2 Timotheo 3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Watu Wengi Wataacha Kumpenda Mungu
3 Kumbuka hili: Katika siku za mwisho nyakati ngumu zitakuja. 2 Watu watajipenda wenyewe na kupenda fedha. Watakuwa na majivuno na wenye jeuri. Watawatukana wengine kwa matusi. Hawatawatii wazazi wao. Watakuwa wasio na shukrani. Watapinga kila kinachompendeza Mungu. 3 Hawatakuwa na upendo kwa wengine na hawatakubali kuwasamehe wengine. Watawasingizia wengine na hawataweza kujizuia. Watakuwa wakatili na watayachukia yaliyo mema. 4 Watu watawasaliti rafiki zao. Watafanya mambo ya kipuuzi bila kufikiri na watajisifu wenyewe. Badala ya kumpenda Mungu watapenda starehe. 5 Watajifanya kuwa wanamheshimu Mungu, lakini watazikana nguvu za uzima ambazo ndizo zinazotuwezesha kwa hakika kumpa utukufu na kumpendeza. Ukae mbali na watu wa jinsi hiyo.
6 Nasema hivi kwa sababu baadhi yao wanaziendea nyumba na kuwateka wanawake dhaifu, waliolemewa na dhambi na kuvutwa na kila aina ya tamaa. 7 Wanawake hawa nyakati zote wanataka kujifunza, lakini hawawezi kamwe kuufikia ufahamu wote wa kweli. 8 Kama ambavyo Yane na Yambre[a] walivyompinga Musa, ndivyo hata watu hawa wanavyoipinga kweli. Ni watu ambao akili zao zimeharibika, nao wameshindwa kuifuata imani. 9 Lakini hawataendelea mbele zaidi, kwa sababu upumbavu wao utadhihirika wazi wazi kwa watu wote, kama ujinga wa Yane na Yambre ulivyojulikana.
Maelekezo ya Mwisho
10 Ninyi hata hivyo mmeyazingatia na kuyashika mafundisho yangu, mwenendo wangu na kusudi langu katika maisha, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu na ustahimilivu wangu, 11 mateso yangu na taabu zangu. Mnayajua mambo yaliyonitokea kule Antiokia, Ikonia, na Listra, mateso ya kutisha niliyoyastahimili! Lakini Bwana akaniokoa kutoka katika hayo yote. 12 Kwa hakika wote wanaoishi maisha yenye kumtukuza Mungu kama wafuasi wa Kristo Yesu watasumbuliwa. 13 Lakini watu waovu na wanaodanganya wengine wataendelea kuwa wabaya zaidi. Watawadaganya wengine na wao pia watajidanganya wenyewe.
14 Lakini imekupasa wewe kuendelea kuyashika mambo yale uliyojifunza na kuyathibitisha moyoni mwako kuwa ni ya kweli. Wewe unawajua na unawaamini wale waliokufundisha. 15 Na unajua kwamba umeyajua Maandiko Matakatifu tangu ukiwa mtoto. Maandiko hayo yana uwezo wa kukupa hekima. Hekima hiyo itakuongoza hadi kwenye wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. 16 Maandiko yote tumepewa na Mungu. Na maandiko yote yanafaa kwa mafundisho kwa kusudi la kuwaonesha watu makosa yao na kuwafundisha njia sahihi ya kuishi 17 ili mtu anayemtumikia Mungu aweze kuandaliwa na kukamilishwa kwa ajili ya kufanya kila kazi njema.
Footnotes
- 3:8 Yane na Yambre Huenda walikuwa wale waganga waliompinga Musa katika baraza la Farao. Tazama Kut 7:11-12,22.
2 Timothy 3
King James Version
3 This know also, that in the last days perilous times shall come.
2 For men shall be lovers of their own selves, covetous, boasters, proud, blasphemers, disobedient to parents, unthankful, unholy,
3 Without natural affection, trucebreakers, false accusers, incontinent, fierce, despisers of those that are good,
4 Traitors, heady, highminded, lovers of pleasures more than lovers of God;
5 Having a form of godliness, but denying the power thereof: from such turn away.
6 For of this sort are they which creep into houses, and lead captive silly women laden with sins, led away with divers lusts,
7 Ever learning, and never able to come to the knowledge of the truth.
8 Now as Jannes and Jambres withstood Moses, so do these also resist the truth: men of corrupt minds, reprobate concerning the faith.
9 But they shall proceed no further: for their folly shall be manifest unto all men, as their's also was.
10 But thou hast fully known my doctrine, manner of life, purpose, faith, longsuffering, charity, patience,
11 Persecutions, afflictions, which came unto me at Antioch, at Iconium, at Lystra; what persecutions I endured: but out of them all the Lord delivered me.
12 Yea, and all that will live godly in Christ Jesus shall suffer persecution.
13 But evil men and seducers shall wax worse and worse, deceiving, and being deceived.
14 But continue thou in the things which thou hast learned and hast been assured of, knowing of whom thou hast learned them;
15 And that from a child thou hast known the holy scriptures, which are able to make thee wise unto salvation through faith which is in Christ Jesus.
16 All scripture is given by inspiration of God, and is profitable for doctrine, for reproof, for correction, for instruction in righteousness:
17 That the man of God may be perfect, thoroughly furnished unto all good works.
2 Timothy 3
New International Version
3 But mark this: There will be terrible times in the last days.(A) 2 People will be lovers of themselves, lovers of money,(B) boastful, proud,(C) abusive,(D) disobedient to their parents,(E) ungrateful, unholy, 3 without love, unforgiving, slanderous, without self-control, brutal, not lovers of the good, 4 treacherous,(F) rash, conceited,(G) lovers of pleasure rather than lovers of God— 5 having a form of godliness(H) but denying its power. Have nothing to do with such people.(I)
6 They are the kind who worm their way(J) into homes and gain control over gullible women, who are loaded down with sins and are swayed by all kinds of evil desires, 7 always learning but never able to come to a knowledge of the truth.(K) 8 Just as Jannes and Jambres opposed Moses,(L) so also these teachers oppose(M) the truth. They are men of depraved minds,(N) who, as far as the faith is concerned, are rejected. 9 But they will not get very far because, as in the case of those men,(O) their folly will be clear to everyone.
A Final Charge to Timothy
10 You, however, know all about my teaching,(P) my way of life, my purpose, faith, patience, love, endurance, 11 persecutions, sufferings—what kinds of things happened to me in Antioch,(Q) Iconium(R) and Lystra,(S) the persecutions I endured.(T) Yet the Lord rescued(U) me from all of them.(V) 12 In fact, everyone who wants to live a godly life in Christ Jesus will be persecuted,(W) 13 while evildoers and impostors will go from bad to worse,(X) deceiving and being deceived.(Y) 14 But as for you, continue in what you have learned and have become convinced of, because you know those from whom you learned it,(Z) 15 and how from infancy(AA) you have known the Holy Scriptures,(AB) which are able to make you wise(AC) for salvation through faith in Christ Jesus. 16 All Scripture is God-breathed(AD) and is useful for teaching,(AE) rebuking, correcting and training in righteousness,(AF) 17 so that the servant of God[a](AG) may be thoroughly equipped for every good work.(AH)
Footnotes
- 2 Timothy 3:17 Or that you, a man of God,
© 2017 Bible League International
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.
