Kutoka kwa Paulo mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu. Kwa Kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watu wote wa Mungu walioko Akaya yote.

Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.

Faraja Katika Mateso

Ashukuriwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja zote. Yeye anatufariji katika mateso yetu yote ili tuweze kuwafariji wale walio katika mateso yo yote, tukitumia faraja ambayo sisi tumepokea kutoka kwa Mungu. Kama vile tunavyoshiriki mateso ya Kristo yaliyo mengi, ndivyo na far aja yetu inavyomiminika kwa wengine. Kama tunateseka ni kwa faraja yenu na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa faraja yenu, ambayo mnapata wakati mkivumilia kwa subira mateso hayo hayo tunayopata sisi. Matumaini yetu kwenu ni imara; kwa maana tunajua ya kuwa kama mnavyoshiriki katika mateso yetu, mtashiriki pia katika faraja yetu.

Hatupendi mkose kujua, ndugu wapendwa, kuhusu mateso tuliy oyapata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo ambayo ilikuwa zaidi ya uwezo wetu kuvumilia, kiasi kwamba tulikata tamaa kwamba tungeishi. Kwa hakika tulijisikia kana kwamba tumehukumiwa kifo. Lakini hii ilitokea ili tusijitegemee wenyewe bali tumtege mee Mungu ambaye anawafufua wafu. 10 Alituokoa katika hatari hiyo ya kifo, na atatuokoa. Tumeweka tumaini letu juu yake kwamba ataendelea kutuokoa. 11 Ninyi pia mtusaidie kwa maombi ili wengi wamshukuru Mungu kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka tulizopokea kama majibu ya maombi ya wengi.

Paulo Abadili Mipango Yake

12 Hii ndio sababu tunajivuna. Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeishi katika ulimwengu, na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, kwa utakatifu na ukweli utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya mwanadamu bali kwa neema ya Mungu. 13 Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma na kuyaelewa. Natumaini mtaelewa kikamilifu, 14 yale ambayo sasa mnayaelewa kwa sehemu, ili siku ile ya Bwana Yesu muweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu.

15 Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilipanga kuwatembelea kwanza ili mpate baraka mara mbili. 16 Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia, na kurudi kwenu tena nikitoka Makedonia ili mnisaidie katika safari yangu ya kwenda Uyahudi. 17 Je, nilikuwa kigeugeu nilipotaka kufanya hivi? Au mimi ninafanya mipango yangu kama watu wa dunia, nikiwa tayari kusema, “Ndiyo” na wakati huo huo kusema, “Hapana”?

18 Lakini kama Mungu alivyo mwaminifu, ahadi yangu haikuwa “Ndiyo” na “Hapana” 19 Kwa kuwa Mwana wa Mungu Yesu Kristo, ambaye tulimhubiri kwenu tukiwa na Silvano, Timotheo, na mimi mwenyewe, hakuwa ‘ndio’ na ‘hapana.’ Katika yeye wakati wote ni ndio. 20 Kwa maana ahadi zote za Mungu ni ‘ndio’ katika Kristo. Ndio sababu tunatamka ‘Amina’ kwa ajili yake, kwa utukufu wa Mungu. 21 Ni Mungu mwenyewe ambaye anatuwezesha sisi na ninyi kusimama imara katika Kristo. Ametuweka wakfu; 22 ametutia mhuri wake juu yetu, akatupa Roho wake mioyoni mwetu kama uthibitisho.

23 Mungu ni shahidi wangu kwamba niliacha kurudi Korintho kwa kuwahurumia. 24 Hatutaki kuwaamrisha kuhusu imani yenu bali tunafanya kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu; kwa maana mnasimama imara kwa imani.