufanya hivi? Au mimi ninafanya mipango yangu kama watu wa dunia, nikiwa tayari kusema, “Ndiyo” na wakati huo huo kusema, “Hapana”?

18 Lakini kama Mungu alivyo mwaminifu, ahadi yangu haikuwa “Ndiyo” na “Hapana” 19 Kwa kuwa Mwana wa Mungu Yesu Kristo, ambaye tulimhubiri kwenu tukiwa na Silvano, Timotheo, na mimi mwenyewe, hakuwa ‘ndio’ na ‘hapana.’ Katika yeye wakati wote ni ndio. 20 Kwa maana ahadi zote za Mungu ni ‘ndio’ katika Kristo. Ndio sababu tunatamka ‘Amina’ kwa ajili yake, kwa utukufu wa Mungu. 21 Ni Mungu mwenyewe ambaye anatuwezesha sisi na ninyi kusimama imara katika Kristo. Ametuweka wakfu; 22 ametutia mhuri wake juu yetu, akatupa Roho wake mioyoni mwetu kama uthibitisho.

23 Mungu ni shahidi wangu kwamba niliacha kurudi Korintho kwa kuwahurumia. 24 Hatutaki kuwaamrisha kuhusu imani yenu bali tunafanya kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu; kwa maana mnasimama imara kwa imani.

Kwa sababu hiyo, niliamua kwamba sitafanya safari nyingine kuja kuwahuzunisha. Kwa kuwa kama nawahuzunisha, ni nani ali yebaki kunifurahisha isipokuwa ninyi ambao nimewahuzunisha? Ndio sababu nikawaandikia ili nitakapokuja nisihuzunishwe na watu ambao wangenifanya nifurahi. Nilikuwa na uhakika kwenu kwamba furaha yangu ingekuwa furaha yenu nyote. Kwa maana nili waandikia katika dhiki na kutaabika moyoni na kwa machozi mengi. Shabaha yangu haikuwa kuwahuzunisha bali kuwaonyesha kina cha upendo wangu kwenu.

Msamaha Kwa Mwenye Dhambi

Basi ikiwa mtu ye yote amesababisha huzuni, kwa kiasi fulani hakunihuzunisha mimi kama alivyowahuzunisha ninyi nyote; sipendi kuweka uzito zaidi kwa upande wenu. Basi adhabu aliyop ewa na wengi inamtosha. Na sasa mnapaswa kumsamehe na kumfariji ili asikate tamaa kabisa kutokana na huzuni kubwa mno aliyo nayo. Kwa hiyo nawasihi mumhakikishie tena kwamba mnampenda. Nili waandikia kuwajaribu ili nione kama mtakuwa watii kwa kila kitu. 10 Mtu ye yote mnayemsamehe na mimi namsamehe. Cho chote nili chosamehe, kama kulikuwa na cha kusamehe, nimesamehe kwa ajili yenu mbele ya Kristo 11 ili shetani asije akatushinda. Kwa maana tunajua mipango yake.

12 Nilipofika Troa kuhubiri Injili ya Kristo, nilikuta Bwana ameshafungua mlango. 13 Lakini sikuweza kutulia kwa sababu sikumkuta ndugu yangu Tito huko. Kwa hiyo nikaagana nao nikaenda Makedonia.

Ushindi Ndani Ya Kristo

14 Lakini Mungu ashukuriwe, ambaye hutuongoza katika ushindi tukiwa ndani ya Kristo. Naye hututumia sisi kueneza maarifa ya kumjua yeye kila mahali kama harufu nzuri. 15 Kwa Mungu sisi ni kama harufu nzuri ya manukato ya Kristo ambayo inatapakaa mion goni mwa wale wanaookolewa na wale wanaopotea. 16 Kwa wale wanaopotea sisi ni kama harufu ya kifo, lakini kwa wale wanaooko lewa sisi ni harufu iletayo uzima. Ni nani basi awezaye kufanya kazi hiyo? 17 Sisi si kama watu wengine ambao wanauza neno la Mungu wajipatie faida. Lakini kama watu wenye moyo safi, tuliot euliwa na Mungu mbele yake mwenyewe, sisi tunazungumza tukiwa ndani ya Kristo.

