Viongozi Katika Kanisa

Neno hili ni kweli, kwamba mtu akitaka kuwa askofu, anata mani kazi njema. Basi, askofu awe mtu asiye na lawama. Awe mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtaratibu, mkarimu na aju aye kufundisha. Asiwe mlevi, wala mgomvi bali awe mpole; asiwe mbishi wala mtu apendaye fedha. Aweze kuisimamia nyumba yake vizuri akiwafanya watoto wake kuwa wanyenyekevu na wenye heshima katika hali zote. Kwa maana kama mtu hawezi kuitawala nyumba yake mwenyewe atawezaje kuliangalia kanisa la Mungu? Asiwe mtu aliyeongoka karibuni asije akajiona na kuhukumiwa kama shetani alivyohukumiwa. Kadhalika, awe mwenye sifa njema kati ya watu wa nje ya kanisa, asije akalaumiwa na kuanguka katika mtego wa shetani.

Wasaidizi Katika Kanisa

Vivyo hivyo mashemasi wawe wenye kuheshimika, si wenye kauli mbili au wanywaji mno wa divai au wenye tamaa ya fedha. Wanapaswa kuizingatia ile siri ya imani kwa dhamiri safi. 10 Ni lazima wapimwe kwanza na wakionekana kuwa wanafaa basi waruhusiwe kutoa huduma ya ushemasi. 11 Hali kadhalika, wake zao wawe wenye kuheshimika, si wasengenyaji bali wenye kiasi na waaminifu katika mambo yote. 12 Shemasi awe mume wa mke mmoja; na aweze kuwatawala watoto wake na jamaa yake vema. 13 Watu wanaotoa huduma njema ya ushemasi hujipatia heshima kubwa na uha kika mkubwa katika imani yao kwa Kristo Yesu.

14 Ninakuandikia mambo haya sasa ingawa natarajia kuwepo pamoja nawe karibuni, 15 ili kama nikicheleweshwa, upate kujua jinsi watu wanavyopaswa kuenenda katika nyumba ya Mungu, ambayo ni kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli. 16 Bila shaka yo yote, siri ya dini yetu ni kuu: Alidhihirishwa katika mwili wa kibinadamu, alithibitishwa katika Roho, alionwa na mal aika, alihubiriwa kati ya mataifa, akaaminiwa ulimwenguni, aka chukuliwa juu katika utukufu.

Maagizo Kwa Timotheo

Roho anasema wazi wazi kwamba katika siku za mwisho watu wengine wataiacha imani yao na kusikiliza roho za udanganyifu na mafundisho ya mashetani. Mafundisho hayo yanaletwa na wanafiki waongo ambao dhamiri zao zimekufa kama vile zimechomwa kwa chuma cha moto. Wao wanawazuia watu kuoa; na wanawaamrisha watu wasile vyakula vya aina fulani - ambavyo Mungu aliviumba vipoke lewe kwa shukrani na wale wanaoamini na waliopata kuijua kweli. Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema wala kitu cho chote kisikataliwe kama kinapokelewa kwa shukrani, maana kina takaswa kwa neno la Mungu na kwa sala.

Mtumishi Mwema Wa Kristo

Ukiwapa ndugu mafundisho haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu ambaye amelishwa vema kwa maneno ya imani na yale mafundisho mema uliyoyafuata. Usijishughulishe kabisa na hadithi zisizo za kidini ambazo hazina maana. Jizoeze kuishi kwa kumcha Mungu. Maana japokuwa mazoezi ya mwili yana faida kiasi, kumcha Mungu kuna faida kwa kila hali, kwa sababu kumcha Mungu kuna faida kwa maisha ya sasa na maisha yajayo.

Neno hili ni la kweli na linastahili kupokelewa, 10 na kwa ajili yake sisi tunajitahidi na kutaabika, kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.

11 Agiza na kufundisha mambo haya. 12 Mtu asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe mfano mwema kwa waamini wote kwa maneno yako, kwa mwenendo wako, katika upendo, imani na usafi.

13 Mpaka hapo nitakapokuja, tumia wakati wako katika kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri, na kufundisha. 14 Usiache kutumia kipawa ulichonacho, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee wa kanisa walipokuwekea mikono. 15 Tekeleza mambo haya. Tumia nguvu zako na wakati wako kuyatimiza ili watu wote waone maendeleo yako.

16 Jilinde sana, na utunze mafundisho yako. Yashikilie, maana kwa kufanya hivyo utajiokoa wewe mwenyewe na wale wanaoku sikiliza.

Maagizo Kuhusu Wajane, Wazee Na Watumwa

Usimkemee mzee bali umwonye kama baba yako. Vijana uwaten dee kama ndugu zako. Uwaheshimu mama wazee kama mama zako na akina mama vijana kama dada zako , kwa usafi wote.

