17 Uwaagize matajiri wa ulimwengu huu waache kujivuna, wala wasiweke matumaini yao katika mali ambayo haina hakika. Bali wam tumaini Mungu ambaye hutupatia vitu vyote kwa wingi ili tuvifu rahie. 18 Waambie watende wema, wawe matajiri katika matendo mema, wawe wakarimu na tayari kushiriki mali zao na wengine. 19 Kwa njia hii watajiwekea msingi imara kwa wakati ujao na hivyo watajipatia uzima ambao ni uzima kweli.

Read full chapter