Wahudumu Wa Agano Jipya

Je mnadhani tunaanza kujisifu tena? Au tunahitaji kupata barua za utambulisho kwenu au kutoka kwenu, kama watu wengine wafanyavyo? Ninyi wenyewe ni barua yetu ya utambulisho iliyoan dikwa katika mioyo yenu, ijulikane na kusomwa na kila mtu. Ni dhahiri kwamba ninyi ni barua iliyoandikwa na Kristo, matokeo ya kazi yetu. Barua hii haikuandikwa kwa wino bali kwa Roho wa Mungu aliye hai.

Hili ndilo tumaini tulilo nalo kwa Mungu ndani ya Kristo. Haina maana kwamba sisi tunaweza wenyewe kupima cho chote tuna chofanya, lakini uwezo wetu unatoka kwa Mungu. Ni yeye ali yetuwezesha sisi kuwa wahudumu wa agano jipya, ambalo limefanywa, si kwa maandishi, bali kwa Roho. Kwa maana maandishi huleta kifo, lakini Roho huleta Uzima.

Utukufu Wa Agano Jipya

Sasa ikiwa huduma iliyoleta kifo, ambayo iliandikwa kwa herufi juu ya jiwe ilikuja kwa utukufu hata ikawa Waisraeli wal ishindwa kutazama uso wa Musa kwa sababu ya kung’aa kwake, ingawa ulikuwa ukififia, je? Huduma ya Roho haitakuwa na utukufu zaidi? Ikiwa huduma inayowahukumu watu ina utukufu, huduma inayoleta haki si itakuwa na utukufu zaidi? 10 Hakika kwa hali hii, kilichokuwa na utukufu hapo mwanzo, sasa hakina utukufu tena kikilinganishwa na utukufu uliopo. 11 Na kama kilichokuwa kina fifia kilikuja kwa utukufu, utukufu wa kile kinachodumu ni zaidi sana!

12 Kwa hiyo kwa kuwa tunatumaini hili, tuna ujasiri. 13 Sisi si kama Musa, ambaye alifunika uso wake kwa kitambaa ili Waisraeli wasione ule mng’ao ulivyokuwa ukififia na kutoweka. 14 Lakini akili zao zilipumbaa, kwa maana mpaka leo akili zao zinafunikwa na kitambaa wakati agano jipya linaposomwa. Hicho kitambaa hakijaondolewa kwa maana ni Kristo peke yake anayeweza kukiondoa. 15 Hata leo, sheria ya Musa inaposomwa, bado kitambaa kinafunika akili zao. 16 Lakini wakati wo wote mtu anapomgeukia Bwana, “kitambaa kinaondolewa.” 17 Basi, Bwana ni Roho, na mahali alipo Roho wa Bwana pana uhuru. 18 Na sisi sote ambao nyuso zetu hazikufunikwa tunaonyesha, kama kwenye kioo, utukufu wa Bwana. Nasi tunabadilishwa tufanane naye, kutoka utukufu hadi utukufu wa juu zaidi, ambao unatoka kwa Bwana ambaye ni Roho.

Hazina Za Roho Kwenye Vyombo Vya Udongo

Kwa hiyo tukiwa na huduma hii kwa rehema ya Mungu, hatu kati tamaa. Tumekataa njia za siri na za aibu. Hatutumii njia za udanganyifu, wala hatupotoshi neno la Mungu. Badala yake, tunaeleza neno la kweli wazi wazi na kujitambulisha kuwa wa kweli kwa dhamiri ya kila mtu mbele ya Mungu. Na hata kama Injili yetu imefichika, basi imefichika kwa wale wanaopotea. Kwa upande wao, mungu wa dunia hii ametia giza akili za wasioamini, ili wasione mwanga wa Injili ya utukufu wa Kristo, ambaye ana sura ya Mungu. Kwa maana hatujihubiri sisi wenyewe ila tunamhu biri Yesu Kristo kuwa ni Bwana, na sisi ni watumishi wenu kwa ajili ya Yesu. Kwa kuwa ni Mungu aliyesema, “Nuru iangaze katika giza,” ambaye ameangaza mioyoni mwetu kutupatia nuru ya ufahamu wa utukufu wa Mungu ung’aao katika uso wa Kristo.

