Askari Mwaminifu Wa Kristo Yesu

Basi, wewe mwanangu, uwe imara katika neema iliyomo ndani ya Kristo Yesu. Na mambo ambayo ulinisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu ambao wataweza kuwa fundisha watu wengine pia. Vumilia mateso pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu. Hakuna askari ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kiraia kwa sababu nia yake ni kumrid hisha yule aliyemwandika kuwa askari. Hali kadhalika mwanar iadha hawezi kupewa tuzo kama hakufuata masharti. Mkulima mwe nye bidii ndiye anayestahili kupata fungu la kwanza la mavuno. Yatafakari haya ninayokuambia, kwa maana Mungu atakupa ufahamu katika mambo yote.

Mkumbuke Yesu Kristo aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, aliyez aliwa katika ukoo wa Daudi. Hii ndio Injili yangu ninayoihubiri. Nami ninateseka kwa sababu ya Injili hii nikivaa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halikufungwa minyororo. 10 Kwa hiyo ninavumilia taabu zote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi na wao pia wapokee wokovu uliomo ndani ya Kristo Yesu pamoja na utukufu wake wa milele.

11 Neno hili ni kweli kabisa: kwamba kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia. 12 Kama tukivumilia, tutatawala pamoja naye pia; kama tukimkana, naye pia atatukana. 13 Tusipo kuwa waaminifu, yeye huendelea kuwa mwaminifu kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.

Mfanyakazi Mwenye Kibali Mbele Za Mungu

14 Wakumbushe mambo haya na uwaamuru mbele za Bwana waache kubishana juu ya maneno. Hii haiwasaidii cho chote bali huwaanga miza wanaowasikiliza. 15 Jitahidi kujidhihirisha mbele za Mungu kama mtu aliyepata kibali chake, mfanyakazi asiyekuwa na sababu yo yote ya kuona aibu, ambaye hulitumia neno la kweli kwa usa hihi. 16 Jiepushe na maneno ya kipuuzi, yasiyo ya kimungu, kwa maana hayo huwavuta watu mbali na Mungu zaidi na zaidi. 17 Mafundisho yao yataendelea kuenea kama donda ndugu. Kati yao wamo Himenayo na Fileto 18 ambao wametanga tanga na kuiacha kweli wakisema kwamba ufufuo umekwishapita. Wanapotosha imani ya baadhi ya watu. 19 Lakini msingi thabiti wa Mungu umesimama imara ukiwa na muhuri wenye maneno haya: “Bwana anawajua walio wake,” na tena, “Kila anayelitaja jina la Bwana aache uovu.”

20 Katika nyumba ya kifahari kuna vyombo vya dhahabu na fedha na pia vimo vyombo vya mbao na vya udongo. Baadhi ya vyombo ni vya heshima lakini vingine sio. 21 Kama mtu akijitakasa na kujitenga na visivyo vya heshima atakuwa chombo cha kutumika kwa shughuli za kifahari; chombo kilichotakaswa kimfaacho Bwana wa nyumba, ambacho ni tayari kwa matumizi yote yaliyo mema. 22 Basi, kimbia tamaa za ujana, na utafute kupata haki, imani, upendo na amani pamoja na wote wamwitao Bwana kwa moyo safi.

23 Usijishughulishe na mabishano yasiyo na maana na ya kipumbavu kwa kuwa unajua ya kwamba hayo huleta ugomvi. 24 Na tena mtumishi wa Bwana hapaswi kuwa mgomvi. Anapaswa kuwa mpole kwa kila mtu na mwalimu mwenye uwezo, na mvumilivu. 25 Anapaswa kuwaonya wale wanaompinga kwa upole, kwa matumaini kwamba Mungu anaweza kuwajalia watubu na kuifahamu kweli; 26 fahamu zao ziwarudie tena, watoke katika mtego wa shetani ambaye amewafunga wafanye kama apendavyo.

The Appeal Renewed

You then, my son,(A) be strong(B) in the grace that is in Christ Jesus. And the things you have heard me say(C) in the presence of many witnesses(D) entrust to reliable people who will also be qualified to teach others. Join with me in suffering,(E) like a good soldier(F) of Christ Jesus. No one serving as a soldier gets entangled in civilian affairs, but rather tries to please his commanding officer. Similarly, anyone who competes as an athlete does not receive the victor’s crown(G) except by competing according to the rules. The hardworking farmer should be the first to receive a share of the crops.(H) Reflect on what I am saying, for the Lord will give you insight into all this.

Remember Jesus Christ, raised from the dead,(I) descended from David.(J) This is my gospel,(K) for which I am suffering(L) even to the point of being chained(M) like a criminal. But God’s word(N) is not chained. 10 Therefore I endure everything(O) for the sake of the elect,(P) that they too may obtain the salvation(Q) that is in Christ Jesus, with eternal glory.(R)

11 Here is a trustworthy saying:(S)

If we died with him,
    we will also live with him;(T)
12 if we endure,
    we will also reign with him.(U)
If we disown him,
    he will also disown us;(V)
13 if we are faithless,
    he remains faithful,(W)
    for he cannot disown himself.

Dealing With False Teachers

14 Keep reminding God’s people of these things. Warn them before God against quarreling about words;(X) it is of no value, and only ruins those who listen. 15 Do your best to present yourself to God as one approved, a worker who does not need to be ashamed and who correctly handles the word of truth.(Y) 16 Avoid godless chatter,(Z) because those who indulge in it will become more and more ungodly. 17 Their teaching will spread like gangrene. Among them are Hymenaeus(AA) and Philetus, 18 who have departed from the truth. They say that the resurrection has already taken place,(AB) and they destroy the faith of some.(AC) 19 Nevertheless, God’s solid foundation stands firm,(AD) sealed with this inscription: “The Lord knows those who are his,”(AE) and, “Everyone who confesses the name of the Lord(AF) must turn away from wickedness.”

20 In a large house there are articles not only of gold and silver, but also of wood and clay; some are for special purposes and some for common use.(AG) 21 Those who cleanse themselves from the latter will be instruments for special purposes, made holy, useful to the Master and prepared to do any good work.(AH)

22 Flee the evil desires of youth and pursue righteousness, faith, love(AI) and peace, along with those who call on the Lord(AJ) out of a pure heart.(AK) 23 Don’t have anything to do with foolish and stupid arguments, because you know they produce quarrels.(AL) 24 And the Lord’s servant must not be quarrelsome but must be kind to everyone, able to teach, not resentful.(AM) 25 Opponents must be gently instructed, in the hope that God will grant them repentance leading them to a knowledge of the truth,(AN) 26 and that they will come to their senses and escape from the trap of the devil,(AO) who has taken them captive to do his will.