2 Timoteo 3
La Nuova Diodati
3 Or sappi questo: che negli ultimi giorni verranno tempi difficili,
2 perché gli uomini saranno amanti di se stessi, avidi di denaro, vanagloriosi superbi, bestemmiatori, disubbidienti ai genitori, ingrati, scellerati,
3 senza affetto, implacabili, calunniatori, intemperanti, crudeli, senza amore per il bene,
4 traditori, temerari, orgogliosi, amanti dei piaceri invece che amanti di Dio,
5 aventi l'apparenza della pietà, ma avendone rinnegato la potenza; da costoro allontanati.
6 Nel numero di questi infatti vi sono quelli che s'introducono nelle case e seducono donnicciole cariche di peccati, dominate da varie passioni,
7 le quali imparano sempre, ma senza mai pervenire ad una piena conoscenza della verità.
8 Ora come Ianne e Iambre, si opposero a Mosé, cosí anche costoro si oppongono alla verità; uomini corrotti di mente e riprovati quanto alla fede.
9 Costoro però non andranno molto avanti, perché la loro stoltezza sarà manifestata a tutti, come avvenne anche per quella di quei tali.
10 Ma tu hai seguito da vicino il mio ammaestramento, la mia condotta, i miei consigli, la mia fede, la mia pazienza, il mio amore, la mia perseveranza,
11 le mie persecuzioni, le mie sofferenze, che mi sono accadute ad Antiochia, a Iconio e a Listra, tu sai quali persecuzioni ho sostenuto, ma il Signore mi ha liberato da tutte.
12 Infatti tutti quelli che vogliono vivere piamente in Cristo Gesú saranno perseguitati,
13 ma i malvagi e gli imbroglioni andranno di male in peggio, seducendo ed essendo sedotti.
14 Tu però persevera nelle cose che hai imparato e nelle quali sei stato confermato, sapendo da chi le hai imparate,
15 e che sin da bambino hai conosciuto le sacre Scritture, le quali ti possono rendere savio a salvezza, per mezzo della fede che è in Cristo Gesú.
16 Tutta la Scrittura è divinamente ispirata e utile a insegnare, a convincere, a correggere e a istruire nella giustizia,
17 affinché l'uomo di Dio sia completo, pienamente fornito per ogni buona opera.
2 Timotheo 3
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Watu Wengi Wataacha Kumpenda Mungu
3 Kumbuka hili: Katika siku za mwisho nyakati ngumu zitakuja. 2 Watu watajipenda wenyewe na kupenda fedha. Watakuwa na majivuno na wenye jeuri. Watawatukana wengine kwa matusi. Hawatawatii wazazi wao. Watakuwa wasio na shukrani. Watapinga kila kinachompendeza Mungu. 3 Hawatakuwa na upendo kwa wengine na hawatakubali kuwasamehe wengine. Watawasingizia wengine na hawataweza kujizuia. Watakuwa wakatili na watayachukia yaliyo mema. 4 Watu watawasaliti rafiki zao. Watafanya mambo ya kipuuzi bila kufikiri na watajisifu wenyewe. Badala ya kumpenda Mungu watapenda starehe. 5 Watajifanya kuwa wanamheshimu Mungu, lakini watazikana nguvu za uzima ambazo ndizo zinazotuwezesha kwa hakika kumpa utukufu na kumpendeza. Ukae mbali na watu wa jinsi hiyo.
6 Nasema hivi kwa sababu baadhi yao wanaziendea nyumba na kuwateka wanawake dhaifu, waliolemewa na dhambi na kuvutwa na kila aina ya tamaa. 7 Wanawake hawa nyakati zote wanataka kujifunza, lakini hawawezi kamwe kuufikia ufahamu wote wa kweli. 8 Kama ambavyo Yane na Yambre[a] walivyompinga Musa, ndivyo hata watu hawa wanavyoipinga kweli. Ni watu ambao akili zao zimeharibika, nao wameshindwa kuifuata imani. 9 Lakini hawataendelea mbele zaidi, kwa sababu upumbavu wao utadhihirika wazi wazi kwa watu wote, kama ujinga wa Yane na Yambre ulivyojulikana.
Maelekezo ya Mwisho
10 Ninyi hata hivyo mmeyazingatia na kuyashika mafundisho yangu, mwenendo wangu na kusudi langu katika maisha, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu na ustahimilivu wangu, 11 mateso yangu na taabu zangu. Mnayajua mambo yaliyonitokea kule Antiokia, Ikonia, na Listra, mateso ya kutisha niliyoyastahimili! Lakini Bwana akaniokoa kutoka katika hayo yote. 12 Kwa hakika wote wanaoishi maisha yenye kumtukuza Mungu kama wafuasi wa Kristo Yesu watasumbuliwa. 13 Lakini watu waovu na wanaodanganya wengine wataendelea kuwa wabaya zaidi. Watawadaganya wengine na wao pia watajidanganya wenyewe.
14 Lakini imekupasa wewe kuendelea kuyashika mambo yale uliyojifunza na kuyathibitisha moyoni mwako kuwa ni ya kweli. Wewe unawajua na unawaamini wale waliokufundisha. 15 Na unajua kwamba umeyajua Maandiko Matakatifu tangu ukiwa mtoto. Maandiko hayo yana uwezo wa kukupa hekima. Hekima hiyo itakuongoza hadi kwenye wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. 16 Maandiko yote tumepewa na Mungu. Na maandiko yote yanafaa kwa mafundisho kwa kusudi la kuwaonesha watu makosa yao na kuwafundisha njia sahihi ya kuishi 17 ili mtu anayemtumikia Mungu aweze kuandaliwa na kukamilishwa kwa ajili ya kufanya kila kazi njema.
Footnotes
- 3:8 Yane na Yambre Huenda walikuwa wale waganga waliompinga Musa katika baraza la Farao. Tazama Kut 7:11-12,22.
Copyright © 1991 by La Buona Novella s.c.r.l.
© 2017 Bible League International