17 Mafundisho yao yataendelea kuenea kama donda ndugu. Kati yao wamo Himenayo na Fileto 18 ambao wametanga tanga na kuiacha kweli wakisema kwamba ufufuo umekwishapita. Wanapotosha imani ya baadhi ya watu. 19 Lakini msingi thabiti wa Mungu umesimama imara ukiwa na muhuri wenye maneno haya: “Bwana anawajua walio wake,” na tena, “Kila anayelitaja jina la Bwana aache uovu.”

Read full chapter