Hata hivyo tunayo hazina hii katika vyombo vya udongo, ili kuonyesha kwamba uwezo huu wa ajabu unatoka kwa Mungu, na si kutoka kwetu. Tumegandamizwa kila upande, lakini hatujashindwa. Tumetatanishwa lakini hatukati tamaa; tumeteswa lakini hatuku achwa upweke; tumetupwa chini lakini hatujateketezwa. 10 Tuna chukua katika mwili wetu kifo cha Yesu wakati wote ili uhai wa Yesu uweze kudhihirika katika miili yetu. 11 Kwa maana sisi tunaoishi, maisha yetu yako katika hatari ya kifo wakati wote kwa ajili ya Yesu ili uhai wake uweze kuonekana katika miili yetu ya mauti. 12 Kwa hiyo, mauti inatuandama wakati wote, bali uzima unafanya kazi ndani yenu. 13 Maandiko yanasema, “Niliamini, kwa hiyo nimesema.” Sisi pia tunaamini, kwa hiyo tunasema. 14 Kwa maana tunajua ya kuwa aliyemfufua Bwana Yesu atatufufua na sisi pamoja na Yesu na kutufikisha sisi na ninyi mbele zake. 15 Haya yote ni kwa ajili yenu, ili kwa kadiri neema ya Mungu inavyowafi kia watu wengi zaidi, wote watoe shukrani kwa utukufu wa Mungu.

16 Kwa hiyo, hatukati tamaa. Ingawa miili yetu inachakaa, utu wetu wa ndani unafanywa upya kila siku. 17 Maana hii dhiki yetu nyepesi na ya muda mfupi inatutayarisha kwa ajili ya utukufu wa uzima wa milele unaozidi sana matatizo haya. 18 Kwa maana hatuweki mawazo yetu kwenye vitu vinavyoonekana bali kwenye vitu visivyoonekana. Maana vile vinavyoonekana ni vya muda mfupi, lakini vile visivyoonekana vinadumu milele.

Makao Ya Mbinguni

Kwa maana twajua kwamba kama hema hii tunamoishi tukiwa ulimwenguni itaharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba ya milele mbinguni, ambayo haikujengwa kwa mikono ya wanadamu. Maana sasa twaugua, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni, kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena tukiwa uchi. Tukiwa bado tunaishi katika hema hii tunaugua na kulemewa, kwa maana hatutaki kukaa bila nguo bali tunatamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili ile hali ya kufa imezwe na uhai. Mungu ndiye aliyetuandaa kwa shabaha hii, naye ametupa Roho wake kama mdha mana, kutuhakikishia mambo yajayo baadaye. Kwa hiyo wakati wote tuna ujasiri mkuu. Tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na nyumbani kwa Bwana. Tunaishi kwa imani na si kwa kuona. Nasema tuna ujasiri na ingekuwa afadhali kuuacha mwili huu tukaishi nyumbani na Bwana. Kwa hiyo, kama tuko nyumbani katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana. 10 Kwa kuwa sisi sote inatubidi kusimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo. Na kila mmoja atapokea mema au mabaya, kulingana na matendo yake alipokuwa katika mwili.

Huduma Ya Upatanisho

11 Kwa hiyo tukijua umuhimu wa kumcha Bwana tunajaribu kuwa vuta watu. Mungu anatufahamu fika. Tunaamini kwamba dhamiri zenu pia zinatufahamu tulivyo. 12 Hatujaribu kujipendekeza kwenu tena, lakini tunataka kuwapeni nafasi mjisifu juu yetu ili muweze kuwajibu hao wanaojisifia mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni. 13 Kama tumeehuka, ni kwa ajili ya Mungu; lakini kama tuna akili timamu ni kwa faida yenu. 14 Kwa kuwa upendo wa Kristo unatusukuma, tunaamini ya kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote kwa hiyo wote walikufa. 15 Naye alikufa kwa ajili ya watu wote ili wote wanaoishi, wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuka tena kwa ajili yao.

16 Tangu sasa hatumtazami mtu ye yote namna ya kibinadamu, ingawaje hapo mwanzo tulimtazama Kristo kwa namna ya kibinadamu. Hatumtazami hivyo tena. 17 Kwa hiyo mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, mapya yamekuja. 18 Haya yote yanatoka kwa Mungu, ambaye kwa njia ya Yesu Kristo ametupatanisha na mwenyewe, na akatupa huduma ya upatanisho. 19 Ndani ya Kristo Mungu aliupatanisha ulimwengu na yeye mwe nyewe, asiwahesabie watu dhambi zao. Naye ametukabidhi ujumbe huu wa upatanisho.

