Mwasherati Atengwe

Kuna habari thabiti kwamba miongoni mwenu kuna uasherati unaotendeka; tena ni uasherati wa aina ambayo hata watu wasiomjua Mungu hawafanyi. Nimesikia kwamba kuna mtu anazini na mama yake wa kambo! Mnawezaje basi kujivuna! Badala yake mngepaswa kuom boleza. Huyo aliyefanya tendo hili afukuzwe na kutengwa nanyi. Japokuwa sipo nanyi katika mwili, lakini nipo nanyi katika roho. Na nimekwisha toa hukumu kuhusu huyo mtu aliyetenda jambo hili, kama vile ningekuwapo. Mnapokutana katika jina la Bwana wetu Yesu nami nikiwepo katika roho, na nguvu ya Bwana wetu Yesu ikiwepo, mtoeni mtu huyu kwa shetani, ili asili yake ya dhambi iangamizwe lakini roho yake iokolewe siku ile ya Bwana.

Kiburi chenu hakifai. Hamjui kwamba hamira kidogo tu huumua donge lote la unga? Ondoeni chachu ya zamani ili mpate kuwa donge lisilo na chachu, kama mnavyotakiwa kuwa. Kwa maana Kristo ambaye ndiye Mwana-kondoo wetu wa Pasaka amekwisha tolewa kama dhabihu. Kwa hiyo, tusherehekee sikukuu hii, sio kwa chachu ya zamani, chachu ya nia mbaya na uovu bali kwa mkate usiotiwa hamira, wa moyo safi na kweli.

Niliwaandikia katika barua yangu kuwa msishirikiane na waasherati. 10 Sikuwa na maana kwamba msishirikiane na watu wa dunia walio waasherati, au wenye tamaa mbaya, wanyang’anyi au waabudu sanamu. Kufanya hivyo ingewabidi mtoke duniani. 11 Lakini nilikuwa namaanisha kwamba msishirikiane na mtu ye yote anayejiita ndugu lakini ni mwasherati, mwenye tamaa mbaya, mwabudu sanamu, mtukanaji, mlevi na laghai. Wala msile na mtu kama huyo.

12 Si kazi yangu kuhukumu watu walio nje ya kanisa. Je, si hao walio ndani ya kanisa mnaopaswa kuwahukumu? 13 Mungu anawa hukumu walio nje ya kanisa. “Mfukuzeni mtu mwovu atoke kutoka katika ushirika wenu.”

Msiwaruhusu Watu Wenu Waishi Katika Dhambi

Sitaki kuyaamini yale ninayosikia, ya kwamba kuna uzinzi katikati yenu. Na ni aina mbaya ya uzinzi ambayo hata wasiomwamini Mungu wetu hawauruhusu. Watu wanasema kuwa huko kwenu kuna mtu anayetenda dhambi ya zinaa na mke wa baba yake. Na mna kiburi! Mngepaswa kuwa na huzuni badala yake. Na mtu aliyetenda dhambi hiyo ilipaswa kuwa amefukuzwa kutoka katika kundi lenu. Siwezi kuwa hapo pamoja nanyi ana kwa ana, lakini niko pamoja nanyi katika roho. Na nimekwisha mhukumu mtu aliyetenda hii kama ambavyo ningemhukumu ikiwa ningekuwa hapo. Nanyi pia mnapaswa kufanya vivyo hivyo. Kusanyikeni pamoja katika jina la Bwana wetu Yesu. Nitakuwa pamoja nanyi katika roho, na nguvu ya Bwana Yesu itakuwa pamoja nanyi. Mtoeni mtu huyu kwa Shetani ili tabia yake ya kujisifu[a] iangamizwe lakini mtu mwenyewe na kanisa, lilojazwa Roho, liweze kuokolewa siku Bwana atakaporudi.

Kujisifu kwenu si kuzuri. Mnajua msemo unaosema, “Chachu kidogo huchahua donge zima.” Ondoeni chachu ya zamani ili muwe donge jipya. Ninyi kwa hakika ni mkate usio na chachu, mkate wa Pasaka,[b] Ndiyo, Kristo aliye Mwanakondoo wetu wa Pasaka[c] amekwisha usawa. Hivyo na tuule mlo wetu wa Pasaka, lakini si pamoja na mkate wenye chachu ya zamani, yaani dhambi na matendo mabaya. Lakini tule mkate usio na chachu. Huu ni mkate wenye ukweli na chachu njema.

