Mathayo 2
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Wenye Hekima Waja Kumwona Yesu
2 Yesu alizaliwa katika mji wa Bethlehemu ya Uyahudi wakati Herode alipokuwa mfalme. Baada ya Yesu kuzaliwa, baadhi ya wenye hekima kutoka mashariki walikuja Yerusalemu. 2 Walipofika wakawauliza watu, “Yuko wapi mtoto aliyezaliwa ili awe Mfalme wa Wayahudi? Tuliiona nyota ilipochomoza na kutuonesha kuwa amezaliwa. Nasi tumekuja ili tumwabudu.”
3 Mfalme Herode aliposikia haya, yeye pamoja na watu wote wakaao Yerusalemu walikasirika sana. 4 Herode aliitisha mkutano wa wakuu wote wa makuhani wa Kiyahudi na walimu wa sheria. Akawauliza ni wapi ambapo Masihi angezaliwa. 5 Wakamjibu, “Ni katika mji wa Bethlehemu ya Yuda kama ambavyo nabii aliandika:
6 ‘Bethlehemu, katika nchi ya Yuda,
wewe ni wa muhimu miongoni mwa watawala wa Yuda.
Ndiyo, mtawala atakayewaongoza
watu wangu Israeli, atatoka kwako.’”(A)
7 Kisha Herode akawaita na kufanya mkutano wa siri na wenye hekima kutoka mashariki. Akaelewa kwa usahihi wakati walipoiona nyota. 8 Kisha akawaruhusu waende Bethlehemu. Akawaambia, “Nendeni mkamtafute mtoto kwa makini na mtakapompata mrudi na kunipa taarifa mahali alipo, ili nami pia niende kumwabudu.”
9 Wenye hekima walipomsikiliza mfalme, waliondoka. Waliiona tena ile nyota waliyoiona hapo mwanzo na wakaifuata. Nyota ile iliwaongoza mpaka mahali alipokuwa mtoto na kusimama juu ya sehemu hiyo. 10 Wenye hekima walipoona kuwa nyota ile imesimama, walifurahi na kushangilia kwa furaha.
11 Wenye hekima hao kisha waliingia katika nyumba alimokuwamo mtoto Yesu pamoja na Mariamu mama yake. Walisujudu na kumwabudu mtoto. Kisha wakafungua masanduku yenye zawadi walizomletea mtoto. Wakampa hazina za dhahabu, uvumba na manemane. 12 Lakini Mungu aliwaonya wenye hekima hao katika ndoto kuwa wasirudi tena kwa Herode. Hivyo kwa kutii walirudi nchini kwao kwa kupitia njia nyingine.
Yesu Apelekwa Uhamishoni Misri
13 Baada ya wenye hekima kuondoka, malaika wa Bwana akamjia Yusufu katika ndoto na kumwambia, “Damka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake ukimbilie Misri kwa sababu Herode amedhamiria kumwua mtoto na sasa atatuma watu kumtafuta. Na mkae Misri mpaka nitakapowaambia mrudi.”
14 Hivyo Yusufu alidamka na kutoka kwenda Misri akiwa na mtoto na mama yake. Nao waliondoka usiku. 15 Yusufu na familia yake walikaa huko Misri mpaka Herode alipofariki. Hili lilitukia ili maneno yaliyosemwa na nabii yatimie: “Nilimwita mwanangu atoke Misri.”(B)
Herode Aua Watoto wa Kiume Katika Mji wa Bethlehemu
16 Herode alipoona kuwa wenye hekima wamemfanya aonekane mjinga, alikasirika sana. Hivyo akatoa amri ya kuua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili au chini ya miaka hiyo katika mji wa Bethlehemu na vitongoji vyake. Herode alifahamu kutoka kwa wenye hekima kwamba walikuwa wameiona nyota miaka miwili kabla. 17 Hili likatimiza yale yaliyosemwa na Mungu kupitia nabii Yeremia aliposema:
18 “Sauti imesikika Rama,
sauti ya kilio na huzuni kuu.
Raheli akiwalilia watoto wake,
na amekataa kufarijiwa
kwa sababu watoto wake hawapo tena.”(C)
Yusufu na Familia Yake Warudi Kutoka Misri
19 Wakati Yusufu na familia yake wakiwa Misri, Herode alifariki. Malaika wa Bwana akamjia Yusufu katika ndoto 20 na akamwambia, “Damka! Mchukue mtoto na mama yake urudi Israeli, kwani waliojaribu kumwua mtoto wamekwisha kufa.”