20 Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, Mungu anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Na sisi tunawasihi ninyi kwa niaba ya Kristo: mpatanishwe na Mungu. 21 Mungu alimfanya yeye ambaye hakujua dhambi, awe dhambi kwa ajili yetu ili ndani yake tupate kuwa haki ya Mungu.

Kama wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msipokee neema ya Mungu bure . Kwa maana Mungu anasema: “Wakati ufaao niliku sikiliza, na siku ya wokovu nilikusaidia. Tazameni, huu ndio wakati ufaao; leo ndio siku ya wokovu.”

Matatizo Ya Paulo

Hatutaki kumwekea mtu ye yote kikwazo ili huduma yetu isionekane kuwa na kasoro. Badala yake, kwa kila njia tunaon yesha ya kuwa sisi ni watumishi wa Mungu kwa kuvumilia: katika taabu, katika misiba, katika shida katika kupigwa, kufungwa gerezani na katika fujo; katika kazi ngumu, kukosa usingizi usiku na katika njaa; katika usafi wa moyo, katika ufahamu, subira na wema; katika Roho Mtakatifu na upendo wa kweli; katika maneno ya kweli na katika uwezo wa Mungu; kwa silaha za haki mkono wa kulia na mkono wa kushoto; katika utukufu na katika aibu, katika sifa na katika lawama; tukiwa wa kweli lakini tukionekana kuwa walaghai; tukiwa maarufu lakini tukihesabiwa kama tusioju likana; tukiwa kama wanaokufa lakini tunaishi; tukiadhibiwa lakini hatuuawi; 10 tukiwa wenye huzuni lakini siku zote tukish angilia; tukionekana maskini lakini tukiwafanya wengi kuwa mata jiri; tukiwa kama wasio na kitu lakini tukiwa na vitu vyote.

11 Tumesema wazi nanyi, ninyi ndugu wa Korintho, na kuweka mioyo yetu wazi kabisa kwenu. 12 Sisi hatujizuii kuwapenda, bali ninyi mmeuzuia upendo wenu usitufikie . 13 Na sasa nasema kama na watoto wangu: ninyi pia fungueni mioyo yenu kabisa kwetu.

Msiambatane Na Wasioamini

14 Msiambatane pamoja na watu wasioamini. Kwa maana kuna uhusiano gani kati ya haki na uovu? Au kuna ushirika gani kati ya nuru na giza? 15 Kuna kuelewana gani kati ya Kristo na shetani? Mwamini ana uhusiano gani na asiyeamini? 16 Kuna uelewano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi ni hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu alivyosema, “Nitaishi ndani yao na kutembea kati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 17 Kwa hiyo, tokeni kati yao, mkajitenge nao, asema Bwana. Msiguse cho chote kisicho safi; ndipo nitawakaribisha kwangu. 18 Nami nitakuwa baba kwenu, nanyi mtakuwa vijana wangu na binti zangu, asema Bwana Mwenyezi.”

Kwa kuwa tumepewa ahadi hizi wapendwa, basi tujitakase kutokana na kila aina ya uchafu wa mwili na roho, na tufanye bidii kufikia ukamilifu kwa kuwa tunamcha Mungu.

Furaha Ya Paulo

Tupokeeni kwa moyo mweupe. Hatujamkosea mtu ye yote, hatu jampotosha mtu ye yote, wala hatujamdhulumu mtu ye yote. Sisemi haya ili kuwahukumu; kwa kuwa, kama nilivyosema mwanzo, tunawath amini kiasi ambacho mpo mioyoni mwetu wakati wote, ikiwa ni kufa pamoja au kuishi pamoja. Ninayo imani kubwa kwenu; ninawaonea fahari kubwa. Nimefarijika sana. Pamoja na taabu zetu zote, furaha yangu haina mfano.

Kwa maana hata tulipofika Makedonia, miili yetu haikuwa na amani. Tulitaabishwa kila upande, kwa nje kulikuwa na upinzani na mioyoni mwetu tulikuwa na hofu. Bali Mungu, ambaye hufariji wenye huzuni, alitufariji kwa kumleta Tito; na si kwa kuwa Tito alifika tu, bali pia kwa kuwa ninyi mlimfariji. Alitueleza juu ya upendo wenu, huzuni yenu na jinsi mlivyonihurumia, kwa hiyo furaha yangu iliongezeka sana.

