耶稣复活

16 过了安息日,抹大拉的玛丽亚、雅各的母亲玛丽亚和撒罗米买了香料,要去抹耶稣的遗体。 周日清早,太阳刚刚升起,她们就去坟墓那里。 途中她们彼此议论说:“谁能替我们滚开墓口那块大石头呢?” 她们抬头一看,那块大石头已经滚到一旁。 她们进了坟墓,看见一位身穿洁白长袍的青年坐在右边,吓了一跳。 那青年对她们说:“不要害怕,你们要找那位被钉十字架的拿撒勒人耶稣吗?祂已经复活了,不在这里。你们看!这是安放祂的地方。 你们快回去,告诉祂的门徒,特别是彼得,‘祂先你们一步去了加利利,你们将在那里见到祂,正如祂以前所说的一样。’”

她们从坟墓出来,跑走了,战战兢兢,疑惑不已,什么也没有告诉他人,因为她们很害怕。

耶稣显现

耶稣在周日清晨复活后,首先向抹大拉的玛丽亚显现,耶稣曾在她身上赶出七个鬼。 10 玛丽亚赶到门徒那里,看见他们仍然在哭泣哀悼, 11 就告诉他们耶稣已经复活了,还向她显现过,但他们不相信。

12 此后,有两个门徒在去乡下的路上,看到耶稣以另一种形象向他们显现。 13 他们回去告诉其他的门徒,但门徒还是不相信。

最后的使命

14 后来,当十一位门徒在一起吃饭的时候,耶稣向他们显现,责备他们又不信又固执,因为他们不肯相信那些人在祂复活后见过祂。 15 耶稣又对他们说:“你们要到世界各地去,向全人类传扬福音。 16 相信并接受洗礼的人必定得救,不肯相信的人必被定罪。 17 必有神迹随着信我的人,他们能奉我的名赶鬼,说新的方言, 18 又能用手拿蛇,万一喝了什么毒物,也不会受害。他们把手按在病人身上,病人就可痊愈。” 19 主耶稣说完这些话,就被接回天上,坐在上帝的右边。 20 门徒出去到处传扬福音,主和他们一同工作,借着神迹证实他们所传的道。

Yesu Amefufuka Kutoka Mauti

(Mt 28:1-8; Lk 24:1-12; Yh 20:1-10)

16 Sabato ilipomalizika, Mariamu Magdalena, Maria mama yake Yakobo, na Salome wakanunua manukato yenye harufu nzuri ili kuyapaka kwenye mwili wa Yesu. Alfajiri na mapema Jumapili, mara tu baada ya jua kuchomoza, walienda kwenye kaburi la Yesu. Nao walikuwa wakiambiana wao kwa wao, ni nani atakayelivingirisha jiwe litoke katika mlango wa kaburi kwa ajili yetu?

Kisha wakatazama juu na wakaona kuwa jiwe lile kubwa lilikuwa limevingirishwa tayari litoke mlangoni mwa kaburi la Yesu. Walipoingia kaburini, wakamwona kijana mmoja ameketi upande wa kulia naye alikuwa amevaa vazi jeupe, nao wakastaajabu.

Naye akamwambia, “Usistaajabu. Unamtafuta Yesu wa Nazareti, aliyesulubiwa? Tazama amefufuka! Hayupo hapa. Angalieni mahali walipokuwa wameweka mwili wake. Hata hivyo nendeni na kuwaeleza wafuasi wake pamoja na Petro kwamba: ‘Ametangulia mbele yenu kuelekea Galilaya. Mtamkuta kule, kama alivyowaambia.’”

Kwa hiyo wale wanawake walitoka na kukimbia kutoka kaburini, kwa sababu hofu na mshangao ulikuwa umewajia. Nao hawakusema chochote kwa mtu yeyote kwani waliogopa.[a]

Baadhi ya Wafuasi Wamwona Yesu

(Mt 28:9-10; Yh 20:11-18; Lk 24:13-35)

Baada ya Yesu kufufuka alfajiri na mapema siku ya Jumapili, alimtokea kwanza Maria Magdalena, ambaye awali alifukuza mashetani saba kutoka kwake. 10 Baada ya Mariamu kumwona Yesu, alienda na kuwaeleza wanafunzi wake. Walikuwa wamehuzunishwa sana na walikuwa wakilia. 11 Lakini Mariamu aliwaambia kwamba Yesu yu hai. Aliwaambia ya kwamba yeye amemwona, lakini wao hawakumwamini.

12 Baada ya hayo, Yesu kwa namna tofauti akawatokea wanafunzi wake wawili walipokuwa wakitembea kuelekea mashambani. 13 Hawa kisha walirudi na wakawasimulia wengine wote, lakini nao hawakuwaamini.

Yesu Awatokea Wafuasi Wake

(Mt 28:16-20; Lk 24:36-49; Yh 20:19-23; Mdo 1:6-8)

14 Baadaye, Yesu aliwatokea wale mitume kumi na mmoja walipokuwa wakila. Naye akawakaripia kwa kutokuwa na imani. Walikuwa wakaidi na walikataa kuwaamini wale waliomwona Yesu baada ya kufufuka kwake.

15 Naye akawaambia, “Nendeni ulimwenguni pote, na mkahubiri Habari Njema kwa uumbaji wote. 16 Yeyote atakayeamini na kubatizwa ataokolewa, lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa. 17 Na wale waaminio wataweza kufanya ishara hizi kama uthibitisho: watafukuza mashetani kwa jina langu; watasema kwa lugha mpya wasizojifunza bado; 18 watakamata nyoka kwa mikono yao; na ikiwa watakunywa sumu yoyote, haitawadhuru; wataweka mikono yao kwa wagonjwa, nao watapona.”

Yesu Arudi Mbinguni

(Lk 24:50-53; Mdo 1:9-11)

19 Hivyo baada ya Bwana Yesu kuzungumza nao, alichukuliwa mbinguni, kuketi katika mkono wa kuume wa Mungu. 20 Na mitume wakatoka na kwenda kuhubiri kila mahali, na Bwana alifanya kazi pamoja nao akithibitisha kuwa ujumbe wao ni wa kweli kwa ishara zilizofuatana na mahubiri yao.

Footnotes

  1. 16:8 Kitabu kinaishia hapa katika nakala mbili za zamani za Kiyunani zilizopatikana. Nakala chache nyingine za baadaye zina mwisho huu mfupi: “Lakini mara wakampa maagizo yote Petro na wale waliokuwa pamoja naye. Kisha Yesu mwenyewe akawatuma watoke na kwenda mashariki na magharibi wakiwa na ujumbe mtakatifu ambao kamwe hautabadilika; kwamba watu wataokolewa milele.”