Waheshimu Wajane walioachwa pekee, ipasavyo. Kama mjane ana watoto ama wajukuu, hao watimize wajibu wao wa kidini kwa familia, kwa kuwahudumia wazazi na hivyo wawarudishie wema wal iowatendea. Kwa kufanya hivyo watampendeza Mungu. Mwanamke ambaye kweli ni mjane na ameachwa peke yake, anamwekea Mungu tumaini lake naye huendelea kusali na kuomba usiku na mchana. Lakini mwanamke aishie kwa anasa, amekufa, ingawa anaishi. Wape maagizo haya, ili wasiwe na lawama. Kama mtu hatunzi jamaa yake, hasa wale waliomo nyumbani mwake, ameikana imani yake, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

Mjane ye yote ambaye hajafikia umri wa miaka sitini na ambaye alikuwa mwaminifu kwa mumewe, asiwekwe kwenye orodha ya wajane. Mjane anayestahili kuwekwa kwenye orodha hiyo lazima pia 10 awe mwenye sifa ya matendo mema, aliyewalea watoto wake vizuri, aliyekuwa mkarimu, aliyewaosha miguu watu wa Mungu, ali yewasaidia watu wenye taabu na aliyejitolea kufanya mema kwa kila njia. 11 Lakini wajane vijana usiwaweke kwenye orodha hiyo, maana tamaa zao za kimaumbile zikizidi kule kujitoa kwao kwa Kristo, watataka kuolewa tena. 12 Na kwa njia hiyo watajiletea hukumu kwa kuivunja ahadi yao ya mwanzo. 13 Isitoshe, wajane kama hao wana tabia ya uvivu wakizurura nyumba kwa nyumba. Tena hawawi wavivu tu, bali pia huwa wasengenyaji, wajiingizao katika mambo yasiyowahusu na kusema mambo wasiyopaswa kusema.

Kwa hiyo napenda wajane vijana waolewe, wazae watoto na watunze nyumba zao, ili yule adui asipate nafasi ya kusema uovu juu yetu. 15 Kwa maana wajane wengine wamekwisha kupotoka na kumfuata she tani.

16 Lakini kama mama mwamini anao ndugu ambao ni wajane, basi awatunze mwenyewe, kanisa lisibebe mzigo huo, ili liweze kuwat unza wale wajane ambao hawana msaada.

Wazee

17 Wazee wa kanisa wanaoongoza shughuli za kanisa vema wanastahili heshima mara mbili, hasa wale ambao kazi yao ni kuhu biri na kufundisha. 18 Maana Maandiko husema, “Ng’ombe apurapo nafaka usimfunge kinywa,” na tena, “Mfanyakazi anastahili msha hara wake.” 19 Usikubali kusikiliza mashtaka juu ya mzee wa kanisa kama hayakuletwa na mashahidi wawili au watatu. 20 Wale wanaoendelea kutenda dhambi uwaonye hadharani kusudi wengine wapate kuogopa.

21 Ninakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu na mbele ya malaika wateule, tekeleza maagizo haya pasipo kubagua wala upendeleo. 22 Usiwe na haraka kumwekea mtu mikono wala usishiriki katika dhambi za mtu mwingine, jiweke katika hali ya usafi.

23 Usiendelee kunywa maji tu bali tumia divai kidogo kwa ajili ya tumbo lako na maumivu yako ya mara kwa mara.

24 Dhambi za watu wengine ni dhahiri nazo zinatangulia huku muni mbele yao. Lakini dhambi za watu wengine huonekana baadaye. 25 Hali kadhalika matendo mema ni dhahiri na hata kama si dha hiri hayawezi kuendelea kufichika.

Watumwa

Watumwa wote wawahesabu mabwana zao kuwa wanastahili hesh ima zote, ili watu wasije wakalitukana jina la Mungu pamoja na mafundisho yetu. Watumwa ambao mabwana zao ni waamini, wasikose kuwaheshimu kwa kuwa ni ndugu; bali watumike kwa ubora zaidi kwa sababu wale wanaonufaika kwa huduma yao ni waamini na ni wapendwa.

Fundisha na kuhimiza mambo haya. Mtu ye yote akifundisha kinyume cha haya na asikubaliane na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo, na mafundisho yanayo ambatana na kumcha Mungu, huyo amejaa majivuno na wala hafahamu cho chote. Mtu kama huyo ana uchu wa ubishi na mashindano ya maneno ambayo huleta wivu, ugomvi, matukano, shuku mbaya, na ugomvi wa mara kwa mara kati ya watu wenye mawazo maovu, ambao hawanayo ile kweli, na ambao hudhani kwamba kumcha Mungu ni njia ya kuchuma fedha.

Bali kumcha Mungu na kuridhika ni faida kubwa. Kwa maana hatukuja na kitu cho chote hapa duniani, wala hatuwezi kutoka na kitu. Lakini kama tuna chakula na mavazi, basi tutaridhika. Watu wanaotamani kuwa matajiri huanguka katika majaribu na mtego na katika tamaa nyingi mbaya na za kijinga, ambazo huwato komeza wanadamu katika upotevu na maangamizi. 10 Maana kupenda fedha ni chanzo cha uovu wote. Tamaa ya fedha imewafanya wengine watangetange mbali na imani na kuteseka kwa huzuni nyingi.