Kutoka kwa Paulo mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu. Kwa Kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watu wote wa Mungu walioko Akaya yote.

Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.

Faraja Katika Mateso

Ashukuriwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja zote. Yeye anatufariji katika mateso yetu yote ili tuweze kuwafariji wale walio katika mateso yo yote, tukitumia faraja ambayo sisi tumepokea kutoka kwa Mungu. Kama vile tunavyoshiriki mateso ya Kristo yaliyo mengi, ndivyo na far aja yetu inavyomiminika kwa wengine. Kama tunateseka ni kwa faraja yenu na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa faraja yenu, ambayo mnapata wakati mkivumilia kwa subira mateso hayo hayo tunayopata sisi. Matumaini yetu kwenu ni imara; kwa maana tunajua ya kuwa kama mnavyoshiriki katika mateso yetu, mtashiriki pia katika faraja yetu.

Hatupendi mkose kujua, ndugu wapendwa, kuhusu mateso tuliy oyapata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo ambayo ilikuwa zaidi ya uwezo wetu kuvumilia, kiasi kwamba tulikata tamaa kwamba tungeishi. Kwa hakika tulijisikia kana kwamba tumehukumiwa kifo. Lakini hii ilitokea ili tusijitegemee wenyewe bali tumtege mee Mungu ambaye anawafufua wafu. 10 Alituokoa katika hatari hiyo ya kifo, na atatuokoa. Tumeweka tumaini letu juu yake kwamba ataendelea kutuokoa. 11 Ninyi pia mtusaidie kwa maombi ili wengi wamshukuru Mungu kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka tulizopokea kama majibu ya maombi ya wengi.

Paulo Abadili Mipango Yake

12 Hii ndio sababu tunajivuna. Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeishi katika ulimwengu, na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, kwa utakatifu na ukweli utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya mwanadamu bali kwa neema ya Mungu. 13 Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma na kuyaelewa. Natumaini mtaelewa kikamilifu, 14 yale ambayo sasa mnayaelewa kwa sehemu, ili siku ile ya Bwana Yesu muweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu.

15 Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilipanga kuwatembelea kwanza ili mpate baraka mara mbili. 16 Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia, na kurudi kwenu tena nikitoka Makedonia ili mnisaidie katika safari yangu ya kwenda Uyahudi. 17 Je, nilikuwa kigeugeu nilipotaka kufanya hivi? Au mimi ninafanya mipango yangu kama watu wa dunia, nikiwa tayari kusema, “Ndiyo” na wakati huo huo kusema, “Hapana”?

18 Lakini kama Mungu alivyo mwaminifu, ahadi yangu haikuwa “Ndiyo” na “Hapana” 19 Kwa kuwa Mwana wa Mungu Yesu Kristo, ambaye tulimhubiri kwenu tukiwa na Silvano, Timotheo, na mimi mwenyewe, hakuwa ‘ndio’ na ‘hapana.’ Katika yeye wakati wote ni ndio. 20 Kwa maana ahadi zote za Mungu ni ‘ndio’ katika Kristo. Ndio sababu tunatamka ‘Amina’ kwa ajili yake, kwa utukufu wa Mungu. 21 Ni Mungu mwenyewe ambaye anatuwezesha sisi na ninyi kusimama imara katika Kristo. Ametuweka wakfu; 22 ametutia mhuri wake juu yetu, akatupa Roho wake mioyoni mwetu kama uthibitisho.

23 Mungu ni shahidi wangu kwamba niliacha kurudi Korintho kwa kuwahurumia. 24 Hatutaki kuwaamrisha kuhusu imani yenu bali tunafanya kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu; kwa maana mnasimama imara kwa imani.

Paul, an apostle(A) of Christ Jesus by the will of God,(B) and Timothy(C) our brother,

To the church of God(D) in Corinth,(E) together with all his holy people throughout Achaia:(F)

Grace and peace to you from God our Father and the Lord Jesus Christ.(G)

Praise to the God of All Comfort

Praise be to the God and Father of our Lord Jesus Christ,(H) the Father of compassion and the God of all comfort, who comforts us(I) in all our troubles, so that we can comfort those in any trouble with the comfort we ourselves receive from God. For just as we share abundantly in the sufferings of Christ,(J) so also our comfort abounds through Christ. If we are distressed, it is for your comfort and salvation;(K) if we are comforted, it is for your comfort, which produces in you patient endurance of the same sufferings we suffer. And our hope for you is firm, because we know that just as you share in our sufferings,(L) so also you share in our comfort.

We do not want you to be uninformed,(M) brothers and sisters,[a] about the troubles we experienced(N) in the province of Asia.(O) We were under great pressure, far beyond our ability to endure, so that we despaired of life itself. Indeed, we felt we had received the sentence of death. But this happened that we might not rely on ourselves but on God,(P) who raises the dead.(Q) 10 He has delivered us from such a deadly peril,(R) and he will deliver us again. On him we have set our hope(S) that he will continue to deliver us, 11 as you help us by your prayers.(T) Then many will give thanks(U) on our behalf for the gracious favor granted us in answer to the prayers of many.

Paul’s Change of Plans

12 Now this is our boast: Our conscience(V) testifies that we have conducted ourselves in the world, and especially in our relations with you, with integrity[b](W) and godly sincerity.(X) We have done so, relying not on worldly wisdom(Y) but on God’s grace. 13 For we do not write you anything you cannot read or understand. And I hope that, 14 as you have understood us in part, you will come to understand fully that you can boast of us just as we will boast of you in the day of the Lord Jesus.(Z)

15 Because I was confident of this, I wanted to visit you(AA) first so that you might benefit twice.(AB) 16 I wanted to visit you on my way(AC) to Macedonia(AD) and to come back to you from Macedonia, and then to have you send me on my way(AE) to Judea.(AF) 17 Was I fickle when I intended to do this? Or do I make my plans in a worldly manner(AG) so that in the same breath I say both “Yes, yes” and “No, no”?

18 But as surely as God is faithful,(AH) our message to you is not “Yes” and “No.” 19 For the Son of God,(AI) Jesus Christ, who was preached among you by us—by me and Silas[c](AJ) and Timothy(AK)—was not “Yes” and “No,” but in him it has always(AL) been “Yes.” 20 For no matter how many promises(AM) God has made, they are “Yes” in Christ. And so through him the “Amen”(AN) is spoken by us to the glory of God.(AO) 21 Now it is God who makes both us and you stand firm(AP) in Christ. He anointed(AQ) us, 22 set his seal(AR) of ownership on us, and put his Spirit in our hearts as a deposit, guaranteeing what is to come.(AS)

23 I call God as my witness(AT)—and I stake my life on it—that it was in order to spare you(AU) that I did not return to Corinth. 24 Not that we lord it over(AV) your faith, but we work with you for your joy, because it is by faith you stand firm.(AW)

Footnotes

  1. 2 Corinthians 1:8 The Greek word for brothers and sisters (adelphoi) refers here to believers, both men and women, as part of God’s family; also in 8:1; 13:11.
  2. 2 Corinthians 1:12 Many manuscripts holiness
  3. 2 Corinthians 1:19 Greek Silvanus, a variant of Silas