21 Hivyo Yusufu alidamka na kumchukua mtoto Yesu na mama yake na kurudi Israeli. 22 Lakini Yusufu aliposikia kuwa Arkelao alikuwa mfalme wa Yuda baada ya baba yake kufa, aliogopa kwenda huko. Lakini baada ya kuonywa na Mungu katika ndoto, Yusufu aliondoka pamoja na familia yake akaenda sehemu za Galilaya. 23 Alikwenda katika mji wa Nazareti na kukaa huko. Hii ilitokea ili kutimiza maneno yale yaliyosemwa na manabii. Mungu alisema Masihi angeitwa Mnazareti.[a]
Footnotes
- 2:23 Mnazareti Mtu anayetoka katika mji wa Nazareti. Jina hili linafanana na neno la Kiebrania linalomaanisha “tawi”. Hivyo inawezekana Mathayo anamaanisha ahadi ya “tawi” la ukoo wa Daudi. Tazama Isa 11:1. Yer 23:5; 33:15; Zek 3:8; 6:12.
Matthew 2
New King James Version
Wise Men from the East
2 Now after (A)Jesus was born in Bethlehem of Judea in the days of Herod the king, behold, [a]wise men (B)from the East came to Jerusalem, 2 saying, (C)“Where is He who has been born King of the Jews? For we have seen (D)His star in the East and have come to worship Him.”
3 When Herod the king heard this, he was troubled, and all Jerusalem with him. 4 And when he had gathered all (E)the chief priests and (F)scribes of the people together, (G)he inquired of them where the Christ was to be born.
5 So they said to him, “In Bethlehem of Judea, for thus it is written by the prophet:
6 ‘But(H) you, Bethlehem, in the land of Judah,
Are not the least among the rulers of Judah;
For out of you shall come a Ruler
(I)Who will shepherd My people Israel.’ ”
7 Then Herod, when he had secretly called the [b]wise men, determined from them what time the (J)star appeared. 8 And he sent them to Bethlehem and said, “Go and search carefully for the young Child, and when you have found Him, bring back word to me, that I may come and worship Him also.”
9 When they heard the king, they departed; and behold, the star which they had seen in the East went before them, till it came and stood over where the young Child was. 10 When they saw the star, they rejoiced with exceedingly great joy. 11 And when they had come into the house, they saw the young Child with Mary His mother, and fell down and worshiped Him. And when they had opened their treasures, (K)they presented gifts to Him: gold, frankincense, and myrrh.
12 Then, being divinely warned (L)in a dream that they should not return to Herod, they departed for their own country another way.
The Flight into Egypt
13 Now when they had departed, behold, an angel of the Lord appeared to Joseph in a dream, saying, “Arise, take the young Child and His mother, flee to Egypt, and stay there until I bring you word; for Herod will seek the young Child to destroy Him.”
14 When he arose, he took the young Child and His mother by night and departed for Egypt, 15 and was there until the death of Herod, that it might be fulfilled which was spoken by the Lord through the prophet, saying, (M)“Out of Egypt I called My Son.”
Massacre of the Innocents
16 Then Herod, when he saw that he was deceived by the wise men, was exceedingly angry; and he sent forth and put to death all the male children who were in Bethlehem and in all its districts, from two years old and under, according to the time which he had determined from the wise men. 17 Then was fulfilled what was spoken by Jeremiah the prophet, saying:
18 “A (N)voice was heard in Ramah,
Lamentation, weeping, and great mourning,
Rachel weeping for her children,
Refusing to be comforted,
Because they are no more.”
The Home in Nazareth(O)
19 Now when Herod was dead, behold, an angel of the Lord appeared in a dream to Joseph in Egypt, 20 (P)saying, “Arise, take the young Child and His mother, and go to the land of Israel, for those who (Q)sought the young Child’s life are dead.” 21 Then he arose, took the young Child and His mother, and came into the land of Israel.
22 But when he heard that Archelaus was reigning over Judea instead of his father Herod, he was afraid to go there. And being warned by God in a (R)dream, he turned aside (S)into the region of Galilee. 23 And he came and dwelt in a city called (T)Nazareth, that it might be fulfilled (U)which was spoken by the prophets, “He shall be called a Nazarene.”
Footnotes
- Matthew 2:1 Gr. magoi
- Matthew 2:7 Gr. magoi
© 2017 Bible League International
Scripture taken from the New King James Version®. Copyright © 1982 by Thomas Nelson. Used by permission. All rights reserved.