Katika barua yangu niliwaandikia kuwa msishirikiane na wazinzi. 10 Lakini sikuwa na maana ya watu wa ulimwengu huu. La sivyo ingewalazimu kuhama katika ulimwengu huu ili mweze kujitenga na wazinzi au walio walafi na waongo, au wale wanaoabudu sanamu. 11 Nilikuwa na maana kuwa msishirikiane na mtu yeyote yule anayedai kuwa anaamini lakini anaendelea kuishi katika dhambi. Usimkaribishe nyumbani kwa chakula kaka ama dada aliye mzinzi, mlafi, anayeabudu sanamu, mtukanaji, mlevi au mwongo.[d]

12-13 Si kazi yangu kuwahukumu wasio sehemu ya kundi la waamini. Mungu atawahukumu, lakini ni lazima mwahukumu wale walio katika kundi lenu. Maandiko yanasema, “Mwondoe mwovu katika kundi lako.”(A)

Footnotes

  1. 5:5 tabia yake ya kujisifu Kwa maana ya kawaida, “Mwili wa dhambi”, ama “damu na nyama”.
  2. 5:7 mkate wa Pasaka Mkate maalum usio na chachu (chachu) ambao Wayahudi walikula katika mlo wa Pasaka. Paulo anamaanisha kuwa waamini hawana dhambi, kama ambavyo mkate wa Pasaka haukuwa na chachu.
  3. 5:7 Mwanakondoo wetu wa Pasaka Yesu alikuwa sadaka kwa ajili ya watu wake, kama mwanakondoo aliyechinjwa kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka ya Kiyahudi.
  4. 5:11 mwongo Kulaghai watu ili kuwaibia.

Dealing With a Case of Incest

It is actually reported that there is sexual immorality among you, and of a kind that even pagans do not tolerate: A man is sleeping with his father’s wife.(A) And you are proud! Shouldn’t you rather have gone into mourning(B) and have put out of your fellowship(C) the man who has been doing this? For my part, even though I am not physically present, I am with you in spirit.(D) As one who is present with you in this way, I have already passed judgment in the name of our Lord Jesus(E) on the one who has been doing this. So when you are assembled and I am with you in spirit, and the power of our Lord Jesus is present, hand this man over(F) to Satan(G) for the destruction of the flesh,[a][b] so that his spirit may be saved on the day of the Lord.(H)

Your boasting is not good.(I) Don’t you know that a little yeast(J) leavens the whole batch of dough?(K) Get rid of the old yeast, so that you may be a new unleavened batch—as you really are. For Christ, our Passover lamb, has been sacrificed.(L) Therefore let us keep the Festival, not with the old bread leavened with malice and wickedness, but with the unleavened bread(M) of sincerity and truth.

I wrote to you in my letter not to associate(N) with sexually immoral people— 10 not at all meaning the people of this world(O) who are immoral, or the greedy and swindlers, or idolaters. In that case you would have to leave this world. 11 But now I am writing to you that you must not associate with anyone who claims to be a brother or sister[c](P) but is sexually immoral or greedy, an idolater(Q) or slanderer, a drunkard or swindler. Do not even eat with such people.(R)

12 What business is it of mine to judge those outside(S) the church? Are you not to judge those inside?(T) 13 God will judge those outside. “Expel the wicked person from among you.”[d](U)

Footnotes

  1. 1 Corinthians 5:5 In contexts like this, the Greek word for flesh (sarx) refers to the sinful state of human beings, often presented as a power in opposition to the Spirit.
  2. 1 Corinthians 5:5 Or of his body
  3. 1 Corinthians 5:11 The Greek word for brother or sister (adelphos) refers here to a believer, whether man or woman, as part of God’s family; also in 8:11, 13.
  4. 1 Corinthians 5:13 Deut. 13:5; 17:7; 19:19; 21:21; 22:21,24; 24:7