Hata kama barua yangu iliwasikitisha, sasa sijuti kwamba niliiandika ingawa nilikuwa nimejuta. Naona barua yangu iliwahu zunisha, lakini kwa muda mfupi. Lakini sasa ninafurahi, si kwa kuwa mlihuzunika, bali kwa kuwa huzuni hiyo iliwafanya mtubu. Kwa maana mlihuzunika kama Mungu anavyopenda watu wahuzunike na hivyo hatukuwadhuru kwa njia yo yote. 10 Kwa maana huzuni ikitumiwa na Mungu huwafanya watu watubu dhambi zao wapate kuokolewa; nao wanakuwa hawana majuto. Lakini huzuni ya kidunia husababisha kifo. 11 Tazameni faida mlizopata kutokana na huzuni hii: bidii mliyo nayo; juhudi mliyofanya kujitetea, uchungu wenu, hofu yenu, upendo wenu, shauku yenu, na jinsi mlivyokuwa tayari kutoa adhabu inayostahili. Kwa kila njia mmethibitisha kuwa hamna hatia katika jambo hilo. 12 Kwa hiyo ingawa niliwaandikia, haikuwa kwa sababu ya huyo aliyekosa au huyo aliyekosewa. Lakini nilitaka ninyi wenyewe muone, mbele za Mungu, jinsi mnavyotupenda kwa moyo wote. 13 Kwa hiyo tumefarijika. Pamoja na faraja tuliyopata, tumefu rahi zaidi kwa kuona jinsi Tito alivyofurahi kwa kuwa mlimwondo lea wasi wasi aliokuwa nao. 14 Nilikuwa nimejisifu kwake juu yenu nanyi hamkuniaibisha. Kama jinsi yale niliyowaambia yalivy okuwa ya kweli, hali kadhalika kujisifu kwetu kwa Tito kuwahusu ninyi kumeonekana kuwa kweli pia. 15 Upendo wake kwenu unaongezeka sana anapokumbuka jinsi mlivyokuwa watii na jinsi mlivyompokea kwa hofu na kutetemeka. 16 Nafurahi kwa sababu nina imani nanyi kabisa.

Kutoa Kwa Ukarimu

Tunapenda mfahamu ndugu zetu, kuhusu neema ambayo Mungu amewapa makanisa ya Makedonia. Pamoja na majaribu makali na taabu walizopata, furaha yao na umaskini wao mkuu zimezaa utajiri wa ukarimu. Ninashuhudia kwamba walitoa kwa kadiri ya uwezo wao hata na zaidi ya uwezo wao. Kwa hiari yao wenyewe, walitusihi wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu. Na hawakufanya tulivyotazamia bali walijitoa wao wenyewe kwa Bwana kwanza na ndipo wakajitoa kwetu, kufuatana na mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo tulimwagiza Tito, kwa kuwa ndiye aliyeanzisha jambo hili, akamilishe kazi hii ya neema pia kwa upande wenu. Basi, kama mlivyo mbele sana katika yote: katika imani, katika kutamka, katika juhudi na katika kutupenda, hakik isheni kuwa mnakuwa wa kwanza pia katika neema hii ya kutoa.

Siwapi amri, lakini nawaonyesha jinsi wengine walivyo tay ari kutoa ili kupima ukweli wa upendo wenu. Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye ingawa alikuwa tajiri, alikubali kuwa maskini kwa ajili yenu, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri. 10 Ushauri wangu kuhusu jambo hili ni huu. Ni vyema mkamilishe sasa jambo ambalo mlinia na mkaanza kulifanya tangu mwaka jana 11 ili wepesi wenu katika kunia ulin gane na kumaliza kwenu kutoa kwa kadiri ya mlicho nacho. 12 Kwa kuwa kama nia ya kutoa ipo, kitolewacho kinakubalika kufuatana na kile mtu alicho nacho, si kufuatana na kile ambacho mtu hana. 13 Nia yetu si kwamba wengine wasaidike wakati ninyi mnateseka bali pawe na uwiano. 14 Kwa wakati huu wingi wa vitu mlivyonavyo usaidie kutosheleza mahitaji yao, ili wakati wao wakiwa na wingi wa vitu, nao wapate kutosheleza mahitaji yenu. 15 Ndipo patakuwa na usawa, kama maandiko yanavyosema, “Aliyekusanya kwa wingi, hakubakiza kitu, na aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”

