1 Wakorintho 2
Neno: Bibilia Takatifu
Ujumbe Wa Msalaba
2 Nilipokuja kwenu ndugu zangu, sikuja kuhubiri siri ya mpango wa Mungu kwa kutumia ufasaha wa kuzungumza au hekima ya binadamu.
2 Kwa kuwa niliamua kwamba wakati nikiwa nanyi nitasahau kila kitu isipokuwa Yesu Kristo; Kristo aliyesulubiwa msalabani. 3 Nilikuja kwenu nikiwa mdhaifu, mwenye woga na nikitetemeka sana. 4 Kuhubiri kwangu na ujumbe wangu haukuwa na hekima na maneno ya kuwashawishi watu, bali ujumbe wangu ulidhihirisha wazi nguvu za Roho, 5 ili imani yenu isiwe imejengwa katika hekima ya wanadamu bali ijengwe katika nguvu ya Mungu.
Hekima Ya Mungu
6 Lakini miongoni mwa watu waliokua kiroho, tunafundisha maneno ya hekima, hii si hekima ya ulimwengu huu au ya watawala wa nyakati hizi ambao watatoweka. 7 Hekima tunayofundisha ni hekima ya siri ya Mungu ambayo imefichwa kwa wanadamu, na ambayo Mungu aliipanga kabla ulimwengu kuwepo, kwa ajili ya utukufu wetu. 8 Watawala wa nyakati zetu hawakuielewa hekima hii. Kwa maana kama wangeliijua, wasingalimsulubisha Bwana wa Utukufu.
9 Lakini, kama Maandiko yasemavyo, “Hakuna aliyeona, hakuna aliyesikia, hakuna aliyewaza, kile ambacho Mungu amekiandaa kwa ajili ya watu wampendao.” 10 Lakini Mungu amekidhihirisha kwetu kwa njia ya Roho wake. Roho huchunguza kila kitu, hata mambo ya ndani ya Mungu. 11 Kwa maana ni nani anajua mawazo ya mtu isipo kuwa roho aliye ndani ya huyo mtu? Vivyo hivyo hakuna mtu anayeelewa mawazo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu. 12 Sisi hat ukupokea roho ya dunia hii bali Roho aliyetoka kwa Mungu ili tuweze kuelewa yale ambayo Mungu ametupatia bure. 13 Haya ndio tunayozungumzia, lakini si kwa maneno tuliyofundishwa na hekima ya wanadamu bali kwa maneno tuliyofundishwa na Roho, nasi tunafa fanua mambo ya kiroho kwa watu wa kiroho. 14 Mtu ambaye hana Roho wa Mungu hawezi kupokea mambo yanayotoka kwa Roho wa Mungu kwa sababu mambo hayo ni upuuzi kwake; na hawezi kuyaelewa kwa kuwa hayo yanaeleweka tu kwa msaada wa Roho.
15 Mtu wa kiroho anao uwezo wa kupima kila kitu, lakini yeye hapimwi na mtu. 16 “Kwa maana ni nani amefahamu mawazo ya Bwana ili apate kumshauri?” Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.
1 Corinthians 2
New International Version
2 And so it was with me, brothers and sisters. When I came to you, I did not come with eloquence or human wisdom(A) as I proclaimed to you the testimony about God.[a] 2 For I resolved to know nothing while I was with you except Jesus Christ and him crucified.(B) 3 I came to you(C) in weakness(D) with great fear and trembling.(E) 4 My message and my preaching were not with wise and persuasive words,(F) but with a demonstration of the Spirit’s power,(G) 5 so that your faith might not rest on human wisdom, but on God’s power.(H)
God’s Wisdom Revealed by the Spirit
6 We do, however, speak a message of wisdom among the mature,(I) but not the wisdom of this age(J) or of the rulers of this age, who are coming to nothing.(K) 7 No, we declare God’s wisdom, a mystery(L) that has been hidden(M) and that God destined for our glory before time began. 8 None of the rulers of this age(N) understood it, for if they had, they would not have crucified the Lord of glory.(O) 9 However, as it is written:
“What no eye has seen,
what no ear has heard,
and what no human mind has conceived”[b]—
the things God has prepared for those who love him—(P)
10 these are the things God has revealed(Q) to us by his Spirit.(R)
The Spirit searches all things, even the deep things of God. 11 For who knows a person’s thoughts(S) except their own spirit(T) within them? In the same way no one knows the thoughts of God except the Spirit of God. 12 What we have received is not the spirit(U) of the world,(V) but the Spirit who is from God, so that we may understand what God has freely given us. 13 This is what we speak, not in words taught us by human wisdom(W) but in words taught by the Spirit, explaining spiritual realities with Spirit-taught words.[c] 14 The person without the Spirit does not accept the things that come from the Spirit of God(X) but considers them foolishness,(Y) and cannot understand them because they are discerned only through the Spirit. 15 The person with the Spirit(Z) makes judgments about all things, but such a person is not subject to merely human judgments, 16 for,
But we have the mind of Christ.(AB)
Footnotes
- 1 Corinthians 2:1 Some manuscripts proclaimed to you God’s mystery
- 1 Corinthians 2:9 Isaiah 64:4
- 1 Corinthians 2:13 Or Spirit, interpreting spiritual truths to those who are spiritual
- 1 Corinthians 2:16 Isaiah 40:13
Copyright © 1989 by Biblica
Holy Bible, New International Version®, NIV® Copyright ©1973, 1978, 1984, 2011 by Biblica, Inc.® Used by permission. All rights reserved worldwide.
NIV Reverse Interlinear Bible: English to Hebrew and English to Greek. Copyright © 2019 by Zondervan.