Add parallel Print Page Options

13 Kama hatutakuwa waaminifu,
    yeye anabaki kuwa mwaminifu,
    kwa sababu hawezi kujikana mwenyewe.

Mtendakazi Ampendezaye Mungu

14 Endelea kuwakumbusha watu juu ya mambo haya. Waonye kwa mamlaka mbele za Mungu wasipigane juu ya maneno. Mapigano hayo hayana mambo mazuri, bali huwaharibu wanaoyasikiliza. 15 Jitahidi kujionesha mwenyewe kuwa umekubaliwa na Mungu, kama mtumishi asiye na kitu cho chote cha kumfadhaisha na anayeufanyia kazi ujumbe wa kweli ya Mungu katika njia sahihi.

Read full chapter