Tito Anatumwa Korintho

16 Tunamshukuru Mungu ambaye amempa Tito moyo wa kuwajali ninyi kama mimi ninavyowajali. 17 Si kwamba amekubali ombi letu tu, bali anakuja kwenu akiwa na ari na kwa hiari yake mwenyewe. 18 Pamoja naye tunamtuma ndugu ambaye anasifiwa na makanisa yote kwa huduma yake ya kuhubiri Injili. 19 Zaidi ya hayo, amechagu liwa na makanisa asafiri nasi kupeleka matoleo haya. Hii ni huduma ambayo tunafanya kwa utukufu wa Bwana na pia kuonyesha nia yetu ya kuwasaidia wengine. 20 Tumenuia kwamba mtu ye yote asiwe na sababu ya kutulaumu kuhusu jinsi tunavyosima mia matoleo haya ya ukarimu. 21 Tunajitahidi kuhakikisha kuwa tunafanya haki machoni pa Bwana na machoni penu, na wala si kama sisi tuonavyo vyema. 22 Pamoja na hawa, tunamtuma ndugu yetu ambaye tumempima mara nyingi tukamwona kuwa wa kweli na mwenye juhudi, hasa zaidi sana kwa kuwa ana imani kubwa kwenu. 23 Kumhusu Tito, yeye ni mwenzangu na mfanyakazi pamoja nami kwa ajili yenu. Kuhusu hawa ndugu wengine, wao ni wawakilishi wa makanisa, nao wanamletea Kristo utukufu. 24 Kwa hiyo, waonyesheni hawa ndugu upendo wenu na sababu inayotufanya tujivune kwa ajili yenu, ili makanisa yote yapate kuona.

Wasaidieni Wakristo Wenzenu

Hakuna sababu ya kuwaandikia kuhusu msaada unaotolewa kwa ajili ya watu wa Mungu, kwa kuwa ninajua mlivyo tayari kutoa, nami nimekuwa nikijivuna kwa ajili yenu kwa watu wa Makedonia, nikiwaambia kuwa ninyi wa Akaya mmekuwa tayari kutoa tangu mwaka jana. Ari yenu imewachochea wengi wao kuanza kutoa. Lakini sasa nawatuma hawa ndugu ili kujivuna kwetu kuhusu mchango wenu kusije kukawa ni maneno matupu, bali muwe tayari kama nilivyosema mko tayari. Isije ikawa nitakapokuja na watu wa Makedonia nikute hamko tayari niaibike, na ninyi zaidi, kwa kuwa nilishasema mko tayari. Kwa hivyo niliona ni muhimu niwahimize hawa ndugu watangulie kuja huko kabla yangu, wafanye mipango yote ya matoleo ya zawadi mliyoahidi ili iwe tayari, si kama mchango wa kulazim ishwa bali kama zawadi ya hiari.

Kumbukeni kwamba, mtu anayepanda mbegu chache, atavuna mazao machache; na mtu anayepanda mbegu nyingi atavuna mazao mengi. Kila mtu atoe kama anavyokusudia moyoni mwake, si kwa kusita au kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mtu anayetoa kwa moyo. Na Mungu anaweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili kila wakati muwe na kila kitu kwa kiasi cha kutosha na ziada kwa ajili ya kila kazi njema. Kama Maandiko yanavyosema, “Yeye hutapanya kila mahali kuwapa maskini, haki yake hudumu milele.” 10 Na Mungu ambaye ndiye humpa mkulima mbegu za kupanda, na mkate kwa chakula, atawapa na kuzidisha mbegu mnazohitaji na kuziwezesha kukua zitoe mazao ya matendo mema ya haki. 11 Atawa fanya kuwa matajiri kwa kila hali ili mpate kuwa wakarimu kila wakati na kwa mchango wenu wa hiari kupitia kwetu, wengi wapate kumshukuru Mungu. 12 Huduma hii mnayofanya si kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watu wa Mungu, bali utaleta mbubujiko wa shukrani nyingi kwa Mungu tu. 13 Kwa kutoa kwenu, mtakuwa mnatoa uthibitisho wa uhakika wa imani yenu. Ndipo watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utii wenu unaoambatana na kukiri kwenu kwa Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wa mchango wenu kwao na kwa wen gine wote. 14 Nao watawaombea kwa upendo mwingi kwa ajili ya neema kuu mliyopewa na Mungu. 15 Tumshukuru Mungu kwa ajili ya zawadi hii isiyoelezeka.